Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya mafunzo ya maisha, nashukuru Mungu kwa kuendelea kutupigania hadi sasa ......karibu.
Kusudi la somo.
Leo nataka tujifunze siri moja ya urafiki ambayo wengi hawajui, au wanaijua lakini hawaitumii. ....mwalimu wangu aliwahi kuniambia kwamba, ikiwa una ujuzi usio kusaidia, ...huna cha kujivunia. ....karibu tuendelee.
SIRI YA KWANZA YA URAFIKI(SIFA YA ZIADA ).
Kwa nini urafiki? ..... utafiti unaonyesha mafanikio yetu yapo ndani ya rafiki zetu wa karibu. ...hii ndio sababu ya mimi kuandika somo hili. .....Siri ya kwanza ni ipi?
Siri ya kwanza kwenye urafiki ni ...sifa ya ziada .....
Sifa ya ziada ni ni sifa ambayo mtu anajiongezea kwa lengo la kumvutia rafiki yake. .. hali hutokea mwanzoni mwa urafiki, .....nini madhara yake?
Kuna watu wapo kwenye urafiki mzuri, ila urafiki huo unaendeshwa na sifa ya ziada ambayo mmoja katika urafiki huo anaitumia. .Mtu ambaye anaitumia sifa ya ziada kuendesha urafiki, anatumia nguvu kubwa sana. ...tena nguvu anayoitumia ina mrudisha sana nyuma kimafanikio na ina mpa madhara ya kisaikolojia. ......!
Je, una uwezo wa kuyaishi maisha yaliyobebwa na sifa ya ziada?
Kila siku tunashuhudia kuvunjika kwa urafiki ambapo sababu kubwa ni mmoja wapo kwenye urafiki kupoteza sifa ya ziada aliyojipatia. ...
Tiba pekee kabla ya kuwa na rafiki, hakikisha unaishi maisha yako. ....be you, be smart. (ishi maisha yako, kuwa nadhifu )....utapata rafiki aina yako.
See you at the top.
scientist Saul kalivubha.
(0652 134 707 )
No comments:
Post a Comment