Tuesday, 25 August 2026

NAJUTA KUMPELELEZA MCHUMBA WANGU FACEBOOK 1

 

SEHEMU YA KWANZA “NAPOKEA FRIEND REQUEST”

Ilikuwa Jumapili nikiwa nimetoka ibadani nimetulia tu kitandani kusaka utulivu wa nafsi, masaa sikuwa nayakumbuka vizuri ila nachokumbuka tu ni kwamba nilikuwa kitandani nimejilaza ili nipumzike, katika kupumzika akili ikaniambia, "Peruza kidogo mitandaoni upate starehe."

Nikaanza na na Facebook, Bila kufikiria sana nikaona ombi la urafiki mpya Jina lilikuwa Koku Muganizi. Sikufanya upekuzi wowote kwa sababu ilikuwa si jambo jipya kukubali maombi kama yale hivyo haraka tu nikaibonyeza "kubali" na kuendelea na maisha yangu.

Baada ya dakika chache alama ya meseji ikaonekana, nilipoingia nilikuta jumbe 3 kutoka kwa huyo rafiki mpya:

"Mambo"

"Asante kunikubalia urafiki"

"Nimefurahi kuwa sehemu yako"

Kama mwanaume, ukipata ujumbe kutoka kwa jinsia ya kike moyo unakuwa mwepesi hivyo bila ajizi niliingia haraka kwenye profile yake nikakuta picha tatu tu za binti mtulivu, mstaarabu na mzuri.

Tukaanza kuzungumza kidogo kidogo lakini kitu kimoja kilinisumbua kichwani nacho ni jina lake halikunipa uhakika kwamba ni msichana kweli maana zama za leo utapeli ni mwingi sana hivyo nikaamua kumpima kwa utani ili kuthibitisha 

Mimi: "Yaonekana wewe ni msichana mtulivu sana" 

Yeye: "Kawaida tu hata wewe pia ni kijana mtulivu."

Jibu lake lilikuwa la haraka sana likafanya nikose la kusema zaidi.

Niliamka kwenda chooni, niliporudi nilishangaa kupata meseji yake kwenye WhatsApp na ilikuwa ni yeye yule yule wa Facebook, Moyoni nilisema, "Labda kachukua namba yangu mahali."Lakini kilichonifanya nisimame ni kitu kingine. Alikuwa ananiita kwa majina yangu yote matatu ya kuzaliwa.  Tatizo ni kwamba Facebook yangu ina majina mawili tu hilo la tatu nililificha, Sasa alilijulia wapi?

Sikumuuliza bali niliijaribu kujipa majibu yangu mwenyewe. "Labda Facebook inaongeza kiotomatiki."

 

Tulizidi kuwasliana mpaka kupeana historia zetu na hapo ndipo tukagundua kuwa tunatoka mkoa mmoja ingawa wilaya zetu ni tofauti yeye alikuwa Bukoba na mimi Muleba, Unajua furaha ya kukutana na mtu wa nyumbani nje ya nyumbani? Inaleta utamu tofauti kabisa.

Siku chache tu, tulikuwa tayari tumeshaingia kwenye mahusiano na wote tulikuwa w mbali na nyumbani, yeye kikazi na mimi pia lakini alinihakikishia kitu kimoja kuwa atakapokuwa na nafasi nitapita kukusalimia maana wote tulikuwa Dar es salaam. Maneno hayo kwa mwanaume ni kama mafuta kwenye moto hakuana asiyependa kutembelewa na msichana.

Siku moja akaniuliza: 

"Unajua tarehe 12 Mwezi wa Sita ni siku yangu ya kumbukizi kuzaliwa?"

Nilijibu kwa furaha: "Nitakutumia kitu hata kama ni zawadi ndogo na kama tutaonana tutasheherekea pamoja" 

Akanijibu: "HAPANA SHAKA. KUNA SIKU ITATUKUTA PAMOJA." Japo tulikuwa pamoja Dar ila sikutaka kuonekana ninaharakisha sana kuoanana naye, Japo ndani yangu kulikuwa na swali moja linaninyima usingizi: Alipata wapi namba yangu? Na alijua vipi jina langu la tatu?

Nikaamua kufanya upelelezi wangu mdogo, nikaangalia kama tunachangia marafiki na kweli, nilimkuta ana rafiki mmoja tuliyesomea naye hapo moyo ukatulia kidogo. Lakini kabla sijapumua, akanitumia ujumbe: 

"Mbona unaonekana una hofu?"            

Nikajibu: "Sina hofu." 

Akarudi tena: "Nafahamu una hofu ya wapi nimepata mawasiliano yako ni rafiki zako. Ndio wamenipa namba yako na majina yako yote."

Damu yangu iliganda, kafahamu vipi kuwa nilikuwa na hofu? Nikaamua kuwapigia wale marafiki zangu na wote walinipa jibu moja:  "Tunamjua tu Facebook ila hatujawahi kuzungumza naye" Nikiwa bado kwenye mshtuko huo, ndipo ujumbe wake mpya ukaingia:  "Wale rafiki niliokwambia sio hawa wa Facebook."

Hapo ndipo hofu yangu ilipanda kilele, Huyu mtu ni nani? Nilijaribu kujituliza. "Labda ni mtu tu aliyenifahamu barabarani akampa taarifa zangu."

Tarehe 12 Juni ilifika ambayo ni siku ya kumbukumbu yake ya kuzaliwa na asubuhi nilimtumia ujumbe wa kumpongeza na kumuahidi kumtumia pesa anunue hata soda., Alifurahi. Baadaye mchana Facebook ilinijulisha: "Leo ni siku ya kuzaliwa kwa Koku Muganizi."  Niliingia kwenye ukurasa wake na picha yake ilikuwa nzuri sana hata kwenye sehemu ya maoni watu wengi walikuwa wakimiminika kumtakia heri ya kuzaliwa japo sikufanikiwa kusoma ila niliamini hivyo. Nilijaribu kusoma sasa maoni lakini hayakufunguka, Nikajaribu kuandika yangu ya kumtakia heri nayo yakakataa nikasema, "Labda ni mtandao."

Akanitumia ujumbe: "Leo Facebook yangu haiko sawa." 

Nami nikakubaliana naye lakini akaniambia, "Jaribu tena."

Niliporudi, mwisho maoni yalifunguka nikapiga hatua kuteremka ili nione ni nani kamtakia heri. niliwaza, kama ana mchumba lazima nimpate hapa kisha nikakutana na maoni ambayo yalibadilisha kila kitu kwenye fikra zangu kwanza maoni mengi yalikuwa kwa lugha nisiyoelewa. labda ni lugha ya kwao, nikajidanganya pili nikaona lipo moja kwa Kiswahili hapo Roho yangu ikatetemeka.

Lilisomeka hivi: 

"Vipi mbona msimu huu umetucheleweshea Damu?"

Naye akajibu: 

"Punde tu mtapata. Si mnajua ugumu ulivyo sasa kuipata?"

Damu?

 Malenga wa Kiha

 Mwanasayansi Saul Kalivubha

 255652134707

Saturday, 3 January 2026

HII KAULI YA " KAMA NI WAKO BASI ATAKUWA" IMEHARIBU WENGI WANAOITAFASIRI NDIVYO SIVYO.

Hii kauli imefanya watu washindwe kujitafajari pale wanapopoteza kwa kujifariji kuwa HAIKUWA RIDHIKI .

Inaweza kuwa ni ridhiki yako ndio lakini ukaipoteza kwa ujinga au tabia zako na kwa sababu ya hiyo faraja unayoijipa  unabaki kuamini tu kama ni chako kitakuwa na kama sivyo kitaondoka lakini swali ni je hata kama ni CHAKO KITAKAA KWENYE TABIA ZISIZO RAFIKI?

Wengi hutafasiri kuwa  kwa sababu tu ulipangiwa basi wewe huna mambo ya kufanya ili kufanya hayo mambo yaje na kudumu kwako badala yake unabweteka ukisubiri tu sasa kwa namna hiyo UTASUBIRI SANA BILA MAFANIKIO.

Ukisoma ajira hazikutafuti bali wewe ndio unatakiwa uzitafute .

Mchumba sahihi atakaa kwako ikiwa tu umeweka mazingira rafiki kwake la sivyo watakuja na kuondoka nawe utabakia tu kujifariji kuwa KISICHORIDHIKI HAKIKAI 


#Mwanasayansi Saul kalivubha 

#Fikia Ndoto Zako

Monday, 6 October 2025

MAMBO YA KUFANYA ILI KUVUKA KIPINDI CHA KUKATALIWA BILA WEWE KUDHURIKA

Kukataliwa sio kitu kigeni kwa sababu uzoefu unaonyesha karibu kila mtu ameshaonja kipindi hiki na hata kama bado basi kuna siku utakipitia .

Inaweza kuwa ndugu, marafiki, makazini au katika mahusiano kote kuna kakataliwa .

Ni kipindi kigumu sana kukabiliana nacho kwa sababu ki asili binadamu tunapenda kukubaliwa hivyo ianapotokea kukataliwa maumivu yake huwa ni makali sana bila kuwa na  ukomavu athari huwa kubwa ikiwemo na kujitoa/kutoa uhai .

UFANYEJE SASA UKIWA KWENYE KIPINDI HICHO?

1.Kubali ukweli (Ukiruka hii hatua utakuwa unajidanganya kuwa uko sawa ila ki uhalisia bado unateseka hivyo lazima ukubali kuwa HAKUTAKI)

2.Ondoa matumaini kuwa kuna siku ATAJIRUDI ( Usiwe na hayo matumaini kwa kuamini ipo siku atajirudi ukaanza kuwa unamtumia meseji mara unamjulia hali au kuendelea kumshirikisha mambo yako kwa tumaini kuwa atakuonea huruma arudi , utateseka)

3.Usitake umsahau kwa kutafuta mbadala wake( kosa kubwa sana hili )

4.Wekeza nguvu kwenye mambo mengine na futa matukio ambayo yatafanya umkumbuke ikiwemo picha kama mlipiga wote au kusikia nyimbo ambazo mlizipenda kwa pamoja)

5.Usijione mwenye kasoro za kukataliwa ( usianze kutafuta sababu za kujiona hufai)

6.Usianzishe maigizo ya kuaminisha watu kuwa upo sawa na soko lako lipo juu 

7.Muda ndio kidonge cha mwisho kumaliza maumivu yako( Huwezi kuwa sawa kesho itachukua muda hivyo kubali hilo)

8.SHUKURU MUNGU KUKATALIWA KWA SABABU KUNA SEHEMU KAKUANDALIA YA KUKUBALIWA 🙏 


NB : KUCHELEWA KUKUBALI KUKATALIWA NI KUENDELEA KUJICHELEWESHA WEWE MWENYEWE 😔 

#Mwanasayansi Saul kalivubha 

#Fikia Ndoto Zako 

+255652 134707

Thursday, 26 June 2025

UTULIVU NI JICHO LA TATU KUKUPA MAAMUZI SAHIHI HASA KWENYE NYAKATI ZA KUVURUGWA

 

Walioachwa kwenye mahusiano wakakurupukia mengine haraka wakiwa kwenye hali ya  kuvurugwa wengi  wao walijikuta wakikosea tena vibaya zaidi ya mwanzo.

Waliofumania wenzi wao au kusikia taarifa mbaya dhidi ya wenzi wao na wakafanya maamuzi wakiwa kwenye hali ya kuvurugwa wengi walijikuta kwenye maamuzi mabaya na yenye majuto kama vile kuua au kujiua.

Waliojibizana wakiwa kwenye hali ya kuvurugwa wengi walijikuta wakiongea maneno ya hovyo na yaliyokosa hekima kiasi cha kujipotezea heshima. 


Furaha na huzuni vyote vinaweza kupoteza utulivu wako na utulivu ukipotea basi tarajia maamuzi ya hovyo kwa asilimia kubwa. 

Adui wabobevu wanalijua hilo ndio maana wakitaka kukushambulia kirahisi basi watatafuta namna ya kukuvuruga na kukushinikiza ufanye maamuzi ukiwa kwenye huo mvurogo wakiamini ni lazima utakosea tu.

Utulivu ndio silaha pekee kwenye nyakati kama hizo na hapo utapata jicho la tatu la kuona hali halisi na maamuzi gani uchukue .

#Mwanasayansi Saul kalivubha 

#Fikia Ndoto Zako

#Mitandaoni @Fikia Ndoto Zako 

Wednesday, 14 August 2024

UKIZALIWA FAMILIA MASKINI JUA TAYARI UMEKUWA JESHI LA MTU MMOJA MSITUNI

 UKIZALIWA FAMILIA MASKINI JUA TAYARI UMEKUWA JESHI LA MTU MMOJA MSITUNI, ACHA KUDEKA. 

Maisha hayako sawa hilo lazima tukubali   na usipolikubali basi utashindwa kupambana kulingana na mwanzo wako ulivyo , Kwa mfano kuna kuna ambao wanarithishwa mali waendeleze na kuna wanaorithishwa matatizo wayatatue.

Kuna ambaye akipata kazi tu hupongezwa kwa kupewa  kiwanja cha nyumba ama fungu la pesa na kuna wewe ambaye ukipata kazi tu matatizo yanaongezeka yaani utatakiwa ujengee wazazi, usomeshe watoto wa ndugu zako na kisha ndio uanze kujiimarisha .

Wewe ambaye simu zote unazopigiwa ni za matatizo usijilinganishe na ambaye hupigiwa simu kwa kukumbukwa, Wewe ni jeshi la mtu mmoja tayari hivyo usitegemee msaada wowote wa kivita kutoka nyuma wala mbele hivyo ni kupambana tu mpaka kieleweke .

Mambo ya kudeka waachie wenyewe ila wewe tambua ukifeli ndugu zako wataumia zaidi kuliko hata wewe muhusika kwa sababu umebeba matumaini ya wengine .

Kila siku historia ya ulipotoka iwe inakukumbusha kuwa WEWE NI JESHI LA MTU MMOJA MSITUNI. 

#Mwanasayansi Saul kalivubha.

#Fikia Ndoto zako 

+255652 134707

Thursday, 1 August 2024

MASKINI ATABAKI KUWA MASKINI TU KAMA ATAENDELEA KUWA NA MARAFIKI MASKINI 😔

 MASKINI ATABAKI KUWA MASKINI TU KAMA ATAENDELEA KUWA NA MARAFIKI MASKINI 😔


Hii sio makala nzuri kwa maskini ambao wameridhika na hali hiyo  hivyo kama umeridhika na umaskini basi acha kabisa kusoma ila kama upo kwenye vita ya kujikwamua kama mimi basi inawezekana ikawa makala yenye mwanzo mpya kwako. 

Ukipokea simu kutoka kwa maskini iwe ni ukoo wako au rafiki zako huko kijijini kama sio ya kukuomba pesa basi itakuwa ya majungu tu, mtaongea majungu kisha mtaagana na baada ya hapo kila mmoja atabaki anatafakari hayo majungu mpaka usiku utafika mtalala na siku itakuwa imeisha hivyo , kweli hapo umaskini utaisha?


Ajabu ni kuwa huyo aliyekupigia simu kwa zaidi ya nusu akikupa majungu siku ikitokea fursa inayohitaji mtu wa sifa yako hatokupa na siku ukijua ukamuuliza atakwambia hakuwa na salio ( vocha ) siku hiyo , Inashangaza na kuchekesha kidogo .



Umaskini ukiwa damuni huwa wahusika wanapendana wakiwa na umaskini wao ila wana wivu mkali siku wakisikia una mipango ya kutaka kuagana na umaskini.

Ukitaka kujua hilo wapelelee habari nzuri maskini rafiki zako utachopkea kwa asilimia kubwa ni kukatishwa tu tamaa kwa kupewa mifano ya watu waliokuwa kama wewe ila wanashindwa na na huo ni ujumbe kwako kuwa achana na mipango hiyo na kwa sababu unaogopa usiwapoteze marafiki zako basi unaamua kuwasikiliza na kughairi harakati zako za kuagana na umaskini. 

Waepuke maskini wa namna hiyo kwa kila hali , hili haliwezekani kwa maskini wanaopenda kuwa maskini ila ni rahisi kwa maskini ambao wapo kwenye harakati za kujikomboa ndio maana awali nilikatunguliza hii makala haiwahusu maskini walioridhika kwa umaskini wao.

KWANINI UWAEPUKE MASKINI?

Kwa sababu wengi wao ( sio wote) watakuwa wanakujaza majungu tu na sio kukupa fursa( njia za kujikwamua)  na usipokuwa makini watakufanyia kitu kibaya endapo wakijua una mipango mizuri ya kuwa tajiri.


Mwanasayansi Saul kalivubha 

Instagram @fikia ndoto zako 

+255652 134707

Thursday, 11 July 2024

HII NDIO KANUNI YA KIJASUSI YA KUISHI NA WATU AMBAO HAWATAKI KUONA WENGINE WAKIFANIKIWA

 KIJASUSI WAPE USHINDI WALEWE ILI WAACHE KUKUFUATILIA BALI WASHANGAZWE KWA MATOKEO.


Jasusi yoyote Duniani huwa habishani na mtu zaidi atakubaliana na wewe ili uvimbe kichwa lakini moyoni mwake hajakubali na kitachokushangaza ni matokeo. 

Hii ni mbinu moja wapo ya kuishi na watu ambao hawataki wengine wafanikiwe kwa kujiona wao ndio wanajua kila kitu , ukisema ujionyeshe ni zaidi yao kwa maneno watakufuatilia sana ili kuzima harakati zako hivyo wewe wape ushindi tu .

Sifa kubwa ya wajuaji kama hao huwa wanapenda sana sifa na kuonekana wao ni zaidi ya yeyote na siri kubwa kuhusu watu hawa huwa wanalewa sifa yaani wakipewa sifa tu tayari wanajisahau hivyo tumia madhaifu haya kuishi nao.

Ukiwapa ushindi watakuona wewe ni bwana mdogo tu na hata siku moja hutokuwa juu sasa kipindi wanashangalia kwa kukuona hivyo wewe pambana kwani hawatakuwa na umakini kwako wakijua tu wewe ni wa kushindwa.

Wakikwambia wao ndio wa mjini na hakuna wa kuwashnda wewe wakubalie kuwa ni kweli wapo hivyo ila ki uhalisia unawaona kabisa hawana lolote ila majigambo tu na huo utakuwa muda mzuri sana kufanya vitu vikubwa bila wao kukufuatilia.

Kwanini hawakufuatilii? Kwa sababu umwapa ushindi hivyo wanajiona washindi na kukuona wa kushindwa tu, Tumia huo muda vizuri. 


#Mwanasayansi Saul kalivubha 

#Fikia Ndoto zako 

+255652 134707