Sunday 26 February 2023

HIVI NAWE UNAFANYA MAMBO KWA HASARA? 😔 KAMA JIBU NI NDIO, MAKALA HII  INAKUHUSU 

 HIVI NAWE UNAFANYA MAMBO KWA HASARA? 😔 KAMA JIBU NI NDIO, MAKALA HII  INAKUHUSU .

Japo wataalamu wanasema hakuna kipimo cha muda sahihi wa mafanikio lakini vipo vipimo vya kujipima kuwa unafanya mambo kwa hasara na ukijua hilo itakuwa rahisi kufanya maamuzi magumu ya kutoendelea na shughuli hiyo inayokupa hasara au kujiboresha ili upate uanze kupata faida.  Inaumiza sana kutumia nguvu kubwa halafu matokeo yaje kidogo au yasije kabisa 😔  Bahati mbaya ni kuwa wengi huwa hatujitambui kuwa tupo tunapoteza muda bure bali tunakuwa tunajifariji kuwa tupo tunavumilia na ipo siku tutafanikiwa, sio vibaya kujipa faraja lakini ni vibaya pia kujipa faraja kwenye sehemu isyo yako au kujipa faraja kwa kitu ambacho haiwezekani.Somo hili lipo mahususi kwa watu ambao wanasumbuka na changamoto ya kufanya mambo kwa hasara.

Zipo dalili nyingi za kujipima ili kujifahamu kuwa upo kwenye kundi la watu ambao hufabya mambo yao kwa hasara, dalili hizo ni kama zifuatazo;

1. Unafanya mambo bila kuyamaliza , kwa mfano leo unaanza safari ya kusoma kabla ya hujamaliza miaka yako ya ki elimu unaona kuwa umekosea unaachana na kozi hiyo na kutafuta kozi nyingine 😔 Unafungua biashara fulani na kabla hujaimudu vyema unajiona kuwa umekosea unaifunga na kuanzisha nyingine 😔 Unaanzisha mahusiano ya kimapenzi kwa furaha zote lakini ndani ya muda mfupi unaona umekosea unamuacha na kutafuta mwingine 😔 

2. Unakaa hatua moja kimafanikio kwa muda mrefu bila kuhama,hii hutokea pale ambapo mbele husogei kwa mfano unauza biashara ya nyanya miaka na miaka na kwa mtaji ule ule  .

3.Unafanya jambo bila kuwa na muda wa ukomo kwa mfano  unaamua kufanya biashara ya kutembeza mitumba ya n  lako la nguo na uachane na kutembeza mtaani. 

4. Upo kwenye mahusiano  na unaona kabisa ishara zote kuwa hutakiwi hapo lakini unaendelea kuvumilia kwa sababu unaona utakosa pakwenda  , hii ni dalili ya kuwa unafanya kihasara. 

Je kuna dalili moja wapo unayo hapo juu? Au zifananazo na hapo? Kama jibu ni ndio basi upo unafanya vitu bila mafanikio , je utatokaje? 

Njia rahisi ya kutoka kwenye kufanya mambo yasiyo na mafanikio ni kuwa na muda wa kutosha wa kujitathmini kwenye chochote ufanyacho na kujitengea ukomo wa muda usikubali ukae eneo moja muda wote la sivyo iwe ndio mwisho wa malengo yako  kama sivyo jiwekee muda wa kutoka hapo kama unauza maji ya basi moja uwe na kiwanda cha kutengeneza maji . Jiwekee mbinu za kujifanyia uchunguzi kila muda fulani.


Makala hii imeandikwa na Mwanasayansi Saul Kalivubha 

+255652134707