Monday 12 March 2018

JINSI YA KUONGEZA THAMANI KWENYE BIDHAA YAKO.

Karibu sana kwenye blog hii inayotoa mafunzo ya maisha na jinsi ya kufikia ndoto zako,hongera kwa hali uliyo nayo,ipo sababu ya wewe kuwa ivyo.


KUSUDI LA SOMO.
Somo hili ni majibu ya watu ambao kila siku wanaogopa kufanya biashara au kuwekeza kwenye kitu ambacho tayari kinafanywa na wengine,kwa hofu ya kupata soko la kutosha.....karibu upate majibu. Kabla hujaendelea mbele,jifunze( JINSI YA KUTENGENEZA SOKO)........Karibu tuendelee.


JINSI YA KUONGEZA THAMANI KWENYE BIDHAA YAKO.

Mwaka 2016 nilifanya utafiti wenye lengo la kugundua sababu zinazofanya wanakijiji wengi waendelee kulima bila kupata mafanikio ya kutosha,utafiti huu niliufanya kwenye kijiji kimoja mkoani Morogoro,,,,,pamoja na mengi niliyoyapata,yapo mambo mambo muhimu matatu ambayo wengi wetu tunakosea hadi kufanya soko liwe changamoto kubwa.


Jitahidi uongeze thamani ya pili kwenye bidhaa yako.mfano,kama una unaona kila mtu ana duka la mbolea,wewe fanya kinyume toa ushauri wa jinsi ya kutumia hiyo mbolea......watu watakuja kupata ushauri huo,wakiridhika ,ni ngumu wakanunue mbolea sehemu nyingine tofauti na kwako.


Usiingize bidhaa yako sokoni ukiwa na shida inayohitaji utatuzi wa haraka.....utajikuta unatumia mbinu ya kuishusha thamani ya bidhaa yako kwa kuiuza kwa bei ya chini,....wanakijiji wengi huingia kwenye kilimo ili watatue matatizo yao kwa haraka,mwisho wa siku wanajikuta wanauza mazoa yao kwa bei yoyote ile,tena wanauza haraka baada tu ya kuvuna......!


Ifanye bidhaa yako kuwa adimu,unaifanya vipi?......hapa unafanya bidhaa yako iwe inapatikana kwa utaratibu ambao wengi hawaufanyi,fatilia wateja wnapata usumbufu gani hadi kuja kuipata bidhaa yako......wapunguzie usumbufu huo....mfano badala ya kuwauzia sabuni kwenye gazeti,wauzie kwenye mfuko mweusi.


Makala hii imeandikwa na Saul Kalivubha,mkurugenzi wa label ya fikia ndoto zako.

0652 134707

Friday 2 March 2018

MAPATO ,MATUMIZI YENYE KURUHUSU UWEKEZAJI.



Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya mafunzo na jinsi ya kufikia ndoto zetu....nina imani kwa namna yoyote ile ,unaendelea vyema.....mshukuru Mungu kwa hali hiyo uliyonayo.ipo sababu ya wewe kuwa kwenye hali hiyo.......karibu sana.

KUSUDI LA SOMO.
Leo nataka tujifunze machache kuhusu mapato na matumizi...hili ni somo pana sana na karibia kila mtu ana nidhamu yake kwenye elimu hii....ila nina kitu pia cha kukuongezea kwenye ufahamu wako.......ila hapa nataka wale wenye mawazo ya kutaka kutumia kidogo walichonacho ili waje wawekeze.....karibu sana.

MAPATO.
 Mapato ni kile kiasi unachoingiza,unaweza kukigawa kwa mwezi au kwa siku ...au hata kwa mwaka,je unaingiza shilling ngapi?...hapa ndipo kuna shida sasa.

Usidharau kiasi unachoingiza,hata kiwe kidogo namna gani,kiandike kwenye daftari,na kwa ushauri wangu ni vizuri ugawe kipato chako kwa sikiu.....mfano kama unaingiza elfu 30 kwa mwezi ,basi kwa siku utakuwa unaingiza 1000 kwa siku....nini umuhimu wake?.....tutajifunza kwenye matumizi.

Kama unaingiza chochote ,lazima uwe na uwezo wa kutoa chochote pia,hivyo heshimu sana unachokiingiza,na hakikisha unakuwa mbunifu kwa kidogo hicho unachokipata ili ukitumie kuongeza vyanzo vya mapato.

Ili uwe na uwezo wa kuongeza chanzo cha mapato ,lazima uwe vizuri kwenye kutambua unachoingiza ili ujibane kwenye matumizi kwa lengo la kubaki na kidogo utakachozalisha.

MATUMIZI

Hapa ndipo kuna matatizo sasa,.....nilisema ugawe mapato yako kwa siku ili ujipime matumizi yako kwa siku yapo juu/chini ya unachoingiza kwa siku?.......je kiasi kinachozidi unakipeleka wapi?....

  1. Tengeneza bajeti ya siku moja,kisha tafuta jumla kwa mwezi unatumia kiasi gani,,,,ila jitahidi unachotumia kwa siku kisizidi kile unachoingiza .
  2. Kwenye maisha kuna dharura ,kutenga kiasi cha dharura sio vibaya,ila lazima uangalizie na dharura ambazo unaweza kuleta matokeo,nyingine ziache zipite.
  3. Namba moja nafikiri inakufundisha kutumia kwa nidhamu,usitumie kilicho nje ya uwezo wako.....je bajeti yako inaruhusu ubaki na chochote?
  4. Tunashariwa kuweka akiba kabla ya matumizi ,ila ni vizuri ukafahamu kwanza mapato yako yakoje kisha ndio uanze kuweka akiba.
  5. Akiba ipe thamani ya kipato kingine,akiba ndio mtaji wako sasa,kama unatafuta mtaji kila siku na huna nidhamu ya kuweka akiba utasumbuka sana.....kama una akiba basi tayari una mtaji mmojawapo.....
NB. Kuwekeza au biashara ni elimu nyingine tofauti na elimu ya kuweka akiba,ingawa unatakiwa uweke akiba ukiwa unafahamu nini unatakiwa kufanya kesho......!!!


Makala hii imeandikwa na Saul Kalivubha,mmiliki wa label ya FIKIA NDOTO ZAKO.

0652 134707