Monday, 6 October 2025

MAMBO YA KUFANYA ILI KUVUKA KIPINDI CHA KUKATALIWA BILA WEWE KUDHURIKA

Kukataliwa sio kitu kigeni kwa sababu uzoefu unaonyesha karibu kila mtu ameshaonja kipindi hiki na hata kama bado basi kuna siku utakipitia .

Inaweza kuwa ndugu, marafiki, makazini au katika mahusiano kote kuna kakataliwa .

Ni kipindi kigumu sana kukabiliana nacho kwa sababu ki asili binadamu tunapenda kukubaliwa hivyo ianapotokea kukataliwa maumivu yake huwa ni makali sana bila kuwa na  ukomavu athari huwa kubwa ikiwemo na kujitoa/kutoa uhai .

UFANYEJE SASA UKIWA KWENYE KIPINDI HICHO?

1.Kubali ukweli (Ukiruka hii hatua utakuwa unajidanganya kuwa uko sawa ila ki uhalisia bado unateseka hivyo lazima ukubali kuwa HAKUTAKI)

2.Ondoa matumaini kuwa kuna siku ATAJIRUDI ( Usiwe na hayo matumaini kwa kuamini ipo siku atajirudi ukaanza kuwa unamtumia meseji mara unamjulia hali au kuendelea kumshirikisha mambo yako kwa tumaini kuwa atakuonea huruma arudi , utateseka)

3.Usitake umsahau kwa kutafuta mbadala wake( kosa kubwa sana hili )

4.Wekeza nguvu kwenye mambo mengine na futa matukio ambayo yatafanya umkumbuke ikiwemo picha kama mlipiga wote au kusikia nyimbo ambazo mlizipenda kwa pamoja)

5.Usijione mwenye kasoro za kukataliwa ( usianze kutafuta sababu za kujiona hufai)

6.Usianzishe maigizo ya kuaminisha watu kuwa upo sawa na soko lako lipo juu 

7.Muda ndio kidonge cha mwisho kumaliza maumivu yako( Huwezi kuwa sawa kesho itachukua muda hivyo kubali hilo)

8.SHUKURU MUNGU KUKATALIWA KWA SABABU KUNA SEHEMU KAKUANDALIA YA KUKUBALIWA 🙏 


NB : KUCHELEWA KUKUBALI KUKATALIWA NI KUENDELEA KUJICHELEWESHA WEWE MWENYEWE 😔 

#Mwanasayansi Saul kalivubha 

#Fikia Ndoto Zako 

+255652 134707

Thursday, 26 June 2025

UTULIVU NI JICHO LA TATU KUKUPA MAAMUZI SAHIHI HASA KWENYE NYAKATI ZA KUVURUGWA

 

Walioachwa kwenye mahusiano wakakurupukia mengine haraka wakiwa kwenye hali ya  kuvurugwa wengi  wao walijikuta wakikosea tena vibaya zaidi ya mwanzo.

Waliofumania wenzi wao au kusikia taarifa mbaya dhidi ya wenzi wao na wakafanya maamuzi wakiwa kwenye hali ya kuvurugwa wengi walijikuta kwenye maamuzi mabaya na yenye majuto kama vile kuua au kujiua.

Waliojibizana wakiwa kwenye hali ya kuvurugwa wengi walijikuta wakiongea maneno ya hovyo na yaliyokosa hekima kiasi cha kujipotezea heshima. 


Furaha na huzuni vyote vinaweza kupoteza utulivu wako na utulivu ukipotea basi tarajia maamuzi ya hovyo kwa asilimia kubwa. 

Adui wabobevu wanalijua hilo ndio maana wakitaka kukushambulia kirahisi basi watatafuta namna ya kukuvuruga na kukushinikiza ufanye maamuzi ukiwa kwenye huo mvurogo wakiamini ni lazima utakosea tu.

Utulivu ndio silaha pekee kwenye nyakati kama hizo na hapo utapata jicho la tatu la kuona hali halisi na maamuzi gani uchukue .

#Mwanasayansi Saul kalivubha 

#Fikia Ndoto Zako

#Mitandaoni @Fikia Ndoto Zako 

Wednesday, 14 August 2024

UKIZALIWA FAMILIA MASKINI JUA TAYARI UMEKUWA JESHI LA MTU MMOJA MSITUNI

 UKIZALIWA FAMILIA MASKINI JUA TAYARI UMEKUWA JESHI LA MTU MMOJA MSITUNI, ACHA KUDEKA. 

Maisha hayako sawa hilo lazima tukubali   na usipolikubali basi utashindwa kupambana kulingana na mwanzo wako ulivyo , Kwa mfano kuna kuna ambao wanarithishwa mali waendeleze na kuna wanaorithishwa matatizo wayatatue.

Kuna ambaye akipata kazi tu hupongezwa kwa kupewa  kiwanja cha nyumba ama fungu la pesa na kuna wewe ambaye ukipata kazi tu matatizo yanaongezeka yaani utatakiwa ujengee wazazi, usomeshe watoto wa ndugu zako na kisha ndio uanze kujiimarisha .

Wewe ambaye simu zote unazopigiwa ni za matatizo usijilinganishe na ambaye hupigiwa simu kwa kukumbukwa, Wewe ni jeshi la mtu mmoja tayari hivyo usitegemee msaada wowote wa kivita kutoka nyuma wala mbele hivyo ni kupambana tu mpaka kieleweke .

Mambo ya kudeka waachie wenyewe ila wewe tambua ukifeli ndugu zako wataumia zaidi kuliko hata wewe muhusika kwa sababu umebeba matumaini ya wengine .

Kila siku historia ya ulipotoka iwe inakukumbusha kuwa WEWE NI JESHI LA MTU MMOJA MSITUNI. 

#Mwanasayansi Saul kalivubha.

#Fikia Ndoto zako 

+255652 134707

Thursday, 1 August 2024

MASKINI ATABAKI KUWA MASKINI TU KAMA ATAENDELEA KUWA NA MARAFIKI MASKINI 😔

 MASKINI ATABAKI KUWA MASKINI TU KAMA ATAENDELEA KUWA NA MARAFIKI MASKINI 😔


Hii sio makala nzuri kwa maskini ambao wameridhika na hali hiyo  hivyo kama umeridhika na umaskini basi acha kabisa kusoma ila kama upo kwenye vita ya kujikwamua kama mimi basi inawezekana ikawa makala yenye mwanzo mpya kwako. 

Ukipokea simu kutoka kwa maskini iwe ni ukoo wako au rafiki zako huko kijijini kama sio ya kukuomba pesa basi itakuwa ya majungu tu, mtaongea majungu kisha mtaagana na baada ya hapo kila mmoja atabaki anatafakari hayo majungu mpaka usiku utafika mtalala na siku itakuwa imeisha hivyo , kweli hapo umaskini utaisha?


Ajabu ni kuwa huyo aliyekupigia simu kwa zaidi ya nusu akikupa majungu siku ikitokea fursa inayohitaji mtu wa sifa yako hatokupa na siku ukijua ukamuuliza atakwambia hakuwa na salio ( vocha ) siku hiyo , Inashangaza na kuchekesha kidogo .



Umaskini ukiwa damuni huwa wahusika wanapendana wakiwa na umaskini wao ila wana wivu mkali siku wakisikia una mipango ya kutaka kuagana na umaskini.

Ukitaka kujua hilo wapelelee habari nzuri maskini rafiki zako utachopkea kwa asilimia kubwa ni kukatishwa tu tamaa kwa kupewa mifano ya watu waliokuwa kama wewe ila wanashindwa na na huo ni ujumbe kwako kuwa achana na mipango hiyo na kwa sababu unaogopa usiwapoteze marafiki zako basi unaamua kuwasikiliza na kughairi harakati zako za kuagana na umaskini. 

Waepuke maskini wa namna hiyo kwa kila hali , hili haliwezekani kwa maskini wanaopenda kuwa maskini ila ni rahisi kwa maskini ambao wapo kwenye harakati za kujikomboa ndio maana awali nilikatunguliza hii makala haiwahusu maskini walioridhika kwa umaskini wao.

KWANINI UWAEPUKE MASKINI?

Kwa sababu wengi wao ( sio wote) watakuwa wanakujaza majungu tu na sio kukupa fursa( njia za kujikwamua)  na usipokuwa makini watakufanyia kitu kibaya endapo wakijua una mipango mizuri ya kuwa tajiri.


Mwanasayansi Saul kalivubha 

Instagram @fikia ndoto zako 

+255652 134707

Thursday, 11 July 2024

HII NDIO KANUNI YA KIJASUSI YA KUISHI NA WATU AMBAO HAWATAKI KUONA WENGINE WAKIFANIKIWA

 KIJASUSI WAPE USHINDI WALEWE ILI WAACHE KUKUFUATILIA BALI WASHANGAZWE KWA MATOKEO.


Jasusi yoyote Duniani huwa habishani na mtu zaidi atakubaliana na wewe ili uvimbe kichwa lakini moyoni mwake hajakubali na kitachokushangaza ni matokeo. 

Hii ni mbinu moja wapo ya kuishi na watu ambao hawataki wengine wafanikiwe kwa kujiona wao ndio wanajua kila kitu , ukisema ujionyeshe ni zaidi yao kwa maneno watakufuatilia sana ili kuzima harakati zako hivyo wewe wape ushindi tu .

Sifa kubwa ya wajuaji kama hao huwa wanapenda sana sifa na kuonekana wao ni zaidi ya yeyote na siri kubwa kuhusu watu hawa huwa wanalewa sifa yaani wakipewa sifa tu tayari wanajisahau hivyo tumia madhaifu haya kuishi nao.

Ukiwapa ushindi watakuona wewe ni bwana mdogo tu na hata siku moja hutokuwa juu sasa kipindi wanashangalia kwa kukuona hivyo wewe pambana kwani hawatakuwa na umakini kwako wakijua tu wewe ni wa kushindwa.

Wakikwambia wao ndio wa mjini na hakuna wa kuwashnda wewe wakubalie kuwa ni kweli wapo hivyo ila ki uhalisia unawaona kabisa hawana lolote ila majigambo tu na huo utakuwa muda mzuri sana kufanya vitu vikubwa bila wao kukufuatilia.

Kwanini hawakufuatilii? Kwa sababu umwapa ushindi hivyo wanajiona washindi na kukuona wa kushindwa tu, Tumia huo muda vizuri. 


#Mwanasayansi Saul kalivubha 

#Fikia Ndoto zako 

+255652 134707

Thursday, 4 July 2024

UKIMILIKI PESA UMEMILIKI HISIA ZA KUJIAMINI NA UKIKOSA BASI UMEPOTEZA SEHEMU YA KUJIAMINI.

 UKIMILIKI PESA UMEMILIKI HISIA ZA KUJIAMINI NA UKIKOSA BASI UMEPOTEZA SEHEMU YA KUJIAMINI.

Linapokuja suala la umiliki wa pesa basi tunazungumzia hisia ziletwazo  na pesa ambavyo kwa namna yoyote unatakiwa hisia hizo zisikushinde bali uzitawale.Wengi hatutafuti pesa kama zilivyo karatasi bali tunatafuta ile hisia ambayo mtu anakuwa nayo akiwa na pesa ndio maana leo hii mtu akiwa na pesa kuna namna atajihisi hata akivaa hovyo hatahisi aibu kwa sababu anajua mtaona kaamua kufanya hivyo ila mtu akikosa pesa kitu cha haraka atachohisi ni aibu na hata kutamka mbele za watu kuwa hana pesa anaweza kushindwa kwa aibu .

Hisia kubwa ileteayo na pesa ni kujiamini na hapo ndipo inatakiwa mtu uwe na nguvu kubwa kuliko hisia itokanayo na pesa bila kujali una pesa ama huna.

Kwa sababu hisia ya kuwa na pesa ikikupa maamuzi ndio utaanza kufanya mambo ya kushangaza na sio kwamba ni mazuri bali ya hovyo kwani utakuwa mtumwa wa pesa.

Vipo viashiria vingi kuwa mtu fulani ni mtumwa pesa na hasa tunaangalia matumizi yake na matendo afanyayo muhusika kama vile:

Ulimbukeni kwenye starehe ambapo muhusika utamuona akitumia pesa bila kuinoea huruma pesa.

Kuanzisha vurugu zisizo na lazima ilimradi tu ujulikane kuwa chanzo ni wewe na tena kwa sababu tu una pesa.

Kuanzisha vitendo vya hovyo kama vile dhuluma kwa wanyonge kwa kutumia nguvu ya pesa ukiwa unasmini hata utatumia pesa kununua haki kama ikitokea unashitaakiwa.

Kibaya zaidi ukiongozwa ba hisia za pesa utakuwa na siku za kuhesabika kwenye umiliki wa pesa kwa sababu utakuwa mwenye matumizi mengi yasiyo na lazima na huo ndio utakuwa mwanzo wa kufilisika 

Je inakuwaje kwa mtu ambaye hana pesa? Kukosa pesa ni mwanzo wa kupoteza hisia za kujiamini na hapo utaingiwa na tatizo la kujishtukia kwa mambo ambayo hata hayapo kama vile:

Usiposalimiwa unahisi ni sababu huna pesa ndio maana hata baadhi ya watu hawakupi salaam zao lakini inawezekana tu hawakusalimii kwa sababu zao binafsi na sio sababu huna pesa.

Ukiambiwa ukweli unaona kama vile  unafokewa kwa sababu huna pesa lakini ukweli ni kuwa wanakuonya tu ili uwe kwenye uelekeo mzuri tu na sio sababu huna pesa.

Ukiachwa kwenye mahusiano kwa sababu hata  nyingine kabisa wewe tayari unajua ni vile tu huna  pesa ndio maana umeachwa.

Kanisani/misikitini au kwenye jamii usipopewa uongozi unajua tayari wamekuona huna pesa ndio maana hawakupi uongozi kumbe hata yawezekana wana sababu zao tofauti na unavyojifikiria na muda wote unahisi kuna watu wana  njama mbaya na wewe. 

Muda wote unajitetea kwa kutumia hali yako ya kukosa pesa na hapo ndipo unakuwa unajipotezea heshima yako.

Unaona watu wanakunyima makusudi pesa ili  kukukomoa ,huamini kama na wao hawana.

Dhibiti hisia za umiliki wa pesa au ukosefu wa pesa na ukiliweza hilo basi pesa itakuwa rafiki yako na hata kama huna basi nguvu ya kutafuta itakujia kwani huathiriwi na hisia zake za kutokuwa nayo.

Acha kuunganisha kila tukio na kukosa kwako pesa bali tambua kuwa matukio mengine yangetokea tu  hata kama ungekuwa na hizo pesa. 

Usiruhusu kila mtu ajue hali yako kiuchumi , Shirikisha baadhi ya watu kuhusu hali yako na uwe umejiaminisha kuwa kweli hao ni watu wa maana na busara

Usijitetee sana kwa kutumia hali yako ya ukosefu wa pesa pia usisahau kutafuta pesa ili usiwe mtu wa kujishtukia

Mwanasayansi Saul kalivubha

+255652 134707

Sunday, 23 June 2024

USIFANYE WATOTO WAKO WACHUKIE WAJOMBA NA BABA ZAO WADOGO KWA SABABU YA MATATIZO YAKO.

 USIFANYE WATOTO WAKO WACHUKIE WAJOMBA NA  BABA ZAO WADOGO  KWA SABABU YA MATATIZO YAKO.

Kuhudumia watoto wako ni jukumu lako kwa 100% na tena hutakiwi kulalamika kwenye hilo kwa sababu hawakukulazimisha uwazae  , ikitokea kuna mtu anakusaidia shukuru na isipotokea hayupo usilaumu maana hilo ni jukumu lako wewe kwa 100% na sio vinginevyo.

Usifanye watoto zako wawachukie wajomba na Baba zao wadogo bure kwa sababu ya matatizo yako kwa sababu wewe ndio unatakiwa uwe mstari wa mbele kuwapa malezi bora na mahitaji yote ya msingi hata ukikwama basi angalau uwe umetimiza kwa 90% na ikitokea unasaidiwa iwe kwa 10% tu na tena mshukuru huyo atakayejitoa kufanya hivyo kwa sababu kaingilia majukumu yako 

Ukishindwa kuwasomesha watoto zako basi  wakulaumiwa ni wewe sio uanze kutafuta nani wa kumtupia lawama na hapa wazazi wengi hukosea kwa kuaminisha watoto zako kuwa wameshindwa kusoma shule nzuri kwa sababu ya wajomba ama Baba wadogo hawakuwasaidia na wana maisha mazuri, swali ni je hilo ni jukumu lao? Hapana hilo ni jukumu lako wewe usikwepe kulaumiwa.

Wakikuta milo yako ni ya kubahatisha wa kulaumiwa ni wewe kwa 100% na sio walioshindwa kukusaidia kwa sababu mtoto hakukulazimisha umzae la sivyo kama ilitokea umebakwa au kubambikiziwa mtoto hapo kweli kuna haja ya kusaidiwa kwa sababu imekuwa dharura ila tofauti na hivyo watoto sio dharura hivyo hutakiwi kulaumu wengine bali kujilaumu kutofanya maandalizi na kama mzazi sio vizuri kuuza majukumu yako pengine bali wajibika mwenyewe.

Wakikuta una chumba kimoja mnabanana humo  wa kulaumiwa ni wewe na sio mjomba wao aliyeshindwa kukusaidia kujenga  nyumba kwa sababu ulijua kabisa watoto wakija watahitaji sehemu ya kulala  hivyo ni wajibu wako kuitafuta hiyo sehemu na sio kulalamika , Kama unajiona kabisa huwezi basi acha mchezo wa kubahatisha kwamba kila mtoto huja na baraka zake bali ruhusu waje watoto ambao unajua fika utawamudu bila kulalamika. 

Kama wangejua hauko tayari kuwahudumia basi wasingechagua kuzaliwa na wewe kama tu wangepewa hiyo nafasi ya kuchagua  na hii ni kutokana na wewe kuwasimanga kwa malezi yako , Sio vizuri mzazi kuona kama unateseka kuwahudumia yaani unalipa ada za shule kwa masimango, unawananulia mavazi kwa masimango na kuwaonyesha kama unawahudumia  ili kesho wakulipe.

Mwanasayansi Saul kalivubha 

+255652 134707