Wednesday 28 February 2018

MAMBO YANAYO PUNGUZA UWEZO WA KUFIKIRI.

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya maisha na jinsi ya kufikia ndoto zetu....nikupongeze kwa maamuzi yako ya kuamua kuwa mtembeleaji wa blog hii,nina amini hutobaki kama ulivyo....lazima mafunzo haya yatasogeza hatua zako mbele ....karibu.

KUSUDI LA SOMO.
Lengo la somo letu hili ni kujifunza sababu zinazopunguza uwezo wa kufikiri,.....na hili somo limekuja maalumu kwa sababu huwezi kufanikiwa nje ya fikra zako,pale ulipo ni matokeo ya kile unachokifikria....mambo gani yanapunguza uwezo wa kufikiria?...jifunze kwa nini rafiki yako hakuamini(urafiki)......


MAMBO YANAYOPUNGUZA UWEZO WA KUFIKIRI.

1.Mahusiano mabovu,..Hapa nazungumzia mahusiano ambayo yamekufanya kuwa mtumwa,haya ni yale mahusiano ambayo yanakufanya muda wote uyafikirie,...kufikiria mahusiano sio vibaya ,ila ubaya huja pale ambapo uliye naye kwenye urafiki amekutengenezea mazingira ya kutojiamini,..muda mwingi utakuwa unafikiria ufanye nini ili asiondoke na matokeo yake utajikuta unakwamisha mipamgo yako mizuri kwa sababu hutoipa nafasi kuifikiria mipango hiyo.

2.Marafiki,Jaribu kuchunguza kile unachokiwaza sana,kisha jiulize ,kwa nini unakiwaza sana?......fatilia marafiki zako wa karibu,wana mtizamo gani kwa kile unachokiwaza sana?.....kama unazungukwa na marafiki wenye uwezo mdogo wa kufikiri,usitegemee kuwa na fikra zaidi yao,.....

3.Ukosefu wa maarifa,Watu wasio na malengo hawpati shida katika kufikria kwa sababu hakuna wanachokitafuta,na mara nyingi watu ambao hawana malengo hupungukiwa pia na  maarifa,....ukipata maarifa,lazima utaongeza uwezo wako wa fikra ili uyahamishe malengo hayo kuwa vitu kamili......kwa hiyo kadri unavyokosa maarifa ya kutosha kuhusu jambo flani ndivyo uwezo wako wa kurifikria jambo hilo unapungua.

4.Historia ya maisha yako,Changamoto ni kinu cha mafunzo ila kwa wasiofahamu hilo mara nyingi hujikuta kwenye falsafa hasi...watu hawa mara nyingi huamini kuwa waliyoptia yaliwapunguzia vigezo vya mafanikio,hivyo hawaoni sababu ya kufikiria mambo  makubwa zaidi,muda mwingi hufikria waliyopitia.....

Hapo ulipo ni matokeo ya uwezo wako wa kufikiri,je upo sehemu sahihi?,kama sio hakikisha unapunguza mambo unayoyapokea kutoka kwenye mazingira yanayokuzunguka,.......jitengenezee uwezo mkubwa wa kufikri ili ubadilishe hivyo ulivyo.


 Makala hii imeandikwa na Saul Kalivubha ,mmiliki wa label ya FIKIA NDOTO zako,

      0652 134707.


Friday 16 February 2018

KWA NINI RAFIKI YAKO HAKUAMINI?

Tarehe 22 FEBRUARY ni siku ambayo nasherehekea siku ya kuzaliwa kwangu......pamoja na furaha yote ya siku hiyo,huwa ni siku pia ambayo nimejiwekea utaratibu wa kukumbuka mambo ambayo yalitokea kwenye safari yangu ya maisha......kiufupi safari yangu kwa asilimia kubwa ilikuwa ya maumivu......hapo ndipo nakumbuka nafasi ya rafiki katika maisha yangu........karibu.

KUSUDI LA SOMO.

Lengo la somo hili ni kutaka kutoa majibu ya kwa nini huna imani na rafiki yako?.....au kwa nini yeye hakuamini?.....hii ni vita kubwa sana ambayo inayumbisha urafiki wa watu wengi na kusababisha kifo cha urafiki..........karibu.

KWA NINI HUNA IMANI NARAFIKI YAKO?.......Sabubu za kwa nini humuanini rafiki yako zipo sawa na kwa nini yeye hakuamini.........hivyo ngoja nielezee sababu zinazo fanya ukose imani na rafikiyako.....kisha utazigeuzia upande wa pili.

1.HISTORIA YAKE.......kufahamu historia ya rafiki yako sio vibaya.na inaweza isiwe hatari kabisa kwa yeye kuptia historia hiyo...tatizo liko wapi?.........hadi wewe kukubali kuwa na urafiki na mtu unayejua historia yake,ni wazi uliamini kuwa kabadilika....lakini kubadilika kwake haina maana kuwa attaishi bila madhaifu yoyote yale........kosa lipo pale ambapo utaanza  kuunganisha madhaifu yake ya kawaida na maisha aliyopitia.....ukiruhusu hali hiyo,nakuhakakishia,hutomuamini hata kidogo,utakuwa mtu wa wasiwasi tu muda wote......ukiona huna busara ya kubeba historia ya nyuma ya rafiki yako,au umejiaminisha kuwa bado hajabadilika......kuwa mbali.

2.HISTORIA YAKO,.....Usipokuwa mwenye hekima na busara,kile unachokitenda au umechotendewa au kuona wengine wakitendewa,kitakufanya uamini watu wote duniani wapo hivyo.....hali hii ukiiruhusu,itakufanya ujihami.....unajua madhara ya kujihami?.......KWANZA wewe mwenyewe utakuwa sio muaminifu,pili, rafiki yako utampa uhusika wako ....hutomuamini pia........kuna kipindi inabidi uishi bila hamasa za nje,hamasa ambazo ni za mawazo hasi.,,,zitakufanya uingiwe na ugonjwa wa kutoamini watu wasio na hatia............

 Hapa nakumbuka utafiti wangu ambao niliufanya ili kugundua ni kwa namna gani watu hawana imani na marafiki zao sababu zilizosababisha hivyo........nilitumia marafiki wa jinsia tofauti,,,,wavulana kumi ambao nilwaulizwa wanajisikiaje ikitokea simu ya rafiki wake wa kike  haitapokelewa au itakuwa busy(kutumika)  pindi wakiwatafuta.......maatokeo yalikuwa hivi:

SITA walisema ,wakikuta hali hiyo,watahisi kusalitiwa,wawili walisema watajisikia vibaya tu.....wengine wawili wa mwisho walisema hiyo ni hali ya kawaida tu......kwa ufupi utafiti huo unaonyesha ni namna gani uaminifu umepungua ......nilivyofatilia zaidi kwa marafiki hao sita ndipo nikapata somo hili la leo......ndani ya sababu hizo mbili kuna sababu ndogo ndogo nyingi.....


Makala hii imeandikwa na Saul Kalivubha.....Mkurugenzi wa label ya FIKIA NDOTO ZAKO.

                                  06552 134707.


Friday 9 February 2018

MAMBO MATANO MUHIMU KABLA YA BIASHARA.

Karibu tena kwenye blog hii inayotoa mafunzo ya elimu ya maisha na jinsi ya kufikia ndoto zako,nikupe pongezi tu kwa kufanya maamuzi sahihi ya kutembelea blog hi,hutobaki kama ulivyo....karibu tujifunze.


KUSUDI LA SOMO.
Lengo la somo hili nataka tujifunze mambo matano muhimu ambayo yanaweza kukusaidia katika kuanzisha biashara yako.........mambo haya nimejifunza kupitia uzoefu wangu niliojifunza kwenye biashara ambayo nimeahi kuifanya na kwenye uwekezaji ambao tayari nipo naufanyasasa, ,pia mengine nimefanya utafiti kutoka kwa  watu wengine........Karibu tujifunze.


Nafikiri kama wewe sio mfanya biashara ,basi utakuwa umewahi kuwaza kuwa mfanya biashara......na kwa sababu umeamua kusoma makala hii,kuna mambo mawili....moja,utakuwa umewahi kufanya biashara lakini haikukulipa,pili utakuwa una shauku kubwa ya kuanzisha biashara ......ni mahali sahihi,.......karibu tujifunze mambo hayo matano.


1.Kuwa makini na biashara zinazofika mtaani kuwa zinaingiza pesa haraka,......inaweza kuwa ni kweli ndio,ila mvuto huo usiwe ndio hamasa namba moja ya kukufanya uifanye bishara hiyo.....biashara inayosifika sana huwa haikawii kuchoka kwa sababu hufanywa na wengi,......kwa hiyo ifatilie kwa kina upate taarifa kamili za wakati huo kuhusu soko lake.....mfano wa biashara zilizosifika ni kilimo cha matikiti,mpunga,bodaboda na bajaji.......bodaboda na matikiti soko lake sio lile ambalo lilisifika miaka michache iliyopita,..limeshuka.....usiingie kwenye biashara bila kuwa na taarifa za wakati huo.

2.Jitahidi uiandike biashara kwenye daftari kabla ya kuanza kuifanya,........andika kuanzia mtaji ,soko lake na malengo ya wewe kuamua kuifanya biashara hiyo.....jipe kikomo cha kukamilisha malengo hayo........weka mikakati itayokufanya uyafikie malengo hayo kwa kupitia biashara hiyo......mfano mimi ni mkulima ambapo malengo yangu ni kumiliki ekari zaidi kumi hadi mwaka kesho kutoka kwenye chache nilizonazo.

3.Weka fungu la pesa,au anzakutafuta pesa ili ukamilishe biashara hiyo sasa uliyoiandika kwenye daftari,...jitahidi tu usitumie pesa yako yote kuanzia biashara,.....tumia akiba kuanzishia biashara.

4.Fanya maamuzi magumu,ishinde hofu ya kushindwa....ukimaliza maandalizi ,mara moja anza biashara.......ila hakikisha umetengeneza soko kabla ya biashara.....tambua ni watu wa aina gani umekusudia waipate bidhaa yako.

5.Fanya biashara kwa juhudi zako zote,kwa ubunifu ,hakikisha unafanya ambayo wengine hawayafanyi kwenye biashara iliyo sawa na wewe.....kuwa mvumilivu na mwenye subira,...biashara mara nyingi hainzi sawa na ulivyotarajia ...utasumbuka kidogo mwanzoni hadi kuja kufikia matarjio.



     Makala hii imeandikwa na Saul Kalivubha,mmiliki wa label ya fikia ndoto zako.


                             See you at the top.
                                  0652 134707