Monday, 10 July 2017

SIRI YA TISA YA URAFIKI

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa mafunzo ya maisha na jinsi ya kufikia ndoto zetu,nashukuru Mungu kwa uzimab wake kwangu ,pia ni imani yangu kuwa wewe ni mzima........karibu.



   KUSUDI LA SOMO.

Tunaendelea na somo letu la siri za urafiki,leo ni siri ya tisa ambayo ni mipaka ya ufahamu,...kabla yakuendelea na somo letu hili,ni vyema ukajifunza kwanza siri ya nane ya urafiki(SIRI YA NANE).,karibu tuendelee.



SIRI YA TISA YA URAFIKI(MIPAKA YA UFAHAMU).

Katika urafiki ni jambo la kawaida sana kufahamu habari za rafiki yako,swala hili ni zuri sana ikiwa unataka kufahamu habari hizo kwa lengo la kudumisha urafiki,ila kuna habari zingine za rafiki yako zinaumiza,kama hauna ujasiri,badala ya urafiki kuimarika,utavunjika......kabla ya kuanza kuzifatilia habari za rafiki yako jitahidi kufahamu haya.

  • Weka mipaka,hakikisha unafahamu mambo yenye fada tu katika ujenzi wa urafiki.
  • Kuwa makini na chanzo cha habari, sio kila chanzo cha taarifa za rafiki yako ni chanzo sahihi.
  • usifatilie habari za rafiki kama kumpeleleza,akijua urafiki wenu utapoteza uaminifu,kuwa mpole na taratibu tu utafahamu mengi kuhusu yeye.
  • Fanyia kazi mambo utayo yafahamu kwa rafiki yako kwa lengo la ujenzi na sio kwa leng la kumuhukumu rafiki yako.


Mwamdishi mmoja wa mambo ya saikolojia aliwahi kuandika kanuni moja muhimu sana ,kanuni hiyo ni hii   "Msongo wa mawazo(Stress) unaongezeka,kila ufahamu unapoongezeka"
Kanuni hii inasaidia kupunguza kufahamu mambo yasiyokuhusu,watu wengi kwenye urafiki wanaishi kwa mawazo kwa sababu tu walifatilia mambo yasiyo wahusu ya rafiki zao.


Kuna mambo sio lazima uyafahamu kutoka kwa rafiki yako,utaumiza kichwa bure tu,tena kibaya zaidi hakuna uwezo wa kuyabadilisha mambo hayo,tena kuyafahamu kwako hakuna faida yoyote kwenye uraki wako .....


                        See you at the top.
                            Saul kalivubha
                               0652 134707.

No comments:

Post a Comment