Wednesday, 27 September 2017

KWA NINI HUPIGI HATUA?

Karibu tena kwenye blog hii  inayotoa elimu ya maisha na  jinsi ya kufikia ndoto zetu,nashukuru Mungu kwa afya yangu ,ni matumaini yangu kuwa na wewe nimzima wa afya(sababu unapumua)..karibu tujifunze............

KUSUDI LA SOMO.
Lengo la somo letu hili ni kujifunza sababu ambazo zinazuia hatua za watu wengi,mimi pia ni moja ya wahanga wa sababu hizo,kwa muda mrefu nilikuwa nina mawazo makubwa ila sipigi hatua,na mwisho wa siku nayapoteza mawazo yale.....kwa nini hupigi hatua?


Kupiga hatua ni hali ya kutoka sehemu moja kwenda nyingine,kutoka sehemu yenye viwango vidogo,kwenda kwenye sehemu  sehemu yemye viwango vikubwa zaidi,inaaweza kuwa kwenye biashara ,shule,urafiki ,uwekezaji n.k( jifunze elimu ya pesa)......Kuna watu wana mawazo mazuri,juhudi na wanajitahidi kujifunza kila siku ,ila bado hawapigi hatua mbele,bado matokeo wapatayo hayaendani na jinsi wanavyojituma........Tujifunze kupitia baadhi ya vikwazo vinavyozuia kupiga hatua kwetu.

 SABABU ZINAZO FANYA USIPIGE HATUA.

  •  Kuwa na imani kwamba kuna watu wanahitajika kukusaidia ili ufikie hatua flani,hii ni imani ambayo inasababisha watu wemgi wasipige hatua mbele kwa kusubiri aina flani ya watu waje watoe msaada,kwa lugha ya haraka tunasema connection au channels....sawa mafanikio yanahitaji watu,ila hata wewe unaweza kuwa channel kwa watu wengine kwa kujaribu kwako.Bahati ina nguvu kwa mtu mwenye juhudi,....jaribu hadi kwenye sehemu inayohitaji mtu wa kukusaidia,ili akitokea akute upo vizuri ki maandalizi

  • Usiogope makosa,....hapa ndipo kuna watu wenye mawazo mazuri sana na elimu ya kutosha kuhusu jambo flani,ila hawapigi hatua,..kwa nini? Watu wenye ujuzi mwingi mara nyingi hawtaki kuonekana wakikosea,bora waendelee kuwa na ujuzi wao kwenye fikra kuliko kujaribu kwa vitendo,hali hii ndio inafanya mara nyingi walimu kushindwa na wanafunzi wao...Hata uwe na elimu ya viwango vya juu kuhusu jambo flani,bila kuihamisha kwenye vitendo ni sawa na kazi bure,kubali kukosea ili upige hatua mbele kwa kufanya sahihi ,

  • Fanya maamuzi ,hata kama matokeo yake yanaumiza au yanapingwa na rafiki zako wa karibu,kuna watu tayari wanatambua ili kupiga hatua lazima wafanye jambo flani,ila kwa sababu tu jambo hilo linapingwa na marafiki ,wanaamua kuvumilia tu ili kuendeleza mahusiano mazuri ,Maisha ni ya kwako,rafiki wataokukimbia kwa maamuzi yako ya mafanikio ,achana nao,ukifanikwa watatafuta njia ya kutudi tena kwako

  • ,
  • Mafanikio ni haki ya kila mtu,hakuna aliyepangiwa viwango flani,hata wewe unawezakufika,ondo ile imani ya kwamba biashara flani inafanywa na watu flani tu,au ufaulu flani una watu wa aina flani tu,hata wewe umo kwenye watu hao ,,,,hivyo usiache malemgo flani kwa kuwa hakuna mtu wa familia yenu amewahi kufanya hivyo,,,,,,hutopiga hatua'

Makala hii imeandikwa na Saul kalivubha,kwa label ya fikia ndoto zako

No comments:

Post a Comment