Friday 12 January 2018

WAZO LA UJASIRIAMALI.

Karibu sana kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya mafunzo ya maisha na jinsi ya kufikia ndoto zetu,....kwanza nikupongeze kwa kuanza mwaka mpya vizuri,nafahamu kuna mapito mengi,mengine yalikuumiza,mengine yalikupa raha,ila yote na yote kila ulipopita,kuna kitu ulijifunza.........kwa kuanza na mwaka huu ,nimeona vyema nikushirikishe somo letu zuri ambalo kwa sehemu nina amini litakufanya uwe wa tofauti.


KUSUDI LA SOMO.
Somo letu la leo ni wazo la ujasiriamali,somo hili litatupa hatua za kufanya wazo letu lizae matunda,inawezekana kwa muda mrefu umekuwa ukiweka mawazo kuhusu biashara /uwekezaji flani.ila mwisho wa siku unaishia kuwaza tu,wazo lisilotekelezeka ,huwa ni wazo sisilo la kijasiriamali,.....wazo la kijasriamali ni nini?.....karibu tujifunze.



WAZO LA KIJASIRIAMALI.
Hili ni wazo ambalo mwisho wa siku ,linatekelezwa,...wazo la kijasriamali huwa lina hatua zake ili liwe na sifa ya kutekelezeka,..wazo linapotekelezwa ,lazima lilete matokeo,matokeo sio lazima yawe na faida tu,yanaweza kuwa na hasara pia......ila faida ya kuwa na wazo la kijasiriamali ni mafunzo tunayoyapata(iwe ni faida au hasara).............jiulize wazo lako ni lipi?, umelipa hatua zipi?


HATUA ZA WAZO LA KIJASIRIAMALI.
Wazo la kijasriamali,lina lina hatua zake tatu,ambazo ni kama zifatazo;

1.WAZO,hii ni hatua ya kwanza,lazima uwe na wazo,wazo una amini litakufikisha uendapo,wazo hilo inatakiwa litanguliwe na kujitambua........ukijitambue wapi unataka kwenda,temgeneza wazo la kuongoza safari yako,.....mfano wazo la kilimo,ufugaji ,biashra flani,elimu nk.....wazo lipi litakufikisha uendapo?......hapa namaanisha nini ufanye ili ufikie unapotaka kwenda?

2,MAANDALIZI: Ukisha kuwa na wazo tayari,anza maandalizi.....maandalizi ni pamoja na kuweka mikakati itayosaidia kuliwezesha wazo lako,.....fanya tafiti za kutosha,jitahidi utambue uhusiano uliopo kati ya wazo lako na mazingira,,,,hii itakusaidia kutambua kama wazo lako hilo litasaidia kutatua chngamoto za watu?...... wazo lako hilo litakupa uhuru wa kujitegemea kuliko kutegemea?

3.UTEKELEZAJI.
Huu ni muda ambao ni wa utekelezaji tu,.....kosa ambalo wengi tunafanya ni kuchangamya vipindi,....kipindi cha utekelezaji ndio tunafanya maandalizi......mara nyingi watu wanao changanya vipindi,huwa wanaishia kupanga tu...........MUHIMU TU....kumbuka kila hatua lazma utakutana na hofu ,jitahidi tu kupunguza mazingira yenye kukupa hofu,.....hofu ndio chanzo kinachofanya watu waishie kwenye hatua ya kwanza.



     Makala hii imeandikwa na Saul Kalivubha,mkurugenzi wa fikia ndoto zako label.
                             mawasiliano: 0652 134707.