Thursday 19 December 2019

RAFIKI YAKO NI NANI?

Habari za kwako ndugu mpenzi msomaji wa blogu yetu pendwa ya FIKIANDOTOZAKO  na hongera sana kwa majukumu ya kila siku na pole kwa changamoto za kila siku pia, karibu kwenye somo maalumu la kufunga na kufungua mwaka liitwalo  RAFIKI YAKO NI NANI?.

Ni kawaida yangu kila mwaka kufanya tathmini ya malengo yango na kisha kutafuta sababu za kwa nini nimeshindwa au nimefanikiwa  na hapo huwa nakuta sababu nyingi  sana nyuma yake  lakini  sababu moja tu huwa ninaipa uzito nayo ni RAFIKI ALIYE NYUMA YANGU NI YUPI? napenda sana kukupa changamoto ya kujitafakari na wewe uchunguze nyuma ya kushindwa/kufanikiwa kwako yupo RAFIKI WA AINA GANI?

Ni kawaida ya watu wengi kujiwekea malengo kila mwanzo wa mwaka mimi pia ni mmoja wao na malengo hayo yanakuwa na uhusiano na maono(vision)yako mfano una maono ya kuwa na kampuni kubwa ya kusaidia vijana baada ya miaka kumi ijayo hivyo ni jukumu lako la kuishi maandalizi kila siku kila mwaka ujione kusogea kwenye hayo maono yako  , sasa angalia maono yako umeyasogelea au umesogea nyuma kabisa? Kwa nini?

RAFIKI YAKO NI NANI? Siku nzima ni ngumu kuisha bila kuwasiliana na rafiki yako wa karibu  na hiyo ndio kawaida ya URAFIKI yaani kunakuwa na hisia za kutaka  ujione karibu na rafiki yako  sasa je MNAONGEA nini? mnaongea kwa mazoea  tu salamu , kukumbushana ya nyuma na kuambiana move zipi nzuri au viwanja vipi vizuri vya starehe kisha usiku mnatakiana usiku mwema, huyo ndio rafiki yako? rafiki anakutafuta akiwa na shida tu au ili URAFIKI uendelee wewe ndio unatakiwa kila siku kuanzisha mazungumzo wewe na kama hiyo haitoshi URAFIKI umejengwa na vitu yaani mmoja anatumia nguvu ya ziada kuufanya URAFIKI uendelee, nikupe pole sana kama upo kwenye URAFIKI wa aina hii kwa sababu hakuna namna unaweza kufikia malengo yako ukiwa kwenye hali hiyo ya marafiki sana utaishi tu maisha ya kawaida huku ukiamini ndio maisha yalivyo.

CHAGUA MARAFIKI WA KUAMBATANA NAO.

Unataka kwenda wapi?

Marafiki wazuri ni wale ambao ukiwa nao unajiona mpya kwenye malengo yako yaani mkiwa wote wanakupa namna utakavyofika na sio wanakuonyesha namna utakavyoshindwa kwa kila malengo yako  , usiwe na marafiki ambao watakufanya mtumwa kwao badala ya wote kwa pamoja kusaidiana jinsi ya kufika wao wanajenga mazingira ya wewe kuwa mtumwa kwao.

Rafiki yako ni nani?

Soft copy ya kitabu cha siri za URAFIKI kinapatikana kwa Tsh 4000 tu .

 Saul Kalivubha.
  Mwanasayansi.
FIKIANDOTOZAKO.
   0652 134707

Thursday 17 October 2019

NGUZO ZA MAAMUZI SAHIHI,JIFUNZE.


Na Mwanasayansi Saul Kalivubha.

Habari ndugu mpenzi msomaji wa blogu yako hii pendwa na karibu tena katika safu hii ambayo tunajifunza  mambo chanya kwa ajili ya kuitafuta hatua mpya  zaidi  ,karibu tujifunze.
Maamuzi sio neno geni hata kidogo na  kila siku lazima kila mtu afanye maamuzi mara nyingi sana  japo idadi ya maamuzi haziwezi kuwa sawa kutoka mtu mmoja kwenda mwingine, maamuzi ni machaguzi hivyo huwezi kuamua ukiwa na jambo moja mkononi  lazima uwe na mambo mawili au zaidi  mkononi ndipo ufanye maamuzi ya kubaki na jambo moja kati ya mengi,je una uhakika gani kama maamuzi unayoenda kuyafanya ni sahihi? Kuna nini nyuma ya maamuzi yako? .

Tumesikia watu wengi sana wakijilaumu kwa maamuzi yao ya jana na kujutia kana kwamba wangalijua mapema wasingefanya maamuzi yale hii ni wazi kuwa maamuzi yao sio sahihi japo kwa muda ule wanaamua walijiona kuwa wapo sahihi.

Tuangazie kidogo juu ya nini kinafanya watu wafanye maamuzi na kwa nini majuto yanafuata baada ya maamuzi.
Kwa nini tunafanya maamuzi? Tunafanya maamuzi kwa sababu mambo tunayokutana nayo hatuwezi kwenda nayo yote hivyo lazima tuamue ili kuchagua machache yanayotufaa na kuacha yasiyo tufaa, maamuzi yoyote yale lazima kuna  chaguo moja ulilipenda ndio maana ukaamua kulichagua chaguo hilo.

Kwa nini ulizwe na chaguo lako mwenyewe?.Nyuma ya maamuzi yoyote yale kuna ufahamu,hisia,msukumo wa watu  na muda.Hivi vitu vinne ndio hasa  vinaoongoza maamuzi yetu hivyo unapoona unajutia maamuzi yako lazima kuna moja kati ya ufahamu wako,msukumo wa watu,hisia  au muda lilikuvuruga.
MUDA, tunapokuja suala la muda tunaangazia sana kuchelewa yaani mtu anapoingiwa na hofu ya kuchelewa huwa anajikuta akifanya maamuzi bila kuyafikiria maamuzi yake kwa utulivu kwani lengo lake kubwa inakuwa ni kutaka tu awahi  hivyo atatumia vigezo vichache katika kufanya machaguzi.

Mara nyingi maamuzi ambayo yanafanywa  kwa kukimbizana na muda huwa ni sahihi kwa muda ule mtu anapoyafanya lakini baadaye anakuja kuyajutia maamuzi yake.Usikubali kufanya maamuzi na hisia za kuchelewa utakosea hivyo ni vizuri utafute utulivu ndio kisha ufanye maamuzi.
Msukumo wa watu, hizi tunaziita kelele za nje zinazokusukuma ufanye jambo  fulani  , sio kwamba hutapswi kutosikiliza kelele za nje la hasha  ila unachopaswa ni kutofanya maamuzi kwa sababu umepigiwa kelele,kelele za nje ni kama upepo uvumao ambapo ukikukuta huna msimamo utayumba na kujikuta unaenda hata usipopotaka  , kwenye mahusiano na biashara suala la kupigiwa kelele huwa lipo huu sana  na wengi waliofanya maamuzi kwa kusukumwa na kelele walipotea, jitafute wewe ni nani na unataka nini ndipo ufanye maamuzi.

HISIA  ,Kila mtu ana msukumo wa hisia ndani yake  kwani hisia ni sehemu ya ulinzi pale tu zinapotumiwa vizuri, zipo hisia za aina nyingi   kama vile  hisia za hasira,hisia za kupenda,hisia za huzuni,hisia za hofu  nakadhalika, sasa  hisia zikiwa juu huwa zinaficha negative side effects (madhara hasi)  na kukuaminisha kuwa  utafurahia matokeo ya maamuzi unayotumwa kufanya na hisia, mtu mwenye hasira akifanya  maamuzi huwa anajiona mwenye furaha kwa muda kisha hasira ikimuachia tu anabaki na majuto  , hivyo unatakiwa kufanya maamuzi bila kusukumwa na hisia.

UFAHAMU, ufahamu wa mtu kuhusu jambo fulani  ndio unamuongoza kufanya maamuzi yanayohusu jambo hilo  ,kwa mfano  wanafunzi wanaochagua kozi za kusoma kwa kutumia ufahamu wa haraka na baadaye wanakuja kuona kuwa wamekosea baada ya ufahamu wao kuongezeka, vivyo hata katika mahusiano,biashara na mengineyo watu wamekuwa wakifanya maamuzi kwa kutumia ufahamu mdogo ,hivyo inashauriwa kutafuta maarifa ya kutosha kabla ya maamuzi fulani .



Sunday 14 July 2019

MBINU ZA KUPIMA UFAHAMU WAKO.

Habari ndugu na mfuatiliaji wa makala zetu za blogu yako pendwa ya FIKIA NDOTO ZAKO,ikiwa imepita muda wa kutosha bila kukuandikia makala katika blogu yetu hii ni kwa sababu tu ya uboreshaji ambao ulikuwa ukiendelea kwa lengo la kukupatia wewe msomaji na mwanafunzi maarifa yaliyo bora,karibu .

Somo letu la leo ni rahisi kama utalipa muda wa kutosha kalitafakari na ni somo gumu kama utapita juu juu,  hivyo inahitaji utulivu wa hali ya juu sana.
Ufahamu  ni moja ya eneo muhimu sana ambalo ndio linakutofautisha wewe na mimi ,wewe na rafiki yako ,wewe na mnyama kama vile sungura n.k,kumbe ufahamu ndio muongozo wa kwanza wa maamuzi yetu na ndio gereza limelofunga hatua zetu.

Ufahamu unaanzia mbali sana pindi mtoto anapozaliwa hadipale ambapo mazingira yatamuhitaji atafute mwenyewe (kujitegemea)  ,hadi kufikia umri wa miaka 9 mpaka 10 ufahamu wa mtoto unakuwa ukiamini kwa 100% muongozo wa mzazi /mlezi wake ndio maana mtoto wa umri huo anakuwa haamini kama kuna mtu zaidi ya baba /mama yake ,hata akutane na kitu cha kutisha namna gani ambapo hata kina nguvu zaidi ya mzazi wake bado atakitishia kitu hicho kwa kumtaja baba yake au mama yake akiamini hicho kitu kitaogopa na kumuacha,yote hiyo ni kwa sababu ufahamu  wake ndio unamtuma hivyo ,je ufahamu wake ni sahihi?

Inawezekana  ukawa ;

1.Unaabudu katika dini/dhehebu  fulani kwa sababu unaamini uliowakuta wakifanya hivyo hawawezi kukosea kuwa katika sehemu hiyo wanayoabudu.
2.Ulichagua kozi fulani kwa sababu waliokushauri uliwapa thamani ya juu kuwa hawawezi kukosea katika machaguzi.
3.Kwa sababu unaona watu wanafanya  ndio maana ufahamu wako unakutuma kuwa hilo jambo ni sahihi n.k

Je unawezaje kuhakikisha kuwa ufahamu wako ni sahihi?
Tukiachana na kupima ufahamu  ulinao kuhusu dini/imani/kanisa/msikiti  ambapo ni somo ndefu na linalohitaji utulivu wa juu zaidi, tuje katika mbinu za pamoja za kupima ufahamu ulionao kwa ujumla ,kwanza  kabla ya mbinu hizo tutambue ya kwamba ufahamu  kwa asilimia nyingi unatokana na mazingira yanayokuzunguruka kama vile marafiki na wazazi/walezi  n.k, pia ufahamu unategemea na umri.

Kadri mazingira yanavyobadilika na umri unavyosogea ndipo unazidi kuona kuwa kuna mambo zaidi ya vile ulivyokuwa ukifahamu na utagundua kuwa ulikuwa unafanya makosa pasipo kufahamu kwa sababu ufahamu wako ndipo ulipoishia pale,kwani maamuzi yetu ni ,matokeo ya ufahamu wetu ulivyo.

MBINU ZA KUPIMA UFAHAMU WAKO.

1.Kwanza jitambue wewe ninani,sio jina lako wala wapi unaishi ,jitambue kwa nini ulizaliwa? utapata sababu ambayo ndio kusudi la wewe kuzaliwa,sababu ya kuzaliwa kwako unaweza pia kuangalia kipi unaona hakiendi sawa yaani kuna namna unasukumwa kutaka kuweka mfumo sawa,hapo kuna kusudi lako na kipaji chako ,ukishajifahamu wewe ni nani tayari utaanza kutafuta ufahamu wa kutosha kujihusu wewe na safari yako.

2.Makosa yetu,kupitia makosa yetu ni njia nzuri sana ya kupima ufahamu wetu,mfano umetumia ufahamu wako kufungua simu ukashindwa ni wazi kuwa ufahamu wako bado, kuna zaidi ya unavyofahamu,unapoingia kwenye makosa kaa chini ujitafakari  ni lazima tu kuna jambo hulijui ndio maana ukakosea hivyo litafute .

3.Kaa chini uchunguze kwa nini unaamini hivyo?  ni kwa sababu uliambiwa hivyo na watu au ni kwa sababu umezaliwa na kukuta watu wakifanya hivyo,kwa mfano wengi tumekuwa tukiwa na ufahamu kuwa shule ndio chanzo cha utajiri kwa sababu tuliambiwa hivyo ,kila siku tunatafuta ajira tukiamini kuwa tukipata tu tutaaga umaskini,lakini ambao tayari wamevipata hivyo ndio wengi wao wanakuja kufahamu ya kuwa kuna zaidi ya shule na ajira ili mtu kuwa tajiri.Hapa tunarudi kwenye namba moja ya kuwa ukishajifahamu wewe ni nani utaanza kutafuta mazingira ya kukupeleka kwako na hapo ndipo utaanza kuachana na ufahamu ambao chanzo chake ni kuaminishwa na watu,watu walikuaminisha vile kwa sababu ya ufahamu wao wa muda ule.


Makala hii imeandikwa na  Saul kalivubha,mwanasayansi na  mwalimu  na mmiliki wa fikia ndoto zako label.

0652 134707.

Tuesday 9 April 2019

HILI NDIO GEREZA LA HATUA ZAKO

Karibu tena kwenye blog hii inayotoa mafunzo ya maisha na jinsi ya kufikia ndoto zako.Ni tumaini langu kuwa wewe ni mzima wa afya na unaendelea kupambana katika utatuzi wa changamoto mbalimbali ili zikupe ushindi wa kuliishi kusudi lako,karibu tujifunze.


KUSUDI LA SOMO.
Somo hili linakusudia kuwasaidia vijana ambao wana tatizo la kutopiga hatua ilihali kila siku wapo kazini na wanapata chochote lakini hawapigi hatua mbele.Katika somo hili ,vijana lengwa ni wale ambao wana maono ya kuifikia hatua fulani lakini siku zasogea na hata dalili za kufika huko hazipo.Wewe pia una tatizo hilo? kama ndivyo ,endelea hadi mwisho utajua gereza lako ni lipi.


KWANINI UNAFANYA HICHO UNACHOKIFANYA LEO?
Hili swali linahitaji sababu ,je umewahi kujiuliza swali kama hilo? na ulipata sababu zipi? .Inawezekana ukawa na majibu yako mengi sana ya kwanini upo unafanya hiyo kazi,wengine watasema ni kwa sababu ndio walichokisomea,wengine watasema ni kwa sababu hawakwenda shule ndo mana wanafanya shughuli hiyo ,n.k.Majibu yatakuwa mengi sana.Mimi kama ningeulizwa swali kama hilo ,jibu langu lingekuwa rahisi sana tu,ningesema sababu inayofanya nifanye hiki nikifanyacho leo ni kwasabu kinanipeleka kwenye kusudi la kuumbwa kwangu. Hivi unafahamu gereza limelofunga hatua zako ni sababu zilipo nyuma ya hicho unachokifanya?

GEREZA LA HATUA YAKO MPYA NI HIYO SABABU YAKO.
 Ni ngumu kupiga hatua mpya kama huna sababu zinazokusuma ufanye hivyo ,na sababu ambazo zitakufanya upige hatua mpya zinategemea sana na wewe unajitambua vipi,hapa ninamaamisha kwamba ni vizuri kwanza ujitambue wewe ni nani na wapi unatakiwa kwenda kulingana na kusudi lililowekwa ndani yako,kisha sasa ndio uangalie hicho unachokifanya ,je kinahusiana vipi na uelekeo wako?

Kama kila siku sababu zako ni kutaka ufanye kazi kwa bidii na kwa weledi,sawa ni sababu nzuri lakini je hicho unachotaka kukifanya kwa juhudi na weledi kinahusiana vipi na kusudi la kuumbwa kwako? kama hakuna mahusiano ndipo pale ambapo utaendelea kuwa na juhudi kwa kufanya jambo fulani lakini hufiki kule kwako ,mfano kama wewe uliumbwa uwe mchoraji ,na sasa upo katika kitengo cha afya kama Daktari,je unaunganisha vipi huo udakitari na kipaji chako cha uchoraji? Hapo unaweza kuiwa na sababu nyingi za kukufanya huo udakitari wako vizuri lakini ukawa huna sababu hata moja ya kutaka ufanye huo udakitari wako uendeleze kiapaji chako ,kwa namna hiyo  utajikuta unaendelea kuwa gerezani tu .

UNATOKAJE KWENYE GEREZA HILO?
Kama nilivyotangulia kusema mwanzo ,kwanza lazima ujitambue wewe ni nani,kisha uangalie unafanya nini kwa sasa,na je ufanyacho kina mahusiano na wewe ni nani? kama hakuna mahusiano sio ukiache ghafla lakini tengeneza mahusiano ,yaani kitumie hicho unachokifanya kusaidia kusudi la kuumbwa kwako,mfano mimi naelekea kuibadili dunia kwa kupitia maandishi na kuongea lakini kwa sasa natumika hospitalini ,je niache kipi?  jibu la haraka ni kwamba navyovipata hospitalini navitumia katika kusukuma kusudi la kuumbwa kwangu ,hivyo nyuma ya haya niyafanyayo kuna sababu zinazoniambia nielekee kwenye ulimwengu wa maandishi na kuzungumza.
Jitahidi utengeneze sababu zinazokusuma kwenda kwenye kusudi lako ,kukosa sababu hizo kunapelekea hali ya kuridhika na hatua hiyo uliyopo ,na hapo ndipo panakuwa mwanzo wa kufanya kazi kwa bidii lakini mbele husogei ,unaishia pale ambapo sababu zako zilikutuma.

Makala hii imeandikwa na Saul Kalivubha.
            0652 134707