Thursday 30 April 2020

UNATAFUTA MAISHA? HAYA HAPA.

UNATAFUTA MAISHA ? HAYA HAPA.

Karibu ndugu msomaji kwenye blogu yako hii pendwa ya FIKIA NDOTO ZAKO  ambapo tunajifunza mengi sana kuhusu maisha ya kila siku.Tupo kwenye hali ya taharuki nakusihi sana ufaute ushauri wa watalaamu na kwa ushauri wangu wa nyongeza katika uchumi kwa sasa kutunza pesa iwe lengo la kwanza  kwa sababu mfumo umeyumba kwa janga hili la Corona hivyo inahitaji utulivu sana kabla ya kuwekeza pesa yako vinginevyo utaisaidia Corona badala ya kujisaidia wewe, tuwe watulivu na hali hii itapita.


Tuachane na stori twende moja kwa moja kwenye somo letu maalumu kwa leo kabla ya vyote nikuulize na wewe upo kundi la watu wasemao " NINATAFUTA MAISHA" umewahi kuyapata? .

Kwa mujibu wa kamusi mbali mbali  MAISHA ni hali ya wewe kuwa mzima tayari hayo ni maisha  hivyo mtu ambaye ni mfu huyo hana maisha Duniani pengine huko aendako ( kuna imani nyingi kuhusu maisha baada ya kifo sitaki twende huko) .Tayari maisha unayo hivyo jivunie kuwa na maisha.
UHAI ni kitu ambacho kinafanya wewe  uwe na maisha mfano chakula ni uhai, maji ni uhai  nk kwa sababu ukivikosa unaweza kupoteza maisha ( kufa).
KUISHI ni namna ya kutetea maisha yako hapa ndipo kiini cha somo, maisha unayo lakini unafanya nini ili UISHI?

Ili uishi kuna mahitaji muhimu ya kwanza ambayo ni CHAKULA na MALAZI ( ule upate na pakulala) kwa sababu ukikosa chakula utakufa, ukilala nje uanaweza shambuliwa na wanyama wakali ukafa .

Mtu akiwa na Nyumba nzuri, gari zuri na kula vyakula vizuri ki kawaida hiyo ni hali ya kawaida na sio mafanikio ya kujitamba kwa sababu ni kawaida ule na upate pakulala ili kutetea uhai wako mambo ya gari ni ziada tu lakini gari halitetei uhai wako. Hatua hii ya kula na kuishi ni hatua ambayo kama umeifikia kujipatia mahitaji hayo tayari unatetea uhai wako  ( magonjwa , ajari nk ni changamoto tu katika kuwinda uhai wako).

HATUA YA PILI NA KUBWA. Kujitofautisha kutoka kwenye kutetea uhai wako tu mpaka kutetea maisha ya wengine hii ni hatua kubwa zaidi ambayo tunaiweka kwenye SAIKOLOJIA na FALSAFA  yaani kujitambua kuwa kuna zaidi ya kula na kulala na starehe. Hapa ni kutafuta wewe halisi ni nani, je ni mwimbaji? Mchezaji mpira  nk.

WEWE HALISI NI NANI? Watu wanaofanikiwa kujitambua hivyo huwa wanaonekana wa tofauti sana kwenye jamii  na kile wanachokifanya hakitetei uhai wao tu bali kuna wengine wanafaidika pia  mfano tuseme msanii Diamond kuimba kwake kuna mfanya atetee uhai wake lakini pia kuna ambao wameajiriwa naye lakini pia kuna watu ambao hisia zao zinapona kwa kusikia tu nyimbo zake.

UNATAFUTA MAISHA? Maisha unayo ila unatafuta namna ya kutetea uhai wako lakini namna nzuri usiishie kwenye kula, kulala na starehe ila tafuta wewe halisi ni nani? Tafuta kipaji chako na ukiishi. Kuishi kipaji chako ni nyongeza kubwa sana ya KUTETEA UHAI WAKO NA WENGINE. Kipaji sio kuimba tu na kucheza mpira au kuandika hapana hata ubunifu nao ni kipaji,kuchora, kushona  nk yaani ni vile tu unaishi kile ulichoombwa kufanya na njia rahisi ya kukijua ni msukumo wako wa ndani unajihisi furaha yako ipo ukiwa unafanya nini?

Makala hii imeandikwa na
Mwanasayansi Saul Kalivubha.
fikiandotozako.
Bila kusahau vitabu vya siri za urafiki na thamani ya changamoto vinapatikana kwa bei ya ofa kwa Tsh 6000 tu vyote, ni soft copy ( nakala tete).
 0652134707/ 0756388688.