PAGES

Showing posts with label SAIKOLOJIA. Show all posts
Showing posts with label SAIKOLOJIA. Show all posts

Tuesday, 9 April 2019

HILI NDIO GEREZA LA HATUA ZAKO

Karibu tena kwenye blog hii inayotoa mafunzo ya maisha na jinsi ya kufikia ndoto zako.Ni tumaini langu kuwa wewe ni mzima wa afya na unaendelea kupambana katika utatuzi wa changamoto mbalimbali ili zikupe ushindi wa kuliishi kusudi lako,karibu tujifunze.


KUSUDI LA SOMO.
Somo hili linakusudia kuwasaidia vijana ambao wana tatizo la kutopiga hatua ilihali kila siku wapo kazini na wanapata chochote lakini hawapigi hatua mbele.Katika somo hili ,vijana lengwa ni wale ambao wana maono ya kuifikia hatua fulani lakini siku zasogea na hata dalili za kufika huko hazipo.Wewe pia una tatizo hilo? kama ndivyo ,endelea hadi mwisho utajua gereza lako ni lipi.


KWANINI UNAFANYA HICHO UNACHOKIFANYA LEO?
Hili swali linahitaji sababu ,je umewahi kujiuliza swali kama hilo? na ulipata sababu zipi? .Inawezekana ukawa na majibu yako mengi sana ya kwanini upo unafanya hiyo kazi,wengine watasema ni kwa sababu ndio walichokisomea,wengine watasema ni kwa sababu hawakwenda shule ndo mana wanafanya shughuli hiyo ,n.k.Majibu yatakuwa mengi sana.Mimi kama ningeulizwa swali kama hilo ,jibu langu lingekuwa rahisi sana tu,ningesema sababu inayofanya nifanye hiki nikifanyacho leo ni kwasabu kinanipeleka kwenye kusudi la kuumbwa kwangu. Hivi unafahamu gereza limelofunga hatua zako ni sababu zilipo nyuma ya hicho unachokifanya?

GEREZA LA HATUA YAKO MPYA NI HIYO SABABU YAKO.
 Ni ngumu kupiga hatua mpya kama huna sababu zinazokusuma ufanye hivyo ,na sababu ambazo zitakufanya upige hatua mpya zinategemea sana na wewe unajitambua vipi,hapa ninamaamisha kwamba ni vizuri kwanza ujitambue wewe ni nani na wapi unatakiwa kwenda kulingana na kusudi lililowekwa ndani yako,kisha sasa ndio uangalie hicho unachokifanya ,je kinahusiana vipi na uelekeo wako?

Kama kila siku sababu zako ni kutaka ufanye kazi kwa bidii na kwa weledi,sawa ni sababu nzuri lakini je hicho unachotaka kukifanya kwa juhudi na weledi kinahusiana vipi na kusudi la kuumbwa kwako? kama hakuna mahusiano ndipo pale ambapo utaendelea kuwa na juhudi kwa kufanya jambo fulani lakini hufiki kule kwako ,mfano kama wewe uliumbwa uwe mchoraji ,na sasa upo katika kitengo cha afya kama Daktari,je unaunganisha vipi huo udakitari na kipaji chako cha uchoraji? Hapo unaweza kuiwa na sababu nyingi za kukufanya huo udakitari wako vizuri lakini ukawa huna sababu hata moja ya kutaka ufanye huo udakitari wako uendeleze kiapaji chako ,kwa namna hiyo  utajikuta unaendelea kuwa gerezani tu .

UNATOKAJE KWENYE GEREZA HILO?
Kama nilivyotangulia kusema mwanzo ,kwanza lazima ujitambue wewe ni nani,kisha uangalie unafanya nini kwa sasa,na je ufanyacho kina mahusiano na wewe ni nani? kama hakuna mahusiano sio ukiache ghafla lakini tengeneza mahusiano ,yaani kitumie hicho unachokifanya kusaidia kusudi la kuumbwa kwako,mfano mimi naelekea kuibadili dunia kwa kupitia maandishi na kuongea lakini kwa sasa natumika hospitalini ,je niache kipi?  jibu la haraka ni kwamba navyovipata hospitalini navitumia katika kusukuma kusudi la kuumbwa kwangu ,hivyo nyuma ya haya niyafanyayo kuna sababu zinazoniambia nielekee kwenye ulimwengu wa maandishi na kuzungumza.
Jitahidi utengeneze sababu zinazokusuma kwenda kwenye kusudi lako ,kukosa sababu hizo kunapelekea hali ya kuridhika na hatua hiyo uliyopo ,na hapo ndipo panakuwa mwanzo wa kufanya kazi kwa bidii lakini mbele husogei ,unaishia pale ambapo sababu zako zilikutuma.

Makala hii imeandikwa na Saul Kalivubha.
            0652 134707



Wednesday, 28 February 2018

MAMBO YANAYO PUNGUZA UWEZO WA KUFIKIRI.

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya maisha na jinsi ya kufikia ndoto zetu....nikupongeze kwa maamuzi yako ya kuamua kuwa mtembeleaji wa blog hii,nina amini hutobaki kama ulivyo....lazima mafunzo haya yatasogeza hatua zako mbele ....karibu.

KUSUDI LA SOMO.
Lengo la somo letu hili ni kujifunza sababu zinazopunguza uwezo wa kufikiri,.....na hili somo limekuja maalumu kwa sababu huwezi kufanikiwa nje ya fikra zako,pale ulipo ni matokeo ya kile unachokifikria....mambo gani yanapunguza uwezo wa kufikiria?...jifunze kwa nini rafiki yako hakuamini(urafiki)......


MAMBO YANAYOPUNGUZA UWEZO WA KUFIKIRI.

1.Mahusiano mabovu,..Hapa nazungumzia mahusiano ambayo yamekufanya kuwa mtumwa,haya ni yale mahusiano ambayo yanakufanya muda wote uyafikirie,...kufikiria mahusiano sio vibaya ,ila ubaya huja pale ambapo uliye naye kwenye urafiki amekutengenezea mazingira ya kutojiamini,..muda mwingi utakuwa unafikiria ufanye nini ili asiondoke na matokeo yake utajikuta unakwamisha mipamgo yako mizuri kwa sababu hutoipa nafasi kuifikiria mipango hiyo.

2.Marafiki,Jaribu kuchunguza kile unachokiwaza sana,kisha jiulize ,kwa nini unakiwaza sana?......fatilia marafiki zako wa karibu,wana mtizamo gani kwa kile unachokiwaza sana?.....kama unazungukwa na marafiki wenye uwezo mdogo wa kufikiri,usitegemee kuwa na fikra zaidi yao,.....

3.Ukosefu wa maarifa,Watu wasio na malengo hawpati shida katika kufikria kwa sababu hakuna wanachokitafuta,na mara nyingi watu ambao hawana malengo hupungukiwa pia na  maarifa,....ukipata maarifa,lazima utaongeza uwezo wako wa fikra ili uyahamishe malengo hayo kuwa vitu kamili......kwa hiyo kadri unavyokosa maarifa ya kutosha kuhusu jambo flani ndivyo uwezo wako wa kurifikria jambo hilo unapungua.

4.Historia ya maisha yako,Changamoto ni kinu cha mafunzo ila kwa wasiofahamu hilo mara nyingi hujikuta kwenye falsafa hasi...watu hawa mara nyingi huamini kuwa waliyoptia yaliwapunguzia vigezo vya mafanikio,hivyo hawaoni sababu ya kufikiria mambo  makubwa zaidi,muda mwingi hufikria waliyopitia.....

Hapo ulipo ni matokeo ya uwezo wako wa kufikiri,je upo sehemu sahihi?,kama sio hakikisha unapunguza mambo unayoyapokea kutoka kwenye mazingira yanayokuzunguka,.......jitengenezee uwezo mkubwa wa kufikri ili ubadilishe hivyo ulivyo.


 Makala hii imeandikwa na Saul Kalivubha ,mmiliki wa label ya FIKIA NDOTO zako,

      0652 134707.


Friday, 13 October 2017

TENGENEZA SOKO KABLA YA SAFARI.

Karibu tena kwenye blog hii inayotoa elimu ya mafunzo ya maisha na jinsi ya kufikia ndoto zetu,nashukuru Mungu kwa pumzi ambayo amekuwa akitupatia bure,karibu tujifunze.

KUSUDI LA SOMO.
Somo letu la leo linahusu umuhimu wa kutengeza soko kabla ya kuanza safari yoyote ya maisha,....Nafikiri wazo la haraka unaposikia neno soko ni biashara,lakini hapa nina maana zaidi ya soko la biashara,,,kabla ya kuendelea na somo jifunze kwanza somo hili (kwa nini hupigi hatua?).....karibu tuendelee.

MAANA YA NENO SOKO.
Kwa haraka ,soko ni sehemu ya kufanyia mauzo ya bidhaa/kitu flani,soko ni kipimo kizuri cha ubora wa kitu flani,mfano,soko la bidhaa flani likishuka,ni wazi kuwa ubora wa bidhaa hiyo unakuwa umeshuka.........Kwa maana pana zaidi na ambayo nataka ndio iwe sehemu kubwa ya somo letu ni hii,SOKO pia ni kipimo kizuri cha huduma yako,huduma yako inapimwa thamani sokoni,ubora wa huduma yako ndio unafanya soko lako liwe juu au chini.


KWANINI UTENGENEZE SOKO KABLA YA SAFARI?
Nafikiri umewahi kuona au kusikia majina ambayo yalifanya vizuri,ila hadi sasa hivi huyasikii tena,...tatizo ni nini?
Pia utakuwa umewahi kushuhudia mtu flani akianza kwa kasi kubwa na kwa ubora wa juu,ila baadae anapotea,tatizo ni nini?

Pamoja na sababu myingi zinazochangia hali hiyo,ila sababu nyingine kubwa ni watu wengi wanaanza safari bila ya kuandaa aina gani ya watu ambao watawafikia na changamoto zake,unapofahamu huduma yako itafikia watu wa aina gani (soko),itakusaidia uanze maandalizi ya kutosha kuhusu ubora wa huduma yako itayokidhi mahitaji ya watu hao kwenye vipindi tofauti tofauti .

Mazingira yanabadilika,mahitaji pia yana badilika,je umejipanga kuibadilisha huduma yako ili iweze kuendana na mabadiliko hayo?

Kabla ya safari ,hakikisha unatambua vizuri soko lako,tena utengeneze na soko mpya litalopatikana kulingana na mabadiliko yatayotokea,ukiendelea kutoa huduma ya aina moja muda wote,ubora wake utashuka kama ikitokea jamii imebadilika ila wewe hujabadilisha aina ya huduma yako.....TENGENEZA SOKO KABLA YA SAFARI.


Makala hii imeandikwa na Saul Kalivubha.
     mkurugenzi wa fikia ndoto zako label
       0652 134707.

Thursday, 30 March 2017

HATUA YA KWANZA KWENYE MAFANIKIO.

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya maisha, ni siku nyingine Mungu amefanya tukutane kwa lengo la kufundishana jinsi ya kufikia ndoto zetu
.
KUSUDI LA SOMO.
Leo nataka tujifunze machache kuhusu hatua ya awali katika safari ya maisha yenye ushindi, bado kuna watu ambao wamejaribu kila namna ya kupiga hatua ili kufikia malengo yao ila badala ya kusogea mbele wao wanarudi nyuma. ........Kibaya zaidi watu hao wameshindwa kufanya tasmini ya matokeo yao ambayo hayaridhishi. ..
Tatizo nini? .....zinaweza kuwa zipo sababu nyingi ila sababu kubwa inaweza kuwa ni kosa la awali. ...ni lipi hilo? .....karibu tujifunze.

 HATUA YA KWANZA KWENYE MAFANIKIO.
Unapoweka malengo ya safari yako lazima ujue mambo muhimu ya kukufanya upige hatua, bila hivyo unaweza kuwa na malengo mazuri yasiyo tembea, zipo njia nyingi ambazo watu tofauti tofauti wanaweza kuzieleza, ila kwa upande wangu taeleza njia tatu za kufanya uweze kupiga hatua, njia ambazo hutengeneza hatua ya awali na muhimu kwenye mafanikio yako. .....njia hizo ni hizi ;

1.Kuwa na marafiki sahihi.ni usemi wa kila siku kuwa mafanikio yako yapo kwa rafiki yako, ila wengi huwa hatujui hilo, bora utumie muda mrefu kuishi bila rafiki kuliko kuwa na rafiki asiyetambua umuhimu wa kusudi lako,Watu wengi wameshindwa kufika waendapo kwa kuwa karibu na marafiki hasi, ....lazima uwe na rafiki sahihi ili uweze kupiga hatua
.
2.Matumizi ya muda. Kwenye matumizi ya muda ndipo kuna mafanikio yote  (tembelea Google search uandike muda wa ziada kalivubha blog ujifunze matumizi sahihi ya muda).Ni ngumu kupiga hatua yoyote ya mafanikio ikiwa bado una matumizi mabovu ya muda,  kuna mambo ambayo lazima uyafanye ili yakupe kibali cha kuendelea, mambo hayo yanahitaji uwe na matumizi mazuri ya muda wako, hatua ya awali ni pamoja na kuwa na ratiba zinazofata muda wako vizuri.

3.Kutambua madhaifu yako. ..wanafalsafa wamewahi kuzungumza kuwa, .."mtu anaekushinda mafanikio kuna mambo anayofanya ambayo wewe hufanyi "..nini maana yake?.ni muhimu kufanya tasmini ya madhaifu ambayo yanaweza kuwa sababu ya kuzuia hatua zako, hiyo itakusaidia kujifunza namna ya kupiga hatua kwa kutumia njia tofauti tofauti zenye kuziba madhaifu yako, ..kujifunza kwa kupitia watu waliofanikiwa sio vibaya, lazima ujue nini ambacho wao wanakushinda .

Ni hatua chache sana za kukufanya upige hatua kwenye malengo yako, ila ni watu wachache sana wamekamilika katika hatua zote hizo tatu, ...fanya tasmini ya maisha yako.

          See you at the top.
          scientist Saul kalivubha.
              (0652134707 )

Wednesday, 22 March 2017

MUDA WA ZIADA -2

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya maisha kila jumatano
jumatano ya wiki, nashukuru Mungu
kwa kuendelea kunisamamia....karibu.
tujifunze.

KUSUDILA SOMO.

Kabla ya kuendelea na kusudi la somo letu hili, nikukumbushe kuwa somo letu lina sehemu mbili. 1.SIRI ZA MAFANIKIO KATIKA MUDA WA ZIADA.
2. MATUMIZI MABOVU YA MUDA WA ZIADA.........

ili tuwe sambamba pitia somo la sehemu ya kwanza, tembelea Google search na kuandika kalivubha blog muda wa ziada au Tembelea page ya FIKIA NDOTO ZAKO Facebook.
Leo tunaendelea na sehemu yetu ya pili.
kumbuka kuwa muda wa ziada ni muda baada ya majukumu ya pamoja, huu ni ule muda ambao upo chini ya utawala wako katika matumizi. .....karibu tuendelee.

2. MATUMIZI MABOVU YA MUDA WA ZIADA.....

KUWA NA MAMBO MENGI;Kuwa na mambo ambayo yana positive effect (matokeo chanya)kwenye ndoto yako sio tatizo, tatizo ni pale mtu anapokosa utaratibu katika kupanga mambo yanayostahili kwanza yawe mbele. ..ukianza kutumia muda wako wa ziada leo  kufanya mambo ya kesho hata kama ni mazuri, utakuwa unapoteza muda, ....lazima uwe na utaratibu katika kufanya mambo yako ili upate muda wa kutosha kufanya yanayostahili kwanza.

STAREHE; hapa ndipo kundi kubwa la watu lipo, maana wengi wanajua starehe lazima itumie pesa  .........hata
ukitumia muda wa ziada kwa mambo yaliyo nje ya ndoto zako tunasema upo
kwenye starehe.
Hili tatizo wanalo watu wengi ambao hawana malengo, ambao hawaumii kutumia sentensi hiii. ."NIPO NAPOTEZA MUDA ".....kila muda unaopoteza lazima utaulipa , je utaulipaje? .....utaulipa kwa majuto.

KULIPA NAFASI JAMBO MOJA. ...hapa tuelewane vizuri , kuna watu ambao wapo addicted na jambo flani, muda wote wa ziada anakuwa busy na jambo hilo tu. .....sio tatizo ikiwa ndio maisha yako yapo kwenye jambo hilo, ..ila kama kuna mambo mengine yamebeba maisha yako ,utakuwa unapoteza muda kwa kufanya jambo hilo moja. ....toa nafasi kwa mambo mengine pia. ...

NB....Kila muda unaopoteza, lazima utaulipa kwa majuto yasiyo na tiba,wengi wetu huwa tunapuuzia usemi huo sababu madhara ya kulipa muda huo huwa yanachelewa. .ila
muda ukifika wa kulipa muda huo lazima mtu akumbuke mambo yaliyo poteza muda wake. .....
Tumia muda wako vizuri leo, ndoto zako zipo kwenye matumizi mazuri ya muda wako wa leo. .........
Unatumiaje muda wako wa ziada?

Karibu kwenye somo mpya muda kama huu. ....

                   See you at the top.
            scientist Saul kalivubha.
                    0652 134707.


Wednesday, 15 March 2017

MUDA WA ZIADA -1

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya maisha, nashukuru Mungu kwa wema wake kwangu, ni jambo jema kama na wewe una utaratibu wa kumshukuru Mungu kwa makuu yake kwako.
Leo ni siku nyingine tena ambayo nimeona vyema tujifunze jinsi ya kutumia muda wetu vizuri ili tufikie malengo yetu.

KUSUDI LA SOMO .
Lengo la somo letu hili ni kujifunza mambo makubwa mawili ambayo ni.
1. SIRI ZA MAFANIKIO KATIKA MUDA WA ZIADA. 2.MATUMIZI MABOVU YA MUDA
WA ZIADA.

Kabla ya kuanza na sehemu ya kwanza ya somo letu, tuangalie maana ya muda wa ziada.
Muda wa ziada ni muda baada ya majukumu ya pamoja , huu ni ule ule muda ambao upo chini ya utawala wako katika matumizi.

      1.SIRI ZA MAFANIKIO KATIKA MUDA WA ZIADA.

Utofauti uliopo kati ya watu wenye majukumu sawa ila mafanikio tofauti upo kwenye jinsi ya kutumia muda wao wa ziada, zipo sababu nyingi zinazoweza kusababisha utofauti huo,
ila matumizi ya muda wa ziada yana nafasi kubwa kwenye kufanya utofauti huo. siri zilizopo kwenye muda wa ziada ni hizi hapa.


Kwenye muda wa ziada ndio sehemu pekee ambayo mtu unaweza tulia na kufanya tasmini ya safari yako, umefikia wapi, na nini ufanye ili kufika uendapo.
Watu wengi huendelea kuishi maisha yasiyo badilika sababu hawafanyi tasmini ya maisha yao.....huwezi kufanya maamuzi ya kubadilisha aina ya maisha unayoishi ikiwa kwenye muda wako wa ziada unautumia kuboresha mazingira ya maisha yenye matokeo hasi.


Kwenye maisha tunapitia mazingira mengi sana hadi kufikia ndoto zetu, kila mazingira yamebeba mchango mkubwa wa ndoto zetu......kuna uwezekano wa kutofikia uendapo ikiwa  utafanya uzembe katika mazingira yako unayopitia.......ili uweze kujua mazingira uliyopo yamebeba nini kwa ajili yako, lazima uwe na muda mzuri wa kuchambua mazingira hayo. .....!

Wana falsafa huwa wanasema kwamba. ....   "usipo charge akili yako huwezi kuwa na uelewa
Nini maana yake?   walimaanisha ili  tuweze kuwa watu wapya lazima tuwe na muda wa
wa kuingiza mambo mapya na yenye  kubeba malengo yetu.....lazima upate muda wa
kuongeza maarifa,utaongeza vipi?  ...fatilia somo la njia za kuongeza maarifa, litafata baada
ya somo hili.

Kuna watu ambao ni wazee sasa, ila hawajui utofauti wao ni upi, kila mtu ana kitu cha
tofauti ambacho ni zawadi kutoka kwa Mungu, ila kuigundua inahitaji muda wa ziada.
utofauti wako ndio umebeba mafanikio yako, kama una matumizi mabovu ya muda wako,
unaweza usijue utofauti ulionao  (labda ije neema ya Mungu tu ).....

Jiulize, unatumia vipi muda wako wa ziada? ...zipo gharama za kulipa kila muda unaopoteza,
unazifahamu? .......................Tukutane wiki ijayo.


                           see you at the top.
                             scientist Saul kalivubha.
                              (0652 134 707 )









Wednesday, 8 March 2017

HOFU YA KUSHINDWA -3

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya maisha, upande wangu nashukuru Mungu anazidi kuonekana katika maisha yangu,ni jambo la kushukuru Mungu ikiwa na wewe ni mzima wa afya.
Karibu tena katika sehemu ya tatu na ya mwisho wa somo letu la HOFU YA KUSHINDWA.
NB. unaweza fatilia sehemu ya 1 na 2 ya somo hili kwa kuingia Google na kuandika. ...hofu ya kushindwa kalivubha blog  , ni vyema ufanye ivyo ili twende sambamba na sehemu yetu hii ya tatu. 

KUSUDI LA SOMO. 
Leo tuna jifunza sehemu ya tatu ya somo letu,kumbuka somo letu lina sehemu tatu ambazo ni  1.CHANZO CHA HOFU YA KUSHINDWA 2.MADHARA YA HOFU YA KUSHINDWA NA 3.JINSI YA KUISHINDA HOFU YA KUSHINDWA. 
NB. Kumbuka tu huwezi kufanikiwa kufanya maamuzi sahihi ikiwa upo kwenye hali ya hofu. 


                3.JINSI YA KUISHINDA HOFU YA KUSHINDWA .
Leo tuangalie njia za kuishinda hofu ya kushindwa ambayo ni ugonjwa hatari sana katika mafanikio yetu, na mbaya zaidi, watu wengi ni wagonjwa wa ugonjwa wa HOFU. ......
Kuna sehemu nyingi ambazo mafanikio yake yanahitaji uishinde kwanza hofu, siwezi kuelezea kila sehemu ,ila nimechagua sehemu tatu ambazo taeleza jinsi ya kukabiliana na hofu kwenye sehemu hizo, ukiweza vizuri itakusaidia kwenye sehemu zingine. 
Sehemu hizo ni BIASHARA, MAHUSIANO NA MAFANIKIO KWA UJUMLA. 
NB. Kumbuka hofu ni tatizo ambalo linahitaji muda ili kulimaliza, na lazima muhusika mwenyewe ajitambue kwanza. 

BIASHARA; watu wengi tumeishia kuwa na malengo ya bila vitendo katika kuanzisha biashara kulingana na HOFU YA KUSHINDWA, nini kifanyike? .....kabla ya kuanzisha biashara hakikisha unatambua kuwa changamoto zipo, usianze ukitegemea faida tu, kwa kutambua hilo itakusaidia kupunguza hofu ya kushindwa, maana tayari umetambua changamoto kabla ya kutokea. ........ila utaendelea kuwa imara kupitia changamoto hizo 
Wanasikolojia wanasema.." Changamoto ambayo umesha itambua kabla haiumizi sana "

MAHUSIANO; Vijana wengi huwa na hofu ya kuambiwa wamechelewa kuingia kwenye mahusiano hadi ndoa, hii imefanya vijana hao kuchukua maamuzi ya haraka na yenye kuipendezesha jamii bila kuwa na manufaa kwao. ....ipo pia hofu inayozuka pale mtu anapoachana na mchumba wake  (hofu ya kutopta tena ).....nini kifanyike? ..hakuna kanuni
ya moja kwa moja ila zipo njia ambazo kwa aslimia nyingi zinaweza punguza HOFU. 
(i).KUJIAMINI, lazima mtu ujiamini kuwa una thamani kwa mwenye kuijua thamani yako, kutambua hilo litakusaidia kufanya mambo yako binafsi huku ukisubiria mtu sahihi kwenye wakati sahihi. 
(ii) kuhakikisha unafahamu uendapo , ni ngumu kupoteza muda na mtu asiye wa kwako. ...ikiwa wako unamjua. ...kwanin usiwe mvumilivu kumsubiri? ....huwezi kuwa na hofu ya kuchelewa ikiwa  unamjua wako yupo njiani. .......yapo mengi ila hayo ni machache ambayo ukiyafahamu unaweza punguza hofu ya kushindwa. 
MAISHA KWA UJUMLA; maisha hayataki haraka  (kama wasemavyo waswahili),yanahitaji 
uvumilivu wa kutosha, ila mtu mwenye hofu sio mvumilivu. ......wataalam wa saikolojia wanasema mtu mwenye hofu hutamani kujisaidia kwa kukimbia  (haraka ) hivyo mambo yake huwa ya haraka haraka. .......nini kifanyike? lazima utambue kuwa mambo unaweza kufikia ndoto zako endapo tu ukiwa na subira, ila iwe subira yenye juhudi. 
Hivyo hata upitie changamoto nyingi sio njia ya wewe kutengeneza hofu. ..ila jifunze na ukiweza badilli mfumo wa utafutaji ili kuendelea na safari ya kuelekea mafanikio yako. 

Nina imani kuna kitu umejifunza kuhusu jinsi ya kuipunguza hofu kwa njia sahihi, somo la hofu ni pana sana, na hofu ndio adui mkubwa wa mafanikio yetu,Shetani pia hupenda mazingira yenye hofu. 
Kwa wale wanao amini, njia nzuri ni kuweka imani na Mungu, ukiweka hofu maana yake huna imani na Mungu. 
ulicho jifunza kitumie katika sehemu zote za maisha, ....ishinde HOFU YA KUSHINDWA. 

Karibu tena kwenye somo mpya muda kama huu, somo hilo ni MUDA WA ZIADA.......
ukitumia muda wa ziada vibaya utajuta milele. ...unatumiaje muda wako wa ziada? 

                                    see you at the top. 
                          scientist Saul kalivubha. 
                           ( 0652 134 707 )

Wednesday, 1 March 2017

HOFU YA KUSHINDWA -2

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya maisha, ni imani yangu kuwa hali yako ki afya ni nzuri, ila kwa wale ambao hawapo vizuri ki afya, Mungu asimamie harakati zote za kuirudisha afya yenu. Tupo kwenye kumalizia robo ya kwanza ya mwaka huu, nakusihi rejea kwenye daftari lako la malengo ujitasmini umefikia wapi.

Karibu kwenye somo letu la HOFU YA KUSHINDWA, nikukumbushe tu kuwa somo letu lina sehemu tatu ambazo ni. 1.CHANZO CHA HOFU. 2 . MADHARA YA HOFU YA KUSHINDWA. 3 . JINSI YA KUSHINDA HOFU YA KUSHINDWA.

KUSUDI LA SOMO.
Leo tunaangalia sehemu ya pili , MADHARA YA HOFU YA KUSHINDWA, nakusihi upitie somo la kwanza, unaweza fata link hii  (http://kalivubha.blogspot.com/2017/02/hofu-ya-kushindwa-1.html?m=1) au ingia Google search,andika kalivubha blog hofu ya kushindwa, utapata somo hilo.
NB.Lengo la somo hili ni kujifunza jinsi HOFU inavyoweza kuzuia mafanikio yako, hapa ninazungumza hofu iliyo zidi kawaida.

                                   2.MADHARA YA HOFU YA KUSHINDWA.
Hofu ina madhara mengi sana katika kufikia ndoto zetu, tuangalie jinsi HOFU inavyoweza kuathiri sehemu hizi tatu muhimu; MAAMUZI, UVUMILIVU NA KUJIAMIN I. .........ukiweza kufahamu madhara ya hofu katika sehemu hizo tatu, nafikiri utakuwa na uwezo wa kujipima  ili ujitambue upo kundi lipi .

MAAMUZI, hii ni sehemu muhimu sana kwenye maisha, ili uweze kuchagua machache kati ya mengi lazima ufanye maamuzi.........ipo vipi kwa mtu mwenye hofu? ...Mtu mwenye hofu anakuwa hajakamilika, tayari akilini mwake anakuwa na jibu la kushindwa hata kabla ya kufanya maamuzi.....Hivyo mtu huyo anakuwa yupo tayari kuchagua jambo lolote lile ambalo ana amini litapunguza hofu yake.
Kumbuka tu ni watu wachache sana ambao wamewahi kufanya maamuzi sahihi wakiwa kwenye hali ya HOFU ya kushindwa.

KUJIAMINI...Nakumbuka mwalimu mmoja aliwahi kuniambia usemi huu. ."Ukitaka kumshinda adui yako, hakikisha unamfanya apunguze KUJIAMINI "
ipo vipi kwa mtu mwenye hofu ya kushindwa? .....Mtu akiwa na tatizo la HOFU YA KUSHINDWA, anakuwa hajiamini, maana tayari anakuwa ameshindwa AKILINI mwake hata kabla ya kujaribu. ...madhara ya kutojiamini ni kufanya mambo hayaendani na thamani yako. .....
Watu wasio jiamini siku zote huwa hawapati wanayostahili, ila hupata yale wanayo amini yanaweza punguza hofu yao.

UVUMILIVU,mtu mvumilivu mara nyingi lazima awe ana jiamini kwa kiasi kinachostahili na pia lazima awe mwenye uwezo wa kufanya maamuzi yasiyo bebwa na Imani ya HOFU. ........
Mtu mwenye hofu ya kushindwa ni vigumu kuwa mvumilivu, huwezi kuwa mvumilivu kwenye jambo ambalo kwa imani yako tayari unajua utashindwa......je una weza kufanikiwa kwa hali hiyo?  ......hapana, maana kwenye maisha kuna malengo ambayo yanahitaji muda mrefu ili yaweze kukamilika, yanahitaji uvumilivu wa kutosha.

Hofu ya kushindwa ni hatari sana, hakikisha unajua tiba yake mapema.....Watu wengi wameacha njia zao ndefu ila zenye mafanikio kwa kufata njia fupi zisizo na mafanikio, wamefanya hivyo kwa kuwa WANA HOFU YA KUSHINDWA. .....wamejiona hawawezi .

Kitabu cha RAFIKI kipo kwenye maandalizi, kitakusaidia kujua kujua siri za mafanikio kupitia rafiki.
        Let's meet on the next week , on the same day.
                       
                                 See you at the top.
                                   scientist Saul kalivubha.
                                    (0652 134 707 )

Friday, 24 February 2017

HOFU YA KUSHINDWA-1

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya maisha, nina imani hali yako ya afya ni njema, shukuru Mungu kwa hilo.
Leo nimeona tujifunze swala zima la HOFU.....maana hakuna mafanikio unaweza fikia ikiwa hofu yako imezidi hali ya kawaida.

KUSUDI LA SOMO.
Lengo la somo letu hili ni kujifunza HOFU YA KUSHINDWA, Somo hili lina sehemu tatu ambazo ni.
                   1. CHANZO CHA HOFU
                     2. MADHARA YA HOFU.
                      3.JINSI YA KUISHINDA HOFU YA KUSHINDWA.

NB. zipo hofu za aina nyingi sana Mfn  hofu ya kujaribu, hofu ya kukoselewa  n.k,ila hofu zote hizo matokeo yake ni KUSHINDWA kwa jambo ambalo mtu anakusudia kufanya.
.......Hofu kwa maana halisi ni hali ya kuogopa anayokuwa mtu juu ya matokeo ya jambo flani.
               
               1.CHANZO CHA HOFU YA KUSHINDWA.

Zipo sababu nyingi sana zinazopelekea watu wengi kuwa na hofu ya kushindwa katika mambo yao wanayokusudia kuyafanya, chache kati ya hizo ni;

HISTORIA YA MTU...,katika maisha yapo mambo mengi mtu anapitia ambayo hayakuwa na matokeo mazuri kwake, inaweza kuwa ni mahusiano, biashara , hata katika masomo. Kupitia matokeo mabaya hayo, watu wengi hutengeneza imani ya kukosa uaminifu wa kurudia tena mambo hayo,hivyo mtu huyu anakuwa na hofu ya kushindwa kila anapokutana na mazingira yaliyo mfanya ashindwe.

KUTOJITAMBUA...,mtu asiye tambua mazingira anayostahili kupitia ili kufikia ndoto yake huwa anakuwa na hofu ya kushindwa, kwa nini? kwa sababu hana uhakika na alicho shika,kwa hiyo muda wote anakuwa anawaza kushindwa tu katika harakati zake.

MARAFIKI, marafiki wana nafasi kubwa ya kutengeneza hofu ya kushindwa kwa mtu, ukiwa na rafiki wengi ambao walijaribu na kushindwa. .....kibaya zaidi wakakata tamaa, ni rahisi wewe kutengeneza hofu ya kushindwa katika mambo ambayo rafiki zako walijaribu na kushindwa hadi kukata tamaa.
kuna uwezekano kuwa walio fanikiwa wengi waliacha rafiki zao wenye mtizamo wa kushindwa. ....hiyo iliwasaidia kupunguza hofu ya kushindwa kwenye mambo yao.

KUKOSA JUHUDI, hii ni sababu nyingine kubwa katika kutengeneza hofu ya kushindwa kwa mtu, kabla ya kufanya jambo flani,  kuna hali inakuja ya kukukumbusha juu ya maandalizi uliyo fanya kuhusu jambo hilo, hapo ndipo HOFU huanzia kutokana na majibu utayojipa.
mfano, kabla ya kufanya mtihani lazima juhudi yako ikupe hali ya hofu au ushujaa wa kufanya mtihani huo.

NB. Huwezi kufanya maamuzi sahihi ukiwa katika hali ya hofu, maana watu wenye  hofu mara nyingi hutafuta njia za ziada za kupunguza hofu zao. .......swali, Hizo njia za ziada zina matokeo gani kwenye kesho yako?
       .Hofu ina tiba,fatilia somo hili hadi mwisho utajua tiba yake.


                            See you at the top
                          Scientist Saul kalivubha
                           (0652 134 707 )

Friday, 20 January 2017

JITAMBUE 2

Nimshukuru  Mungu kwa siku nyingine hii, pia niseme asante kwake kwa uzima wako, Karibu tena kwenye blog hii kwa series ya somo letu la KUJITAMBUA.
Week iliyopita tulijifunza SIFA ZA MTU ASIYE JITAMBUA. ......kama hukupitia somo hilo ni vyema ukalipitia kabla ya kuendelea na hili la leo  (http://kalivubha.blogspot.com/2017/01/jitambue.html?m=1).

Leo nataka tujifunze sehemu zilizobaki kwenye somo letu hili. .....nazo ni MADHARA YA KUTOJITAMBUA NA JINSI YA KUTIBU UGONJWA WA KUTOJITAMBUA. ..


        2.MADHARA YA KUTOJITAMBUA.
Kutojitambua ni tatizo ambalo  limefanya wahusika wawe sehemu zisizo sahihi  (kwenye mahusiano, biashara, mafanikio n.k).
Madhara ya kutojitambua ni matokeo ya kuwa sehemu isiyo ya kwako. ......

 Madhara makubwa ambayo yanaweza beba yote kwa mtu asiye jitambua ni kutofanikiwa kwa jambo lolote, huwezi fanikiwa ikiwa hujui wapi umetoka, wapi ulipo na wapi uendapo, ili mtu afanikiwe kwa jambo lolote lazima ajue vizuri sehemu anayoenda, ikiwa haitoshi lazima mtu atambue vizuri mazingira ya kumfikisha aendapo.

Mtu asiye jitambua mara nyingi hushangiliwa na watu wavivu(watu wanaopenda sehemu rahisi )  hii humfanya mtu huyo kuendelea kufanya mambo ambayo yapo kinyume na jamii inayojitambua, hivyo mtu huyu hupoteza uaminifu. ....

  3. JINSI YA KUTIBU UGONJWA WA KUTOJITAMBUA.  
Kutojitambua huwa nasema ni ugonjwa kwa sababu kila mtu anaweza ambukizwa tabia ya kutojitambua kutoka kwenye mazingira.
Huwa ni rahisi kuzuia ugonjwa huu, ila ni Kazi kubwa sana kuutibu endapo mtu akiupata. ...hii hutokana na wagonjwa wa tabia hii kuwa wagumu kukubali kuwa ni victims.

 Ili mtu apone ugonjwa huu inabidi kwanza yeye mwenyewe atambue kuwa ni mgonjwa, kisha hatua inayofata ni zoezi la kubadili MARAFIKI. .....maana mtu asiye jitambua kuna uwezekano mkubwa hata rafiki zake hawajitambui pia.
Zoezi la kubadili rafiki huwa ni ngumu kidogo  (lina hitaji ujasiri ) Ila ndio tiba pekee ya kuaminika kwa mgonjwa wa aina hii.


Let's meet on the next week , we will be having  a new lesson termed as NDOTO YA MSIMU.



                    see you at the top
                    Scientist Saul kalivubha.

Thursday, 12 January 2017

JITAMBUE 1

 Nashukuru Mungu kwa uzima wangu, bila shaka wewe pia ni mzima wa afya. Ni utamaduni mzuri sana kuwa na ibada ya kumshukuru Mungu kwa makuu yake.

KUSUDI LASOMO
.Tukiwa bado tupo kwenye safari ya maisha nimeona vyema tujifunze somo la KUJITAMBUA. Somo hili litakuwa na sehemu tatu.

   1.SIFA ZA MTU ASIYE JITAMBUA.

  2.MADHARA YA KUTOJITAMBUA.
                        3.JINSI YA KUTIBU UGONJWA WA KUTOJITAMBUA.


Kujitambua kwa maana (definition) rahisi ni kufahamu vizuri mazingira yako, ..kufahamu mazingira yako tu haitoshi, kufahamu kwa nini upo kwenye mazingira hayo ndo Kujitambua kamili.
Kuna uwezekano kuwa watu wengi wapo maeneo yasiyo sahihi kwa sababu tu hawajitambui, na wataendelea kuwa maeneo hayo sababu  ya tatizo la kutofanya TASMINI.


                         SIFA ZA MTU ASIYE JITAMBUA

Kutojitambua
ni tatizo ambalo wengi wetu tunalo,ila ukiwa hujakutana na mazingira ya kulichochea tatizo hilo ni vigumu kuona dalili zake. ......na mara nyingi mtu mwenye tatizo hilo huwa hakubali kama analo. ....

zifatazo ni baadhi ya sifa za mtu aliye na tatizo la KUTOJITAMBUA.

KUTOKUWA NA MALENGO : hii inaweza kuwa ni sifa kuu ya mtu asiye jitambua,  neno malengo kwake anakuwa analisika tu. Kumbuka tu usipokuwa na malengo huwezi kujua usahihi wa eneo ulilopo, kila jambo kwako utaona sahihi ila mazingira yakibadilika kidogo utaona sio eneo sahihi kwako.

 KUTOKUWA NA RATIBA; mtu asiye jitambua huishi kwa ratiba za watu wengine,  kama huna ratiba ya kuongoza maisha yako ni ngumu  kuwa na mipaka ya kulinda muda wako. .....kila ratiba ya nje itakuwa inafanya mabadiliko kwako...kumbuka tu watu hupenda sehemu rahisi, kila wakiwa na free time hutafuta sehemu rahisi ya kupumzikia. ...mtu asiye jitambua huwa busy kwenye free za watu wengine.


KUWA TAYARI KUACHIA ALICHO NACHO; ..Ni jambo jema mtu kufanya tasmini na kubadili mazingira  (endapo akigundua hayupo sehemu sahihi ,ila hii ni tofauti kwa mtu asiye jitambua, ..mtu huyu yupo tayari kuacha sehemu salama na kuelekea pasipo salama,  hii mara nyingi hutokana na tabia kutojiamini (tabia ya mtu asiye jitambua ).....ni vigumu kuamini kitu ulicho nacho na wakati hujui sahihi ni kipi, na ukikosa imani na ulicho nacho just muda wote utakuwa na mawazo ya kukiacha.


KUISHI KWA MAZOEA;  mtu asiye jitambua huishi kwa mazoea, muda wote yeye anakuwa anaamini kufanya mafanikio mwisho wa safari yake,  kwa kuwa amepoteza kujitambua,mtu huyu
hana sababu za kwanini yupo  pale alipo. ....swali zuri la kujiuliza siku zote ni " upo hapo ulipo kwa sababu wengine wapo or upo kwa sababu lipo kusudi la wewe kuwepo hapo ?"


KUKOSA UVUMILIVU; mtu asiye jitambua hana uvumilivu hata kidogo, hii hutokana na kutojua  umuhimu au hasara wa alicho nacho, ni vigumu kuvumilia na huku hujui kwa nini unavumilia. ......wavumilivu ni wale wanao tambua mazingira yao vizuri.


      KUTOJITAMBUA ni ugonjwa wa kuzuia mafanikio, ugonjwa huu tafasiri yake ni sawa na msafiri ambaye huchukua maamuzi ya kupanda gari bila kujua aendapo.

.......welcome again next session on next week.

                 See you at the top.
             Scientist Saul kalivubha.
                 0652 134707


Thursday, 5 January 2017

MAAMUZI

Nimshukuru kwa kunipigania kila siku, hadi sasa nipo salama. .....ni vyema kama na wewe una utaratibu wa kumshukutu Mungu.....

KUSUDI LA SOMO. 

Leo nataka  tujifunze machache kuhusu  Maamuzi......karibu tujifunze,

                  MAAMUZI. .....

 Mwandishi :Saul kalivubha.

Maamuzi kwa mtazamo wangu huwa nasema. ....Maamuzi ni miguu,  usipofanya maamuzi huwezi piga hatua. ..
Mazingira tunayoishi yamebeba mambo mengi,...ili kupiga hatua lazima tuchague machache kati ya mengi. ...maamuzi ni kuchagua pia na ni changamoto kubwa sana kwenye mafanikio yetu. ...

                  MAMBO YA KUFAHAMU KUHUSU MAAMUZI. 
Unapofanya maamuzi, fahamu kuna hatua itafata ambayo ni utekelezaji, kabla ya utekelezaji  ni bora ukatasmini upya maamuzi yako. hii nafaida kubwa, maana mara nyingi mtu hufanya maamuzi kulingana na hali aliyonayo muda huo. .....inawezekana maamuzi yako sio halisi ila ya hali uliyokuwa nayo tu. ....je hali hiyo ikitoweka bado utaona upo kwenye maamuzi sahihi? 

Sifa kubwa ya maamuzi sahihi ni kuwa na matokeo yenye changamoto, Hapa ndipo wengi hujikuta wakibadilisha msimamo. ....Maamuzi sahihi ni chukizo kubwa kwa rafiki zako wanaotamani usitembee, changamoto zitaanzia kwa wao kupinga utekelezaji wa maamuzi yako. Kwa sababu wengi wetu hufanya maamuzi ili kufurahisha watu, tukiona rafiki zetu huchukia maamuzi yetu na sisi hubadili msimamo wetu. ......usiogope kupoteza rafiki walio kinyume na wewe,kumbuka tu bila maamuzi huwezi kupiga hatua. 

Kama una ugonjwa wa kukata tamaa hakikisha unafanya maamuzi ya kutibu ugonjwa huo kabla ya kufanya maamuzi mengine. ....almost watu wote waliokata tamaa huwa maamuzi yao ni sahihi kwao ila huwa hayana mafanikio. ......mtu aliyekata tamaa huwa na imani flani akilini mwake, hivyo imani yake ndio hutwala maamuzi yake.Imani ya mtu aliyekata tamaa ni  ni HOFU. .....ukifanya maamuzi ukiwa na hali ya hofu jiandae kupokea matokeo yenye kukatisha tamaa zaidi ya mwanzo. 


Ukishindwa kufanya maamuzi, mazingira yatafakufanyia maamuzi. ....wapo watu ambao hawajui waendapo wala watokapo. ..ni vigumu kusema jambo hili sio sahihi na huku sahihi hulijui,hivyo ukiwa kwenye hali hiyo tayari umetoa kibali cha mazingira kukufanyia maamuzi. 
Tatizo hili wanalo wengi, ili ujue kama una tatizo hilo jaribu kutasmini maamuzi unayofanya ukiwa kwenye mkusanyiko wa watu. .....jiulize hayo maamuzi ni yako au ni influence za wanaokuzunguka? ............


Watu ambao mazingira yamewafanyia maamuzi ila bado wanahisi ni maamuzi yao kuna uwezekano kuwa hawapo sehemu sahihi  (iwe  kwenye mahusiano, ndoa, biashara nk).
Jitahidi uwe makini kwenye maamuzi. 


                             See you at the top.
                      scientist Saul kalivubha.
                                  0652 134707.


Tuesday, 27 December 2016

SIFA ZA MTU ALIYEKATA TAMAA

Nashukuru Mungu kwa uwepo wake kwangu, anazidi kuonekana katika maisha yangu. Imani yangu ni kuwa wewe pia Mungu anaonekana kwako . Tukiwa mwishoni mwa mwaka huu,, nataka tujifunze machache kuhusu mtu aliyekata tamaa.                                                                        Muhimu ni kuwa huwezi fanikiwa ukiwa umekata tamaa.  Hapa chini ni baadhi ya sifa za mtu aliye kata tamaa.
1 . Huwa anakuwa na sababu nyingi za kutetea hali aliyonayo, kwenye ufahamu wake anakuwa na mifano mingi ya walioshindwa tu. 

2 . huwa anaamini mafanikio ni bahati na sio juhudi, kila aliyefanikiwa kwake humuona mwenye bahati na haamini kuwa juhudi zina nguvu katika mafanikio. 

3. Hapendi mafanikio ya wenzake, na hii ndio sababu yeye pia hafanikiwi. .....huwezi fanikiwa ukiwa hupendi mafanikio ya wenzako. 

4.huwa ni mtu wa kulaumu muda wote, hutafuta uadui na wanaomshinda....muda mwingi huwatafutia sababu waliofanikiwa  zaidi yake. 

5. Rafiki zake pia ni wenye sifa za kukata tamaa, ndio mana huwa ni ngumu kwa mtu aliyekata tamaa kubadilika. .....maana huwezi kuwa na mawazo tofauti na rafiki zako. .na ukifanikisha kuwa na mawazo tofauti huwezi kuwa na rafiki ambao mmepishana. 

6.mtu aliyekata tamaa  huwa anajaribu kutafuta short cut za kufanikiwa......siku zote kufanikiwa kwa ujanja ujanja mwisho wake ni kufa maskini. 

NOTE :Kukata tamaa ni ugonjwa, ugonjwa huu mara nyingi hutokana na historia ya mtu aliyopitia. ....inaweza kuwa ni kwenye mahusiano,biashara, Masomo etc 
             
           Huwa sio Kazi rahisi kutibu ugonjwa huu kwa haraka, kumbe ukiwa na rafiki mwenye kukata tamaa jitahidi maisha yako yawe sehemu ya  kumbadilisha(ingawa ni hatari sana kuwa karibu na aliye kata tamaa, badala ya kumbadilisha unaweza badilika wewe )

Jitahidi sana uwe makini na historia umeyopitia, uliyopitia jana, juzi au miaka ya nyuma hayana mahusiano na mafanikio yako. ......ila kama ulifanya maamuzi ya kudumu kwa uliyopitia ,tayari utakuwa umeingia tayari kwenye kundi la watu walio kata tamaa.
                See you at the top.
              scientist Saul kalivubha.
                       0652 134 707.