Wednesday, 31 May 2017

SIRI YA NNE YA URAFIKI

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa mafunzo ya elimu ya maisha kwa lengo la kufikia ndoto zetu,nashukuru mungu kwa kuendelea kunipigania mimi pamoja na wewe...........karibu.


KUSUDI LA SOMO.
Lengo la somo letu la leo ni kujifunza siri ya nne ya urafiki ambayo ni uvumilivu,ili tuwe pamoja jifunze kwanza SIRI YA TATU kwa kubofya hapa.SIRI YA TATU,..........ikumbukwe tu rafiki ana sehemu kubwa sana kwenye ndoto zetu,hii ndio sababu ya mimi kufundisha somo hili.

SIRI YA NNE YA URAFIKI(UVUMILIVU).
Uvumilivu ni uwezo wa kuzitawala hisia zitokanazo na mambo yasiyo pendeza,hisia ambazo zikiruhusiwa zinaweza kuwa hanzo cha matokeo hasi(negatives effects).........kwenye urafiki pia kuna mambo ambayo yanahitaji kuvumiliwa,ndani ya urafiki kuna mambo yasiyopendeza yenye lengo la kuimarisha urafiki,mtu usipo kuwa mvumilivu unaweza kuwapotezamarafiki wengi sana wasio na hatia..............

Uvumilivu katika urafiki unahitajika sana hasa kwenye hali kuu mbili zifatazo:



  • MADHAIFU;watu wengi wanaingia kwenye urafiki wakiwa na picha ya madhaifu machache waliyo yaona kabla ya kuanza urafiki,ila kuna madhaifu mengine ya ndani ambayo huwezi kuyaona hadi uingie kwenye urafiki,......usipokuwa mvumilivu ,madhaifu haya ya ndani yana nguvu kubwa ya kuvunja urafiki.

  • CHANGAMOTO:Changamoto ni moja ya sehemu muhimu sana ya urafiki,ni sehemu ambayo inahitaji uvumilivu wa hali ya juu,pia ni sehemu ambayo inahitaji matumizi ya hekima na busara,maanakila changamoto ina jambo la kufundisha kwenye urafiki wako.....kuna usemi mmoja unasema "Kama upo kwenye urafiki usio na changamoto yoyote ile,kaa chini ufikirie tena mara ya pili"

              See you at the top.
          Scientist Saul kalivubha.
                (0652 134707)

No comments:

Post a Comment