Karibu tena kwenye blog hii inayotoa elimu ya mafunzo ya maisha na jinsi ya kufikia ndoto zetu,nashukuru Mungu kwa pumzi ambayo amekuwa akitupatia bure,karibu tujifunze.
KUSUDI LA SOMO.
Somo letu la leo linahusu umuhimu wa kutengeza soko kabla ya kuanza safari yoyote ya maisha,....Nafikiri wazo la haraka unaposikia neno soko ni biashara,lakini hapa nina maana zaidi ya soko la biashara,,,kabla ya kuendelea na somo jifunze kwanza somo hili (kwa nini hupigi hatua?).....karibu tuendelee.
MAANA YA NENO SOKO.
Kwa haraka ,soko ni sehemu ya kufanyia mauzo ya bidhaa/kitu flani,soko ni kipimo kizuri cha ubora wa kitu flani,mfano,soko la bidhaa flani likishuka,ni wazi kuwa ubora wa bidhaa hiyo unakuwa umeshuka.........Kwa maana pana zaidi na ambayo nataka ndio iwe sehemu kubwa ya somo letu ni hii,SOKO pia ni kipimo kizuri cha huduma yako,huduma yako inapimwa thamani sokoni,ubora wa huduma yako ndio unafanya soko lako liwe juu au chini.
KWANINI UTENGENEZE SOKO KABLA YA SAFARI?
Nafikiri umewahi kuona au kusikia majina ambayo yalifanya vizuri,ila hadi sasa hivi huyasikii tena,...tatizo ni nini?
Pia utakuwa umewahi kushuhudia mtu flani akianza kwa kasi kubwa na kwa ubora wa juu,ila baadae anapotea,tatizo ni nini?
Pamoja na sababu myingi zinazochangia hali hiyo,ila sababu nyingine kubwa ni watu wengi wanaanza safari bila ya kuandaa aina gani ya watu ambao watawafikia na changamoto zake,unapofahamu huduma yako itafikia watu wa aina gani (soko),itakusaidia uanze maandalizi ya kutosha kuhusu ubora wa huduma yako itayokidhi mahitaji ya watu hao kwenye vipindi tofauti tofauti .
Mazingira yanabadilika,mahitaji pia yana badilika,je umejipanga kuibadilisha huduma yako ili iweze kuendana na mabadiliko hayo?
Kabla ya safari ,hakikisha unatambua vizuri soko lako,tena utengeneze na soko mpya litalopatikana kulingana na mabadiliko yatayotokea,ukiendelea kutoa huduma ya aina moja muda wote,ubora wake utashuka kama ikitokea jamii imebadilika ila wewe hujabadilisha aina ya huduma yako.....TENGENEZA SOKO KABLA YA SAFARI.
Makala hii imeandikwa na Saul Kalivubha.
mkurugenzi wa fikia ndoto zako label
0652 134707.
No comments:
Post a Comment