Tuesday 24 October 2017

JITENGENEZEE KESHO YENYE MATUNDA.

Habari za kwako rafiki ambaye tumekuwa pamoja kwenye darasa hili la maisha ,kwa lengo la kusaidia kufikia ndoto zetu,nashukuru Mungu kwa kuendelea kutupigania,karibu tujifunze.

Kusudi la somo.
Leo nataka tujifunze namna tunavyoweza kutengeneza kesho yetu iliyo ndani ya ndoto zetu,somo hili kwa bahati mbaya wengi wanalipata wakiwa tayari wamekosea sana kiasi kwamba kuanza safari upya inakuwa ngumu ,hivyo wanaamua kuendelea na safari isiyo ya aina yao,...tatizo kubwa ni kwamba mazingira yapo kinyume na kesho za watu wengi,hivyo kulipata somo hili na kuliishi,inahitaji ujasiri wa kutosha ,karibu tuendelee(tengeneza soko lako kabla ya safari)

ITAMBUE KESHO YAKO.
Hii ni hatua ya kwanza kabisa ya kuandaa kesho yako,bahati mbaya kwa upande wa Afrika ni watu wachache sana ambao wanafanikiwa kutambua kesho yao mapema,na wanaofanikwa kufanya hivyo ,wanashindwa kuifikia kwa kukusa maandalizi,kwa wenzetu wazungu ,hali ipo tofauti,wao hutambua kesho yao wakiwa na umri mdogo na wanaanza kutengeza mazingira mapema ya kuja kuiishi kesho yao..........Unafikiri kwa nini wao wanaweza?

Bill Gate akiwa na umri mdogo sana,aligundua kuwa anapenda sana kuchezea Computer,alichofanya alitafuta rafiki wa aina yake ambapo walitenga muda wa kuwa wanajifunza zaidi kuhusu computer kwenye Library ya shule,....akiwa na ndoto ya kumiliki company,alitumia muda mwingi kuwa kwenye mazingira yaliyomfanya awe mpya kila siku kwenye kile akipendacho,Je wewe hadi sasa hujagundua unapenda nini?,Je unakuwa mpya kila siku kwenye eneo lako?......Unafikiri tatizo ni  nini?


HALI YA KUSHANGAZA.

  • Watu wengi wanaifahamu mapema sana kesho yao,na wanajua kabisa jinsi ya kufanya ili waje kuishi kesho hiyo,ila tatizo ni uwezo wa kuthubutu unakuwa mdogo,...kama wewe unataka kesho umiliki kampuni,una maandalizi gani sasa?.....jaribu kutengeneza uhusiano wa kile unachokifanya sasa kiwe msaada wa kusaidia ndoto zako za kesho....kuna gharama,ila lazime uzilipe ili kuweza kuifikia kesho yako.

  • Watu wengi wa wengi tunakwepa maumivu kwa kuyahamishia kesho,....kuliko mtu kuanza maandalizi mapema ya kuandaa kesho ya malengo yake,anaona afanye maandalizi hayo kesho,unachokwepa leo nini?......kila siku ifanye iwe ya maandalizi ya kesho yako.

  • Watu wengi tunataka tuifikie kesho iliyo kamilika.....Hapa nakumbuka mwanafunzi mmoja aliwahi kuniambia,safari yake ya maisha itaanza baada ya kumaliza chuo,swali la haraka likanijia,....Atamaliza na umri gani?,kisha nikajiuliza,ina maana huyu mwanafunzi leo yupo anapoteza muda?,maana bado hajaanza safari ya maisha.
Kesho yako inaanza pale ambapo tayari umejitambua upo kwenye safari ya aina gani,kama safari yako inaenda kwenye kumiliki nyumba za kifahari,anza kuzitengeza leo,,,,,huwezi kuzipa ta nyumba hizo kwa siku moja,ujenzi wake unaanza leo,kila siku jitaahidi unapata maarifa ya kutosha kuhusu hizo myumba unazo zihitaji.



Makala hii imeandikwa na Saul Kalivubha,mkurugenzi wa label ya FIKIA NDOTO zako.

                    See You At The Top.
                        0652 134707

Friday 13 October 2017

TENGENEZA SOKO KABLA YA SAFARI.

Karibu tena kwenye blog hii inayotoa elimu ya mafunzo ya maisha na jinsi ya kufikia ndoto zetu,nashukuru Mungu kwa pumzi ambayo amekuwa akitupatia bure,karibu tujifunze.

KUSUDI LA SOMO.
Somo letu la leo linahusu umuhimu wa kutengeza soko kabla ya kuanza safari yoyote ya maisha,....Nafikiri wazo la haraka unaposikia neno soko ni biashara,lakini hapa nina maana zaidi ya soko la biashara,,,kabla ya kuendelea na somo jifunze kwanza somo hili (kwa nini hupigi hatua?).....karibu tuendelee.

MAANA YA NENO SOKO.
Kwa haraka ,soko ni sehemu ya kufanyia mauzo ya bidhaa/kitu flani,soko ni kipimo kizuri cha ubora wa kitu flani,mfano,soko la bidhaa flani likishuka,ni wazi kuwa ubora wa bidhaa hiyo unakuwa umeshuka.........Kwa maana pana zaidi na ambayo nataka ndio iwe sehemu kubwa ya somo letu ni hii,SOKO pia ni kipimo kizuri cha huduma yako,huduma yako inapimwa thamani sokoni,ubora wa huduma yako ndio unafanya soko lako liwe juu au chini.


KWANINI UTENGENEZE SOKO KABLA YA SAFARI?
Nafikiri umewahi kuona au kusikia majina ambayo yalifanya vizuri,ila hadi sasa hivi huyasikii tena,...tatizo ni nini?
Pia utakuwa umewahi kushuhudia mtu flani akianza kwa kasi kubwa na kwa ubora wa juu,ila baadae anapotea,tatizo ni nini?

Pamoja na sababu myingi zinazochangia hali hiyo,ila sababu nyingine kubwa ni watu wengi wanaanza safari bila ya kuandaa aina gani ya watu ambao watawafikia na changamoto zake,unapofahamu huduma yako itafikia watu wa aina gani (soko),itakusaidia uanze maandalizi ya kutosha kuhusu ubora wa huduma yako itayokidhi mahitaji ya watu hao kwenye vipindi tofauti tofauti .

Mazingira yanabadilika,mahitaji pia yana badilika,je umejipanga kuibadilisha huduma yako ili iweze kuendana na mabadiliko hayo?

Kabla ya safari ,hakikisha unatambua vizuri soko lako,tena utengeneze na soko mpya litalopatikana kulingana na mabadiliko yatayotokea,ukiendelea kutoa huduma ya aina moja muda wote,ubora wake utashuka kama ikitokea jamii imebadilika ila wewe hujabadilisha aina ya huduma yako.....TENGENEZA SOKO KABLA YA SAFARI.


Makala hii imeandikwa na Saul Kalivubha.
     mkurugenzi wa fikia ndoto zako label
       0652 134707.