Friday, 16 February 2018

KWA NINI RAFIKI YAKO HAKUAMINI?

Tarehe 22 FEBRUARY ni siku ambayo nasherehekea siku ya kuzaliwa kwangu......pamoja na furaha yote ya siku hiyo,huwa ni siku pia ambayo nimejiwekea utaratibu wa kukumbuka mambo ambayo yalitokea kwenye safari yangu ya maisha......kiufupi safari yangu kwa asilimia kubwa ilikuwa ya maumivu......hapo ndipo nakumbuka nafasi ya rafiki katika maisha yangu........karibu.

KUSUDI LA SOMO.

Lengo la somo hili ni kutaka kutoa majibu ya kwa nini huna imani na rafiki yako?.....au kwa nini yeye hakuamini?.....hii ni vita kubwa sana ambayo inayumbisha urafiki wa watu wengi na kusababisha kifo cha urafiki..........karibu.

KWA NINI HUNA IMANI NARAFIKI YAKO?.......Sabubu za kwa nini humuanini rafiki yako zipo sawa na kwa nini yeye hakuamini.........hivyo ngoja nielezee sababu zinazo fanya ukose imani na rafikiyako.....kisha utazigeuzia upande wa pili.

1.HISTORIA YAKE.......kufahamu historia ya rafiki yako sio vibaya.na inaweza isiwe hatari kabisa kwa yeye kuptia historia hiyo...tatizo liko wapi?.........hadi wewe kukubali kuwa na urafiki na mtu unayejua historia yake,ni wazi uliamini kuwa kabadilika....lakini kubadilika kwake haina maana kuwa attaishi bila madhaifu yoyote yale........kosa lipo pale ambapo utaanza  kuunganisha madhaifu yake ya kawaida na maisha aliyopitia.....ukiruhusu hali hiyo,nakuhakakishia,hutomuamini hata kidogo,utakuwa mtu wa wasiwasi tu muda wote......ukiona huna busara ya kubeba historia ya nyuma ya rafiki yako,au umejiaminisha kuwa bado hajabadilika......kuwa mbali.

2.HISTORIA YAKO,.....Usipokuwa mwenye hekima na busara,kile unachokitenda au umechotendewa au kuona wengine wakitendewa,kitakufanya uamini watu wote duniani wapo hivyo.....hali hii ukiiruhusu,itakufanya ujihami.....unajua madhara ya kujihami?.......KWANZA wewe mwenyewe utakuwa sio muaminifu,pili, rafiki yako utampa uhusika wako ....hutomuamini pia........kuna kipindi inabidi uishi bila hamasa za nje,hamasa ambazo ni za mawazo hasi.,,,zitakufanya uingiwe na ugonjwa wa kutoamini watu wasio na hatia............

 Hapa nakumbuka utafiti wangu ambao niliufanya ili kugundua ni kwa namna gani watu hawana imani na marafiki zao sababu zilizosababisha hivyo........nilitumia marafiki wa jinsia tofauti,,,,wavulana kumi ambao nilwaulizwa wanajisikiaje ikitokea simu ya rafiki wake wa kike  haitapokelewa au itakuwa busy(kutumika)  pindi wakiwatafuta.......maatokeo yalikuwa hivi:

SITA walisema ,wakikuta hali hiyo,watahisi kusalitiwa,wawili walisema watajisikia vibaya tu.....wengine wawili wa mwisho walisema hiyo ni hali ya kawaida tu......kwa ufupi utafiti huo unaonyesha ni namna gani uaminifu umepungua ......nilivyofatilia zaidi kwa marafiki hao sita ndipo nikapata somo hili la leo......ndani ya sababu hizo mbili kuna sababu ndogo ndogo nyingi.....


Makala hii imeandikwa na Saul Kalivubha.....Mkurugenzi wa label ya FIKIA NDOTO ZAKO.

                                  06552 134707.


No comments:

Post a Comment