Wednesday 28 July 2021

WAFAHAMU WATU HAWA WAWILI HATARI KWENYE MAISHA YAKO

 WAFAHAMU WATU HAWA WAWILI HATARI KWENYE MAISHA YAKO. 

Urafiki ni hisia zisizo epukika ndio maana sio rahisi kuishi peke yako hata uwe na tabia gani mbaya lazima umpate rafiki ambaye mtakuwa nnaweza kupikika chungu kimoja na hiyo ndio maana halisi ya urafiki ni hisia, lakini kwenye eneo hilohilo ndipo kuna vilio vingi sana vya watu kuumizwa , je nawe umewahi kuumizwa? 

Katika maisha ya urafiki kuna makundi makubwa matatu ya watu ambao watakuja kwako ambayo ni WAPITAJI, WAKAAJI na WAFANYA MAJARIBIO sasa ukiweza kufahamu elimu hii vizuri kuna uwezekano mkubwa ukawa hupati shida sana kwenye kutibu majeraha yako yatokanayo  na maumivu ya urafiki. 

 WAPITAJI: Hili ni kundi ambalo ni kubwa sana yaani namaanisha utakutana na wapitaji wengi sana kwenye maisha yako na kuitwa wapitaji haimaanishi kuwa sio watu wazuri kwenye maisha yote la hasha ni watu wazuri tena sana lakini kosa lipo kwako unapolazmisha wapitaji wawe marafiki wa kudumu kwako. 

Wapitaji ni watu wazuri ikiwa utakubaliana na kanuni ya asili kuwa muda wake ukifika wa kuondoka utamwacha aondoke na kwa nini aondoke? Ni kwa sababu kusudi lililomleta kwako limeisha kwa mfano ikiwa kuna mtu alikuja kwako ili tu mshirikiane kimasomo basi mkimaliza shule kuna uwezekano mkubwa urafiki ukapungua na kabla hujambadilishia nafasi nyingine kaa chini jitafakari uone ni kweli atakuwa bora tena hata kwenye nafasi nyingine utakayompa? La sivyo muache aende tu usilazimishe abaki. 

WAFANYA MAJARIBIO; Hawa ni watu ambao wapo kwenye makuzi ya kujifunza na mara nyingi hutokea sana kwenye urafiki wa kimapenzi ndio kuna watu watakuja kwako kwa minajiri ya mahusiano lakini sio kwa sababu wana lengo kuu na wewe la kesho ( future) bali ni kwa sababu ndio kwanza mahusiano kwao imekuwa starehe ya kwanza hivyo wanataka tu mcheze michezo ya kimahusiano, watu hawa mara nyingi utawagundua kwenye namna wanavyosuasua kwenye kuwa na subira na kuipanga kesho yake ikiwa pamoja nawe kwa lugha rahisi ni watu ambao wanahitaji mahusiano ya kutimiza hisia za mwili tu na sio mengineyo.

Makala hiii imeandikwa na Mwanasayansi Saul Kalivubha 

0652134707