Tuesday 11 April 2023

SABABU ZITAKAZOFANYA UKOSEE KUCHAGUA MWENZI WA MAISHA.

SABABU ZITAKAZOFANYA UKOSEE KUCHAGUA MWENZI WA MAISHA.

Ni jambo la kawaida kuishi wawili( mke na mume) ambapo nyuma ya kuishi pamoja kuna maandalizi ya kumtafuta huyo mwenza hivyo kuna wakati ukifika karibu kila mtu anakuwa na picha ya yupi anamtafuta ndio maana kuna ambao utawakataa na kuna wengine utawakubali , hali ya kumkataa mmoja na kumkubali mwingine ni dalili kuwa kichwani mwako kuna picha ya umtakaye na huyo uliyemkubali ndio picha halisi ya umtakaye, lakini kwa hali isiyoyakawaida kuna kipindi unamchukia uliyemchagua au unaona makwazo kwa aliyekuchagua ilihali yeye ndiye aliyefanya maamuzi ya kukuchagua, hii chanzo chake ni kipi?.

Katika harakati za kumtafuta mwenzi huwa kuna mengi sana nyuma ya zoezi hilo na hapo ndipo huwa kuna kupatia au kukosea zoezi hilo na moja ya sababu hizo ni kama zilivyojadiliwa hapa chini :

Kumtafuta mwenzi kwa ulimbukeni, Limbukeni kwa tafasiri ya haraka ila makinifu ni mtu mshamba au mtu ambaye anakurupukia vitu bila kuwa na ufahamu navyo . Kuna mtu anakuchagua kama mwenzi wake kwa ulimbukeni tu ila kikawaida ingefaa ajitulize sana kabla ya maamuzi yake hayo sasa baadaye mkiwa tayari mpo naye anakuja kugundua kuwa kumbe sio wewe anayekutafuta hapo sasa anaanza kukuchonga ili uwe yule anayemtafuta na hapo ndipo ataanza kukukosoa kila siku .

Kumchagua mwenzi bila utulivu, hii inatokea hasa kwa mtu ambaye anajiona kachelewa hivyo anakuwa haangalii tena vigezo bali anaangalia tu mtu yupi yupo tayari ( kama ni mvulana anaangalia msichana yupi yupo tayari na kama ni mvulana basi anaangalia msichana yupi yupo tayari ) Hapa kukosea ni rahisi sana japo inawezekana ukabahatisha lakini hiyo ni kwa wachache sana wengi hukosea.

Kupitia kipindi cha kukataliwa sana! Mtu aliyepitia kipindi cha kukataliwa sana asipojithibiti kuna uwezekano mkubwa akaja kukosea kuchagua mwenzi kwa sababu atajiona mwenye mkosi sana sasa siku akikubaliwa na yoyote ataona kama bahati hata kama huyo aliyemkubali si sahihi. 

Kufanya maamuzi haraka baada ya kuachwa! mtu anapoachwa huwa hana utulivu na ile hali inamfanya akose utulivu kwa sababu ile hali ya kurudi tena single ( pekee) inampa msongo na anakuwa anataka asionekane hana soko hivyo anaweza kuamua kumkubali yoyote bila kujali ni sahihi au la.

Shinikizo la wengine! Hii ni pale ambapo unataka kuendana na wengine bila kujali kuwa ni wakati sahihi au la bali anataka tu afanye kama wengine kwa mfano marafiki zake wote wameoa bado yeye tu hali hiyo inamfanya na yeye aamue kuoa .

Kukimbia umri! Hii ni sababu nyingine kubwa ya kukosea kwa sababu Kukimbia umri kuna fanya uchague bila kuzingatia ubora wa unachokitaka , na hatimaye kujikuta umekosea. 


Makala hii imeandikwa na Mwanasayansi Saul Kalivubha 

Kitabu cha siri za urafiki kinapatikana soft copy ( nakala tete) kwa Tsh4000. 

0652 134707/0756388688