Monday 3 October 2022

 USISUBIRI PESA IPUNGUE NDIO UWEKE NIDHAMU YA MATUMIZI

Matumizi ya pesa bado ni changamoto kwa watu wengi na matokeo yake hujikuta katika ukosefu wa pesa wa mara kwa mara na hii sio kwa waajiwa tu hata waliojiajiri kwenye mambo yao binafsi  bado hujikuta kwenye kipindi kigumu cha ukosefu wa pesa sio kwa sababu haikuwepo la hasha ni kwa sababu ilikuwepo lakini ikatumiwa bila kuzingatia matumizi sahihi kutokana na kipato. Ukipata muda tulivu ukajitafakari utagundua kuwa pindi upatapo pesa matumizi yako yanakuwa juu na hupungua kadri pesa inavyopungua yaani kwa lugha rahisi  ni kuwa nidhamu yako ya matumizi ya pesa inaongezeka kadri unavyoishiwa pesa. 

Pesa ni nguvu ya kihisia ambapo usipoitawala itakutawala yenyewe kwa kukupa maamuzi mengi na hapo utakosa utulivu hali ambayo itafanya upoteze nidhamu ya matumizi ndio maana mshahara ukiingia unaweza jikuta unafanya manunuzi bila kuangalia ukubwa wa gharama kwa sababu unajua pesa ipo lakini ukianza kusikia mfuko umepwaya ndio utarudisha makini wa matumizi kwa mfano mwanzo ulilipwa laki tano na ilipofikia mfukoni umebaki na laki moja ndio utaanza kuipigia mahesabu hiyo laki moja kuangalia kama itakufikisha mwezi mwingine, je kwa nini hukufikiria hivyo tangu ukiwa na laki tano? 

Nidhamu ya pesa ni kuheshimu pato lako kwanza na pili ni kuheshimu matumizi sahihi yaliyo ndani ya kipato chako kama ulipanga kununua kitu cha shilingi mia ndio itakuwa sawa kulingana na kipato chako basi fanya hivyo lakini ulinunua kwa shilingi Mia mbili ujue umekula na pesa ya siku fulani hivyo jiandaye siku hiyo kukosa pesa la sivyo iwe ni dharura ndio tumia lakini kama si dharura yatakiwa ujidhibiti dhidi ya matumizi ya pesa pale tu unapoipata, changamoto ya pesa ni kuwa ukitumia pesa ndogo unaona kawaida tu lakini mwisho wa siku ukijumlisha unakuta kama ungehifadhi ungekuwa mbali sana kifedha hivyo nidhamu ukianza na kuheshimu matumizi yako yaliyo ndani ya kipato chako utakuwa kwenye kiwango kizuri cha kuweka akiba. 

Nidhamu binafsi katika matumizi ya pesa inajengwa na lengo kuu ulilonalo la kesho hapo ndio utakuwa unatumia pesa ukikumbuka kesho hivyo utakuwa ukijikumbusha kila kabla ya matumizi ambayo si salama kulingana na kipato chako na utakuwa na nidhamu muda wote, lazima uwe na nidhamu au ukose nidhamu lakini ukubali kupoteza lengo kuu la kesho na njia nzuri nyingine ni kuigawa pesa yako kwa siku utagundua unaingiza shilingi ngapi kila siku na kisha angalia matumizi yako kila siku yanaendana na pato lako la siku? Kwa kuanzia na hapo utajirekebisha kimatumizi na utaheshimu matumizi sahihi ya pesa. 

Pesa ikiwa nyingi itakupa upofu wa kuamini kuwa huwezi kuishiwa hivyo kila matumizi yakujiayo kichwani utayafanya na hapo ndio mwanzo wa kutumia hovyo pesa  mpaka baadaye ikipungua ndio itakutoa upofu uone kuwa kuna hatari itokanayo na ukosefu wa pesa kwa sababu pesa uliyonayo haitoshi kukufikisha msimu mwingine wa pesa kumbe kuna kuna nguvu kubwa inatakiwa uwe nayo awali ili kudhibiti hisia za pesa zisikutawale. 

Kujua unataka nini pia ni moja wapo wa ujenzi mzuri wa nidhamu ya pesa kwa sababu utajizuia dhidi ya matumizi ambayo sio ya msingi kwako na hayapo ndani ya bajeti yako kwa kipato chako na aina yako ya safari uliyonayo, kutojua nini unataka itakuingiza kwenye matumizi yasiyo sahihi kwa sababu kila utakachokiona kinavutia utahitaji kukinunua. Pesa isikuendeshe bali unatakiwa wewe ndio uipangie majukumu  na ukiona unalemewa basi jitahidi usiwe unatembea na pesa nyingi mfukoni hii ni njia nzuri pia ya kuitawala pesa kwa sababu huwezi kufanya manunuzi yasiyo na mpangilio, tunafanya manunuzi yasiyo na mpangilio kwa sababu tunakuwa na pesa au urahisi wa kuipata pesa. Usikumbushwe na matatizo bali jikumbushe mwenyewe kuwa kuna siku changamoto zitatokea na uhitaji wa pesa utatakiwa na sio usubiri matatizo yakufikie ndio uone umuhimu wa kutunza akiba kabla. 

Njia nyingine nzuri itakayokifanya uwe na nidhamu ya pesa wakati wote ni kupunguza matumizi yasiyo na lazima na kujenga utaratibu wa kununua vitu vya jumla kuliko vya reja reja  na pia kusimamia lengo kuu kwa msimu kwa mfano kila mwaka uwe na lengo kuu la kufanya hivyo kwa namna yoyote utajibana ubaki na pesa ya kufanikisha lengo hilo  maana ukitumia hovyo pesa basi uwe tayari pia kulipoteza lengo hilo 


Mwanasayansi Saul Kalivubha 

0652 134707

Thursday 28 July 2022

NAMNA YA KUWEKA NIDHAMU YA PESA

NIDHAMU YA MATUMIZI SAHIHI YA PESA 

Matumizi ya pesa bado ni changamoto kwa watu wengi na matokeo yake ni hujikuta katika ukosefu wa pesa mara kwa mara na hii sio kwa waajiwa tu hata waliojiajiri kwenye mambo binafsi  bado hujikuta kwenye kipindi kigumu cha ukosefu wa pesa sio kwa sababu haikuwepo la hasha ni kwa sababu ilikuwepo lakini ikatumiwa bila kuzingatia matumizi sahihi kutokana na kipato. Ukipata muda tulivu ukajitafakari utagundua kuwa pindi upatapo pesa matumizi yako yanakuwa juu na hupungua kadri pesa inavyopungua yaani kwa lugha rahisi  ni kuwa nidhamu yako ya matumizi ya pesa inaongezeka kadri unavyoishiwa pesa. 

Pesa ni nguvu ya kihisia ambapo usipoitawala itakutawala yenyewe kwa kukupa maamuzi mengi na hapo utakosa utulivu hali ambayo itafanya upoteze nidhamu ya matumizi ndio maana mshahara ukiingia unaweza jikuta unafanya manunuzi bila kuangalia ukubwa wa gharama kwa sababu unajua pesa ipo lakini ukianza kusikia mfuko umepwaya ndio utarudisha makini wa matumizi kwa mfano mwanzo ulilipwa laki tano na ilipofikia mfukoni umebaki na laki moja ndio utaanza kuipogia mahesabu hiyo laki moja kuangalia kama itakufikisha mwezi mwingine, je kwa nini hukufikiria hivyo tangu ukiwa na laki tano? 

Nidhamu ya pesa ni kuheshimu pato lako kwanza na pili ni kuheshimu matumizi sahihi yaliyo ndani ya kipato chako kama ulipanga kununua kitu cha shilingi mia ndio itakuwa sawa kulingana na kipato chako basi fanya hivyo lakini ulinunua kwa shilingi Mia mbili ujue umekula na pesa ya siku fulani hivyo jiandaye siku hiyo kukosa pesa la sivyo iwe ni dharura ndio tumia lakini kama si dharura yatakiwa ujidhibiti dhidi ya matumizi ya pesa pale tu unapoipata, changamoto ya pesa ni kuwa ukitumia pesa ndogo unaona kawaida tu lakini mwisho wa siku ukijumlisha unakuta kama ungehifadhi ungekuwa mbali sana kifedha hivyo nidhamu ukianza na kuheshimu matumizi yako yaliyo ndani ya kipato chako utakuwa kwenye kiwango kizuri cha kuweka akiba. 

Nidhamu binafsi katika matumizi ya pesa inajengwa na lengo kuu ulilonalo la kesho hapo ndio utakuwa unatumia pesa ukikumbuka kesho hivyo utakuwa ukijikumbusha kila kabla ya matumizi ambayo si salama kulingana na kipato chako na utakuwa na nidhamu muda wote, lazima uwe na nidhamu au ukose nidhamu lakini ukubali kupoteza lengo kuu la kesho na njia nzuri nyingine ni kuigawa pesa yako kwa siku utagundua unaingiza shilingi ngapi kila siku na kisha angalia matumizi yako kila siku yanaendana na pato lako la siku? Kwa kuanzia na hapo utajirekebisha kimatumizi na utaheshimu matumizi sahihi ya pesa. 

Pesa ikiwa nyingi itakupa upofu uuamini kuwa huwezi kuishiwa hivyo kila matumizi yakujiayo kichwani utayafanya na hapo ndio mwanzo wa kutumia hovyo pesa  mpaka baadaye ikipungua ndio itakutoa upofu uone kuwa kuna hatari itokanayo na ukosefu wa pesa kwa sababu pesa uliyonayo haitoshi kukufikisha msimu mwingine wa pesa kumbe kuna kuna nguvu kubwa inatakiwa uwe nayo awali ili kudhibiti hisia za pesa zisikutawale. 

Kujua unataka nini pia ni moja wapo wa ujenzi mzuri wa nidhamu ya pesa kwa sababu utajizuia dhidi ya matumizi ambayo sio ya msingi kwako na hayapo ndani ya bajeti yako kwa kipato chako na aina yako ya safari uliyonayo, kutojua nini unataka itakuingiza kwenye matumizi yasiyo sahihi kwa sababu kila utakachokiona kinavutia utahitaji kukinunua. 


Mwanasayansi Saul Kalivubha 

0652 134707

Saturday 30 April 2022

MAISHA HAYA HAPA

UNATAFUTA MAISHA? HAYA HAPA.

Kumekuwa na semi nyingi kuhusu maisha na karibia kila siku watu hutoa majibu kuwa wametingwa na harakati za kutafuta maisha  lakini swali ni je unajua unachokitafuta?  Unayajua maisha?  
Maisha ni uhai hivyo kama wewe sio mfu basi tayari una maisha kwa sababu ungekuwa huna maisha ungekuwa kaburini leo ila kwa kuwa unapumua tayari maisha unayo yafaa ushukuru Mungu kwanza kwa hilo la wewe kuwa na uhai mpaka sasa ni nafasi ya upendeleo kwako.
Unatafuta nini? Unachotafuta ni vitu ambavyo vitafanya maisha yako yaendelee kuwepo ambapo vitu hivyo vipo kwenye makundi makubwa mawili  ambayo ni vitu vya msingi kwa uhai na vitu vya zaidi ya uhai .
Vitu vya msingi kwa uhai ndivyo huitwa mahitaji ya lazima ili kuulinda uhai wako  na ukifanikiwa vitu hivyo tayari hiyo ni hatua ya awali ya mafanikio kwa sababu ukiwa na hivyo akili itaacha kuwa na msongo wa mawazo juu ya vitu hivyo na sasa itaanza kuwazia hatua ya pili ambayo ni mafanikio zaidi ya kuwa hai .
Mahitaji ya msingi kulinda uhai wako ni kama vile  Chakula, malazi na mavazi . Bila chakula huwezi kuwa na uhai kwa sababu mwili unahitaji chakula ili usipoteze uhai  , bila malazi pia unakuwa kwenye hatari kubwa ya kuupoteza uhai kwa sababu ni rahisi kushambuliwa na wanyama wakali na endapo utalala nje na hatimaye kuupoteza uhai na bila ya mavazi pia ni hatari kwa sababu ni hatari kushambuliwa na vimelea vya magonjwa na hata kupoteza kujiamini kwa sababu tu unatembea utupu ilihali wengine wamevaa. 
Unaweza kumudu Chakula?
 Unaweza kujimudu sehemu ya kuishi?
 Unaweza kujimudu mavazi?  
Kama maswali yote matatu kwako majibu ni ndiyo basi hongera sana hiyo ni hatua kubwa sana kimafanikio inayolinda uhai na kama majibu yako kwa maswali yote matatu ni hapana basi bado kwa namna moja utakuwa bado ni tegemezi na kama umri wako kisheria ushavuka utegemezi basi mapambano yaendelee kutafuta kwanza vitu hivyo vitatu ili uweze kujimudu kwanza na kisha uanze kuwazia hatua ya pili ya mafanikio. 
Hatua ya pili ya mafanikio inategemea na hiyo ya kwanza, ukishakuwa una uwezo wa kujimudu tayari  sasa hatua ya pili itakuwa kutafuta zaidi ya uhai na hiyo ndio hatua ya kuacha alama kwenye maisha yako , hatua hiyo ya pili ni kuliishi kusudi la kuumbwa kwako hivyo kama uliumbwa kuwa mchezaji wa mpira basi simamia vizuri eneo lako , kama uliumbiwa kuwa mwimbaji basi simamia vizuri eneo hilo kwa ufupi tu tuseme kuwa hatua ya pili ni kuishi ulichoumbiwa  .

Mafanikio mazuri ni muungano wa hatua zote mbili ambazo  ni uwezo wa kujimudu na uwezo wa kuishi kusudi la kuumbwa. Hatua ya kwanza ya kujimudu kwenye chakula, malazi na mavazi inahitaji ubunifu wa hali ya juu sana la sivyo utashindwa kuivuka hatua hiyo na muda wote utakuwa unapambana kwa ajili  ya mwili wako tu na sio kwa mapendeleo zaidi, unahitaji ujenge mfumo utakaofanya uwe unapata mahitaji yako bila wewe kujishughurisha moja kwa moja kwa mfano unaweza kuwa na biashara ambayo itakuwa inajiendesha ili kukupatia pesa ya chakula, malazi na mavazi  lli kipindi biashara hiyo inaendelea wewe unakuwa busy na kupambania hatua ya pili ya mafanikio. 
Karibia kila siku inatakiwa uwe unajitathmini kujiona ni hatua gani upo? na mipango ipi umeweka ili kuvuka  hatua ya kwanza.

Upo hatua gani wewe? 

#Mwanasayansi Saul Kalivubha. 
#Fikiandotozako.
+255652134707

Saturday 9 April 2022

NAMNA YA KUTIBU MAJERAHA YA KIHISIA

 TIBA YA HISIA ZILIZOJERUHIWA. 

HISIA ni msukumo ambao unahitaji kutimilizwa , mfano  mtu ukiwa na hisia za kupenda utafurahi ukipendwa, ukiwa na hisia za hasira utataka ufanye jambo fulani kuimaliza hasira n.k, sasa tunapata picha kuwa kila kwenye hisia kuna jambo litatakiwa kufanywa ili kutimiliza lengo la hisia.Tuangalie kisa  hiki ambapo najua kwa namna moja au nyingine utakuwa umewahi kuwa muhanga, mmepanga kukutana na rafiki yako mnayependana kweli   mara ghafla siku moja kabla anakutumia ujumbe kuwa hatoweza kuja tena siku hiyo kapatwa na dharura  hivyo mpaka siku nyingine kama wewe utajisikiaje? Kwa jibu la haraka utajisikia vibaya na sababu kubwa sio kuwa kakupotezea muda kama wengi wanavyodai la hasha ni kwa sababu ujio wake kwako ulikuwa ni tiba ya hisia fulani ambazo tayari zilikupanda pale tu mlipokubaliana  kukutana  tena kibaya zaidi mkiwa mna mahusiano ya kimapenzi ndio utatumia zaidi  kwa sababu kajeruhi hisia zako. 

Tumeona kuwa kila kwenye hisia kuna jambo linatakiwa hivyo lisipofanyika basi hisia zako zitakuwa zimejeruhiwa. Jeraha la kihisia ( psychological trauma)   linatofautiana ukubwa kutokana na aina ya hisia iliyojeruhiwa  mfano hasira uliyonayo dhidi ya mtu unayemdai na unataka uonane naye umwambie bayana endapo hutaonana naye utaumia lakini muda sio mrefu jeraha lake litapona utaendelea na maisha lakini hisia za kupenda ikitokea umempenda mtu  lakini mwenzako akawa msaliti na mwisho mkavunja uhusiano hilo jeraha lake  kupona sio rahisi na litakuathiri sana kama utakosa mbinu za kujitibu.

Bila shaka umewahi kuona watu wakiwa na tabia mpya punde tu baada ya kukutwa na maswaibu fulani, ulevi, wizi, uhuni , kuchelewa kuoa/kuolewa kwa kutoamini tena mahusiano  n.k, hayo ni moja ya matokeo ya kushindwa kujitibu majeraha ya hisia zilizojeruhiwa au  kujitibu kwa mbinu zisizo sahihi  kwa sababu baada ya hisia kujeruhiwa  kinachofuata  ni muhusika kutafuta tabia mpya itakayomsaidia kusahau maumivu  sasa hapo ndipo kuna tatizo  wengi huchagua tabia ambayo ndio badala ya kuwatibu ndio inawakandamiza zaidi mfano baada ya mtu kuachwa kwenye mahusiano anaamua kutokuwa tena muaminifu au kutowaamini tena watu tabia ambayo inamfanya aendelee kuteseka kwa sababu ataachwa tena kwa kukosa uaminifu. 

Hisia zinapojeruhiwa jitahidi ukubali kwanza hali  na pia katika machaguzi ya tabia mpya itayokufanya ujione sawa usichague vilevi  na wala usichague kulipiza kisasi bali chagua kujiboresha zaidi ili hata ikitokea tena basi sababu nyingi zisilalie kwako , fuata hatua hizi :

1.ikubali hali. 

2.Usianzishe tabia za kujisaulisha kwa muda  mfano kuanza ulevi n.k,bali tafuta tabia itayokuboresha zaidi 

3. Jipe muda mrefu wa kujiboresha ukiwa bora itakujengea kujiamini. 

4.Ukiridhika kuwa umejiboresha sasa unaweza kuendelea na maisha mengine na ukiweza epuka vichocheo vitavyokufanya ukumbuke namna ulivyojeruhiwa kihisia.

Saul Kalivubha ,Mwanasayansi tiba  

            +255652 134707


Saturday 26 March 2022

MUMBO MUHIMU KABLA YA KUCHUKUA MKOPO

MAMBO MUHIMU YA KUJIULIZA KABLA YA KUCHUKUA MKOPO 

Mikopo ni mkombozi kwa watu wa tabaka zote  wenye kipato kidogo na matajiri pia hivyo sio kitu kibaya bali ni sehemu ya kujikomboa kiuchumi, mikopo hutolewa na taasisi nyingi za kifedha na hata zisizo za kifedha kuna mashirika na makampuni nayo hutoa mikopo vilevile, lakini mikopo yote hiyo huwa na masharti na sharti kubwa ni riba pamoja na ukomo wa muda wa kulipa huo mkopo na kabla ya mteja kukopeshwa lazima ukidhi vigezo ikiwemo pamoja na mteja kukubaliana na masharti kwa kutia saini fomu ya maridhiano hayo .

Makazini kuna kila aina ya watu katika suala la mafanikio na maamuzi pia, kuna ambao tayari wanahatua fulani katika maendeleo na kuna ambao bado kwanza wanaanza nikimaanisha waajiriwa wapya na wengine sio waajiriwa wapya bali kipato chao sio kikubwa kiasi cha kufanya mambo makubwa ya kifedha hivyo na hapo ndipo suala la kujilinganisha na waliowatungulia kunaanza lakini kosa huja pale ambapo hamasa ya kufanya vitu vikubwa ndani ya muda mfupi inamuandama mfanyakazi na bila kufikiria mara ya pili anaamua kuchukua mkopo ulio nje ya uwezo wake. 

Mfanyakazi kabla hujachukua mkopo kwanza hakikisha una ufahamu wako timamu na umejihakikishia kuwa masharti ya mkopo husika na muda husika wa ukomo wa mkopo wako umejiridhisha kuwa hakuna madhara makubwa utapata bali faida kubwa hapo sasa waweza chukua mikopo huo na isiwe una shauku ya kutaka mafanikio makubwa au ukawa umejilinganisha na wafanyakazi wenzako ukajiona uko nyuma kimafanikio sasa unataka uchukue mkopo ili ukimbizane nao kwa sababu hizo ikiwa ndio unazo basi hustahili kuchukua huo mkopo acha kabisa. 

Kabla ya kuchukua mkopo utambue kuwa kuna makato mengine yanafanyika kwenya mshahara wako wa msingi hivyo mkopo utakuja kuongeza asilimia ya makato yako kama ilikuwa unakatwa asilimia kumi sasa itakuwa pengine asilimia ishirini  hivyo utaweza kuishi kwa mshahara wa asilimia themanini mpaka hapo utakapomaliza kukatwa na wadeni wako? 

Jambo lingine muhimu la kuzingatia ni kuwa huo mkopo unachukua kwa ajili ya kutimizia jambo fulani sasa ikiwa ungeweka akiba ungefikisha kiasi sawa na mkopo unaotoka kuuchukua kwa miaka hiyo ambayo utamaliza kuulipa? ikiwa ndio basi tambua huo mkopo uko ndani ya uwezo wako na ikiwa huoni ikiwa hivyo jitafakari upya kabla ya kuingia huo mkataba wa mkopo. 

Kutokana na majukumu kuongezeka kila siku na kipato kuwa kilekile sio vibaya kufikiria mikopo kama suluhisho la kutatua uhuru wako kiuchumi hilo ni wazo zuri lakini isiwe ni kwa mihemko ukifanya kwa mihemko utajikuta kwenye matatizo na majuto ya kuulipa huo mkopo na pengine ukaingiwa na msongo wa mawazo hadi mwishowe ukaamua kujikatisha uhai wako wa thamani na wakati ikiwa ungekaa vizuri na akili yako ungepata maamuzi sahihi kabla ya kuuchukua huo mkopo.

Ikiwa ni mkopo unahitaji kwa ajili ya biashara basi jitahidi uwe na uhakika na wazo lako la biashara  kwa kufanya utafiti wa kutosha kujiridhisha kabla ya uanzishaji huo  na ikiwezekana usitumie pesa yote ya mkopo kwenye biashara bali anza kwa kiasi fulani kisha uende unaongeza mtaji taratibu kwa sababu mara nyingi biashara ikiwa unaanza huwa ni za majaribio chako zitakuwa nyingi sana na inaweza kufa na kuanza tena upya hivyo lazima ujihami katika hilo pia


Mwanasayansi Saul Kalivubha 


+255652 134707

Saturday 19 March 2022

ELIMU YA KUJIAJIRI KWA WANAFUNZI

 ELIMU YA  KUJIAJIRI IFUNDISHWE MASHULENI 

Katika karne hii ya 21 suala la  mtu kumaliza shule na kukosa ajira sasa sio geni tena kwa sababu ongezeko la wakosa ajira limekuwa kubwa sana na  sababu inaweza isiwe moja tu  serikali kushindwa kuajiri wasomi wake wote  bali hata mfumo wa maisha wa sasa umebadilika mbali na kuwa wimbi la wasomi linaongezeka kila siku lakini pia  ajira za watu sasa zinachukuliwa na mapinduzi ya kiteknolojia  mfano zamani ilitakiwa watu waajiriwe kukata tiketi lakini sasa tiketi zinakatwa na mashine hivyo anatakiwa mtu mmoja tu kuisimamia hiyo mashine. 

Baadhi ya viongozi hasa wana siasa wamekuwa wakihimiza suala la wahitimu wa vyuo vikuu kujiajiri  pindi wamalizapo masomo yao na wasitegemee kuajiriwa na serikali na mwisho wa siku kosa inaonekana ni la uvivu wa muhitimu kushindwa kujiajiri  lakini ki uhalisia sio kweli kwa sababu ni rahisi kumwambia mtu ajiajiri lakini kwa muhitimu wa chuo kikuu sio rahisi kwake kwa sababu zaidi ya miaka kumi darasani anaandaliwa kuajiriwa wafikiri siku moja tu itambadili mtizamo aliojengewa kwa miaka kumi? Serikali iweke mfumo wa mwanafunzi tokea shule ya msingi mpaka chuo kikuu hapo mazingira angalau yatakuwa rafiki kujiajiri kwa sababu msingi utakuwa umemjenga, kwa mfano mtu kamaliza taaluma yake ya ualimu kaandaliwa kufundisha sasa akimaliza ajiajiri vipi? afungue kituo cha kufundisha masomo kwa  ziada ( tuition) napo nado ni changamoto kwa sababu sasa serikali inahimiza wanafunzi wamakinike zaidi na darasani na sio kwenye  vituo vya kufundisha masomo kwa ziada hivyo inakuwa ngumu kutumia taaluma kujiajiri na kujiajiri kwenye mambo mengine nje ya taaluma ndio hayo ambayo mwanafunzi hakupewa misingi tokea mapema. 

Serikali kupitia mitaala ya elimu iweke masomo ya kufundisha maisha nje ya taaluma kwa nadharia na vitendo  kwa mfano kuwepo na somo la maisha na kujitegemea ambapo hapo mwanafunzi afundishwe stadi mbali mbali za kuyakabili mazingira tofauti na ile taaluma yake kwa mfano kama ni mwalimu afundishe ni namna gani anaweza kuyakabili mazingira bila kuwa na ajira hivyo apewe stadi hizo kama mbinu za kuanzisha biashara ndogo ndogo na namna ya kuikuza biashara hiyo na mwisho wa siku apewe mtihani wa vitendo kwa kuendesha mradi wa shule au kuleta ubunifu wa mradi hii itasaidia sana kumfanya mwanafunzi azoee mazingira mapema. 

Wanafunzi wengi bado wanaamini kujiajiri ni umaskini ndio maana  wengi wao hilo wazo la kujiajiri hata hawalifikirii na sio makosa yao kuwaza hivyo ni kwa sababu darasani hawakuambiwa ukweli kuwa kuna kukosa ajira na kuishi maisha nje ya ajira ndio maana kila muhitimu kilio chake ni kupata ajira, kuna uwezekano mkubwa wahitimu wakipewa hata mitaji wengi watashindwa kujitegemea kibiashara kwa sababu elimu ya kujitegemea haikufundishwa darasani  ni tofauti na mtu ambaye hakuendelea na masomo tayari akili yake aliiandaa kuwa hakuna namna anaweza kuishi bila kujiajiri mwenyewe hivyo anamakinika zaidi na mwisho wa siku anakuwa na elimu nzuri ya kujitegemea. 


Serikali iweke ukweli kwa wanafunzi mapema kuwa kuajiriwa sasa ni bahati ya wachache na tena kwa baadhi ya kada na iziweke wazi kada hizo na kwa kada zile ambazo ajira zake hazitoki sana basi zipunguziwe udahili vyuoni wachukuliwe wachache ili kuepusha mlindikano wa wahitimu wasio na ajira mtaani. Suala la kujiajiri kwa sasa inatikiwa iwe ni kama kampeni kwa wanafunzi kwa sababu hali ya wahitimu sio rafiki sana mtaani bado kuna umuhimu wa serikali kuingilia kati kwa kubadili mitaala ya elimu 


Mwanasayansi Saul Kalivubha 

+255652 134707

Sunday 13 March 2022

MBINU ZA KUWEKA AKIBA

 JINSI YA KUWEKA AKIBA 

Elimu ya pesa kila siku inakuwa changamoto mpya kwa watu wengi ndio maana  bado kuna watu wanaingiza pesa ya kutosha lakini matumizi yao sio rafiki kiasi cha kuwafanya wabaki na ziada ya pesa . Inawezekana hata wewe ukawa kwenye kundi hilo la watu ambao wanaweka malengo ya kujikomboa kiuchumi kila siku lakini utekekelezaji wake ni mdogo au haupo kabisa, ukijiona wa hali hiyo basi tambua una changamoto katika namna nzima ya kuitawala pesa  na njia rahisi kwa watu  hali zote za vipato ni uwekaji wa akiba na mipango madhubuti ya namna ya kuizalisha hiyo akiba ili nayo ilete faida. 

Akiba kwa tafasiri isiyo rasmi ni namna mtu anavyoijali kesho yake ndio maana leo unajinyima ili kesho ufanikiwe katika jambo fulani , mfano  unaingiza shilingi elfu kumi kila mwezi na unataka baada ya mwaka uwe na mtaji wa laki mbili hapo lengo ni wewe upate mtaji wa laki mbili lakini mfukoni una shilingi elfu kumi ambayo kila mwezi utaipata, kwa kawaida unaweza kuiona ndogo lakini  kuna uwekano mkubwa mtu asiifikishe kwa mwaka .

Kuna elimu nyingi kuhusu uwekaji wa akiba ambazo hutolewa kila leo na pengine ukawa moja kati ya watu ambao tayari wamewahi kuzitumia njia hizo lakini bila mafanikio yoyote, unafikiri tatizo ni nini?  Kuna kitu muhimu kutambua kabla ya kuanza zoezi la kuweka akiba ya pesa nacho ni wazo kuu la kesho, jiulize kesho unataka ufanye nini?  na ili ufanikiwe jambo hilo wahitaji kiasi gani cha fedha?  Ukifahamu kiasi cha fedha unachohitaji ili kufikia lengo hilo utatakiwa kujua kwa sasa wewe unapata kiasi gani cha fedha? iwe ni kwa mwezi au kwa kila siku muhimu uwe na uhakika na kiasi hicho cha fedha. 

Ukijua unaingia shilingi ngapi labda kwa mwezi sasa utatakiwa ujue pia matumizi yako kwa mwezi yakoje? Yanagharimu kiasi kipi cha fedha?  Na je matumizi yako kwa siku mpaka mwezi yanakuruhusu uweze kuyafikia malengo yako? Ukiwa na majibu ya maswali hayo ndipo utaangalia sasa kipi kinawezekana kupuguzwa ili matumizi yako kwa mwezi yapungue. 

Hatua ya pili ni kuorodhesha matumizi yako katika safu mbili , moja iwe ya matumizi ya lazima mfano chakula  n.k na ya pili iwe ni ya matumizi yasiyo ya lazima kisha  tafuta uwezekano wa kupunguza matumizi yasiyo ya lazima ili pesa ambayo ilikuwa inatumika kwenye matumizi hayo  iingie kwenye akiba na pia uanze kujinyima kimatumizi  ili upate pesa ya ziada .

Hatua ya tatu ni kujiwekea mikakati ya kujikumbusha malengo yako kwa mfano unaweza kuwa na utaratibu wa kila siku jioni unapitia daftari lako la malengo ili uwe na shauku ya kuendelea na mapambano bila kuchoka. Unatakiwa Kuheshimu mikakati yako kwa kuwa na nidhamu katika  kuweka akiba ili uweze kufikia malengo yako. 

Hatua ya mwisho ni kuhakikisha pale upatapo pesa  unatoa kwanza kiasi ambacho umeridhia kukiweka kabla ya matumizi mengine yoyote  usifanye makosa kwa kuanza kutumia pesa kwanza kisha ndio ubakize akiba , fanya zoezi hilo kwa nidhamu yote na lifanye kwa kuongozwa  na malengo ya kesho.

Makala hii imeandikwa na Mwanasayansi Saul Kalivubha 

+255652 134707 

Friday 18 February 2022

MBINU ZA KUISHI NA WATU WENYE TABIA NGUMU

MBINU ZA KUISHI NA WATU WENYE TABIA NGUMU MAKAZINI. 

Kama sio wewe basi utakuwa umewahi kutana na mtu akilalamika dhidi ya watu ambao wana tabia zisizo rafiki na pengine mpaka mtu huyo anatamani kuachana na kazi hiyo ili aepuke kukutana na watu hao , ni kweli wapo watu wana tabia ambazo ni ngumu kuvumilikika kiasi kiasi cha kufanya wengine wakose amani pindi wakiwa na watu watu hao wenye tabia zisizo rafiki. 

Pengine hata wewe kuna mtu ana tabia ambazo zimekufanya ujiulize swali hili " hivi huyu mtu anaishije na familia yake kwa tabia hizi?" Maana kama yuko hivyo kazini inakuwaje nyumbani kwa ndugu zake ambao wengine analala nao kitanda kimoja  na kula nao meza moja si pengine ikawa kila siku makwazo kwenye nyumba hiyo ? Lakini ukweli ni kuwa hakuna makwazo kabisa anaishi na familia yake vizuri tu kwa sababu  walipomfahamu walijifunza kuishi naye kwa kumzoea alivyo  changamoto ipo kwako ambaye hujazaliwa naye bado hujajifunza kuishi naye na pengine hutaki kujifunza kuishi naye. 

Hakuna namna utaishi bila kukutana na watu wenye tabia zote nzuri na mbaya ili uepuke hilo basi kajifungie kisiwani peke yako lakini tofauti na hivyo lazima utakutana na watu wenye tabia zote nzuri na mbaya sasa itategemea na watu hao umekutana nao wapi na wana nafasi gani kwako  kama ni kazini na ofisi moja je utaacha kazi kwa sababu ya watu hao?  Au utakuwa unakaa nje ya ofisi kuwakwepa watu hao ? Haiwezekani hilo na sio suluhisho lake lazima ujifunze kuishi nao watu hao. 

Jitahidi ujue mnapishana sana kwenye kipi kwa sababu sio kweli kwamba mtapishana kwenye kila kitu lazima tu kuna sehemu moja  ndio huwa chanzo cha kupishana naye na ukilitambua  eneo hilo basi tenga siku moja tafuta eneo tulivu jitafakari ni kwa nini mtapishana? na kwa nini eneo hilo? Anza kutengeneza mbinu za kuishi naye mtu huyo kwenye eneo hilo na moja wapo ya mbinu nzuri ni kutojibana naye sana kwenye eneo hilo jifunze kupuuzia baadhi ya kauli zake , pengine uone ugumu kukaa kimya pindi anapoongea kama tabia yake ilivyo lakini baadaye utazoea tu na itakuwa akiongea mambo yake unajibu machache mengine unamsikiliza. 

Mbinu nyingine ni kumpuuza kwenye baadhi ya mambo yake lakini usimuonyeshe kuwa unampuuza bali usifanyie kazi kila tukio lake kwako kwa mfano mmekutana kazini umemsalimia hajaitika au yeye hakusalimii  hilo lisikupe msongo wa mawazo kwa kujiuliza kwa nini haitikii salamu zako bali mpuuzie tu kwa sababu ndivyo alivyo na usiache kutabasamu pindi ukikutana naye na wala usilipe kisasi kwa anayokufanyia  na hapo itakuwa mwanzo wa wewe kuishi naye mtu huyo. 

Mbinu nyingine ya tatu ni kujitahidi unaepuka mazingira ya kukaa na mtu huyo muda mrefu ila isipokuwa pale tu inapobidi kwa sababu za kikazi tofauti na hivyo muepuke mtu huyo kwa kujishugulisha na mambo yako mengine. 

Mbinu nyingine ni usiitizame tabia yake kama kikwazo kwako bali muone kama ndivyo aliumbwa hivyo na ukiliweza hili basi usiwe unamuongelea jinsi alivyo mbele ya wengine bali muombee kubadilika kwa sababu tabia yake sio kwamba unaiyona wewe tu bali kuna wengine pia wanaiyona hivyo tabia yake inakuwa kikwazo kwake sio kikwazo kwako wewe kazi yako ni moja tu kujifunza kuishi naye 

Makala hii imeandikwa na Mwanasayansi Saul Kalivubha


+255652134707

Tuesday 1 February 2022

ELIMU YA PESA

 USISUBIRI PESA IPUNGUE NDIO UWEKE NIDHAMU YA MATUMIZI

Matumizi ya pesa bado ni changamoto kwa watu wengi na matokeo yake ni hujikuta katika ukosefu wa pesa mara kwa mara na hii sio kwa waajiwa tu hata waliojiajiri kwenye mambo binafsi  bado hujikuta kwenye kipindi kigumu cha ukosefu wa pesa sio kwa sababu haikuwepo la hasha ni kwa sababu ilikuwepo lakini ikatumiwa bila kuzingatia matumizi sahihi kutokana na kipato. Ukipata muda tulivu ukajitafakari utagundua kuwa pindi upatapo pesa matumizi yako yanakuwa juu na hupungua kadri pesa inavyopungua yaani kwa lugha rahisi  ni kuwa nidhamu yako ya matumizi ya pesa inaongezeka kadri unavyoishiwa pesa. 

Pesa ni nguvu ya kihisia ambapo usipoitawala itakutawala yenyewe kwa kukupa maamuzi mengi na hapo utakosa utulivu hali ambayo itafanya upoteze nidhamu ya matumizi ndio maana mshahara ukiingia unaweza jikuta unafanya manunuzi bila kuangalia ukubwa wa gharama kwa sababu unajua pesa ipo lakini ukianza kusikia mfuko umepwaya ndio utarudisha makini wa matumizi kwa mfano mwanzo ulilipwa laki tano na ilipofikia mfukoni umebaki na laki moja ndio utaanza kuipogia mahesabu hiyo laki moja kuangalia kama itakufikisha mwezi mwingine, je kwa nini hukufikiria hivyo tangu ukiwa na laki tano? 

Nidhamu ya pesa ni kuheshimu pato lako kwanza na pili ni kuheshimu matumizi sahihi yaliyo ndani ya kipato chako kama ulipanga kununua kitu cha shilingi mia ndio itakuwa sawa kulingana na kipato chako basi fanya hivyo lakini ulinunua kwa shilingi Mia mbili ujue umekula na pesa ya siku fulani hivyo jiandaye siku hiyo kukosa pesa la sivyo iwe ni dharura ndio tumia lakini kama si dharura yatakiwa ujidhibiti dhidi ya matumizi ya pesa pale tu unapoipata, changamoto ya pesa ni kuwa ukitumia pesa ndogo unaona kawaida tu lakini mwisho wa siku ukijumlisha unakuta kama ungehifadhi ungekuwa mbali sana kifedha hivyo nidhamu ukianza na kuheshimu matumizi yako yaliyo ndani ya kipato chako utakuwa kwenye kiwango kizuri cha kuweka akiba. 

Nidhamu binafsi katika matumizi ya pesa inajengwa na lengo kuu ulilonalo la kesho hapo ndio utakuwa unatumia pesa ukikumbuka kesho hivyo utakuwa ukijikumbusha kila kabla ya matumizi ambayo si salama kulingana na kipato chako na utakuwa na nidhamu muda wote, lazima uwe na nidhamu au ukose nidhamu lakini ukubali kupoteza lengo kuu la kesho na njia nzuri nyingine ni kuigawa pesa yako kwa siku utagundua unaingiza shilingi ngapi kila siku na kisha angalia matumizi yako kila siku yanaendana na pato lako la siku? Kwa kuanzia na hapo utajirekebisha kimatumizi na utaheshimu matumizi sahihi ya pesa. 

Pesa ikiwa nyingi itakupa upofu uuamini kuwa huwezi kuishiwa hivyo kila matumizi yakujiayo kichwani utayafanya na hapo ndio mwanzo wa kutumia hovyo pesa  mpaka baadaye ikipungua ndio itakutoa upofu uone kuwa kuna hatari itokanayo na ukosefu wa pesa kwa sababu pesa uliyonayo haitoshi kukufikisha msimu mwingine wa pesa kumbe kuna kuna nguvu kubwa inatakiwa uwe nayo awali ili kudhibiti hisia za pesa zisikutawale. 

Kujua unataka nini pia ni moja wapo wa ujenzi mzuri wa nidhamu ya pesa kwa sababu utajizuia dhidi ya matumizi ambayo sio ya msingi kwako na hayapo ndani ya bajeti yako kwa kipato chako na aina yako ya safari uliyonayo, kutojua nini unataka itakuingiza kwenye matumizi yasiyo sahihi kwa sababu kila utakachokiona kinavutia utahitaji kukinunua. 


Mwanasayansi Saul Kalivubha 

0652 134707