Friday 21 February 2020

USIYOJUA KUMUHUSU SAUL KALIVUBHA

USIYOJUA KUMUHUSU SAUL KALIVUBHA.

Karibu sana ndugu mpenzi msomaji wa blogu yako pendwa hii ya fikiandotozako ambayo inakupa  mafunzo mbali mbali ya maisha na bila kusahau kutufuatilia katika majukwaa yetu ya Facebook, you tube na Instagram kwa jina moja tu la FIKIANDOTOZAKO,  Karibu sana.

Leo ni somo la tofauti sana kama zawadi kwako  ikiwa ni sherehe ya kumbukizi ya  siku ya kuzaliwa kwangu nikiwa natimiza umri wa miaka 28 , ulifikiri nina umri gani kabla?.Nawashukuru sana wazazi wangu na nyinyi wapenzi wasomaji kwa kuwa nami karibu katika kujifunza mambo mbali mbali ya maisha.

SAUL KALIVUBHA  ni nani? na itakusaidia nini kumfahamu? twende sambamba mpaka mwisho wa darasa kuna kitu utajifunza.

1.Ni mzawa wa Kigoma katika familia yenye uchumi wa kawaida sana (uchumi wa daraja la tatu) yaani uchumi wa mwisho kutokea  uchumi wa juu, uchumi wa kati na uchumi wa mwisho, hivyo Saul Kalivubha katokea familia yenye uchumi wa mwisho.

2.Ni mtu wa kundi la watu wasiowaongeaji sana na wenye usiri mkubwa sana (melancholic) , hili ni kundi la watu ambao muda mwingi hupenda kukaa peke yao kuliko kuwa na makundi, faida ya kundi hilo mojawapo ni kuwa wabunifu na wenye kufikiria sana lakini pia hasara moja wapo ya watu wa kundi hilo ni kuumia sana kwa sababu hukaa na mambo mengi moyoni bila kushirikisha wengine (marafiki).

3.Kasoma katika mazingira magumu kuanzia shule ya msingi mpaka shule ya upili, mazingira magumu yalimfanya atoke shule ya vipaji maalumu ya Musoma wavulana sekondari ya ufundi na kurudi shule ya kata ambapo alisoma kidato cha kwanza mpaka cha nne, hilo halikumkatisha tamaa zaidi ya kujitoa zaidi akiwa shule hiyo ya kata na kupata matokea mazuri ya kuendelea kidato cha tano na sita .

4.Maisha ya kidato cha tano na sita katika shule ya bwiru wavulana pia hayakuwa rahisi ki uchumi kwani ilimlazimu awe anasoma huku akitafuta pesa za kulipia michango midogo midogo ya shuleni.

5.Ugumu wa maisha ya shule hamkufanya akate tamaa hivyo alipambana na vikwazo na hatimaye akapata ufaulu wa kumfanya aendelee na masomo  ya chuo kikuu japo hakuweza kwenda mwaka huo aliomaliza shule (2014) na akaenda chuo mwaka uliofata (2015).

5.Mwaka 2015 aliweza kujiunga na chuo kikuu cha afya na sayansi shirikishi (Muhimbili) kwa kozi ya Mwanasayansi tiba wa maabara za binadamu (Medical laboratory science) .Maisha ya chuo hayakuwa magumu sana ki uchumi kulinganisha na hatua za nyuma hivyo kidogo unafuu ulionekaa wa maisha.

6.Maisha ya chuo yana changamoto nyingi sana lakini pia ni jukwaa zuri sana la kujifunza maisha kwa upana zaidi kwani unakutana na watu wengi mnaopishana mitizamo hivyo kupitia kupishana huko mtu unajifunza mambo mengi sana.

7.Safari ya uandishi ulianza rasmi akiwa chuoni mwaka wa pili ni safari isiyo rahisi lakini ilikuwa ndio mahala pake kwani kukutana na watu wengi wenye upeo tofauti ilimfanya ajifunze zaidi na kuanzisha jukwaa la FIKIANDOTOZAKO ambalo hadi sasa linafikia watu wengi nchini na nje ya nje katika kuwafungua vijana namna na kuwapa moyo wa kuendelea mbele.

8.Saul Kalivubha sasa sio mwanafunzi tena tayari ni muhimu  haijalishi changamoto zipi zilijitokeza lakini safari iliisha salama.Vikwazo vya maisha ni vingi sana  lakini hupaswi kusema nimeshindwa kwa sababu hakuna safari rahisi japo ugumu unatofautiana kulingana na aina ya safari uliyonayo.

9.kuna muda unahisi wewe utabaki hapo hapo ulipo kulingana na vikwazo vinavyofanya usione njia mbele, safari inakuwa na giza   na Dunia hata siku moja haitambui shida zako hivyo haiwezi kukuonea huruma. Muhimu ni kutoa imani  ya kubaki ulipo kwa sababu maisha ya leo yatakufunza funzo la kuishi kesho hivyo kesho utakuwa mtu mpya kabisa ni uvumilivu tu.

10.Uvumilivu sio kazi rahisi hata kidogo ni kazi ngumu sana kwa sababu silaha pekee ya uvumilivu ni IMANI  , unavumilia ukiwa na tumaini kuwa hali hiyo itapita na kweli itapita  kwa sababu  njia unazohisi zitakupa mafanikio ya haraka zina gharama iliyo nje ya uwezo wako zitakufanya ufilisike na bado hayo mafanikio usiyaone , tembea mwendo wako kwa kufuata nchi yako (Mungu aliyokuandalia).

Makala hii imeandikwa na.

 #Mwanasayansi Saul Kalivubha
  #0652 134707