Wednesday 27 September 2017

KWA NINI HUPIGI HATUA?

Karibu tena kwenye blog hii  inayotoa elimu ya maisha na  jinsi ya kufikia ndoto zetu,nashukuru Mungu kwa afya yangu ,ni matumaini yangu kuwa na wewe nimzima wa afya(sababu unapumua)..karibu tujifunze............

KUSUDI LA SOMO.
Lengo la somo letu hili ni kujifunza sababu ambazo zinazuia hatua za watu wengi,mimi pia ni moja ya wahanga wa sababu hizo,kwa muda mrefu nilikuwa nina mawazo makubwa ila sipigi hatua,na mwisho wa siku nayapoteza mawazo yale.....kwa nini hupigi hatua?


Kupiga hatua ni hali ya kutoka sehemu moja kwenda nyingine,kutoka sehemu yenye viwango vidogo,kwenda kwenye sehemu  sehemu yemye viwango vikubwa zaidi,inaaweza kuwa kwenye biashara ,shule,urafiki ,uwekezaji n.k( jifunze elimu ya pesa)......Kuna watu wana mawazo mazuri,juhudi na wanajitahidi kujifunza kila siku ,ila bado hawapigi hatua mbele,bado matokeo wapatayo hayaendani na jinsi wanavyojituma........Tujifunze kupitia baadhi ya vikwazo vinavyozuia kupiga hatua kwetu.

 SABABU ZINAZO FANYA USIPIGE HATUA.

  •  Kuwa na imani kwamba kuna watu wanahitajika kukusaidia ili ufikie hatua flani,hii ni imani ambayo inasababisha watu wemgi wasipige hatua mbele kwa kusubiri aina flani ya watu waje watoe msaada,kwa lugha ya haraka tunasema connection au channels....sawa mafanikio yanahitaji watu,ila hata wewe unaweza kuwa channel kwa watu wengine kwa kujaribu kwako.Bahati ina nguvu kwa mtu mwenye juhudi,....jaribu hadi kwenye sehemu inayohitaji mtu wa kukusaidia,ili akitokea akute upo vizuri ki maandalizi

  • Usiogope makosa,....hapa ndipo kuna watu wenye mawazo mazuri sana na elimu ya kutosha kuhusu jambo flani,ila hawapigi hatua,..kwa nini? Watu wenye ujuzi mwingi mara nyingi hawtaki kuonekana wakikosea,bora waendelee kuwa na ujuzi wao kwenye fikra kuliko kujaribu kwa vitendo,hali hii ndio inafanya mara nyingi walimu kushindwa na wanafunzi wao...Hata uwe na elimu ya viwango vya juu kuhusu jambo flani,bila kuihamisha kwenye vitendo ni sawa na kazi bure,kubali kukosea ili upige hatua mbele kwa kufanya sahihi ,

  • Fanya maamuzi ,hata kama matokeo yake yanaumiza au yanapingwa na rafiki zako wa karibu,kuna watu tayari wanatambua ili kupiga hatua lazima wafanye jambo flani,ila kwa sababu tu jambo hilo linapingwa na marafiki ,wanaamua kuvumilia tu ili kuendeleza mahusiano mazuri ,Maisha ni ya kwako,rafiki wataokukimbia kwa maamuzi yako ya mafanikio ,achana nao,ukifanikwa watatafuta njia ya kutudi tena kwako

  • ,
  • Mafanikio ni haki ya kila mtu,hakuna aliyepangiwa viwango flani,hata wewe unawezakufika,ondo ile imani ya kwamba biashara flani inafanywa na watu flani tu,au ufaulu flani una watu wa aina flani tu,hata wewe umo kwenye watu hao ,,,,hivyo usiache malemgo flani kwa kuwa hakuna mtu wa familia yenu amewahi kufanya hivyo,,,,,,hutopiga hatua'

Makala hii imeandikwa na Saul kalivubha,kwa label ya fikia ndoto zako

Friday 15 September 2017

SAIKOLOJIA YA PESA.

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya maisha ,nashukuru Mungu kwa kunipigania kwake kila siku, furaha yangu kubwa ni sababu  na wewe ni mzima.,kama ni mgonjwa pia ondoa hofu,yupo mponyaji mkuu kwa  ajili yako ambaye ni Mungu.

KUSUDI LA SOMO.
Leo nataka tujifunze saikolojia ya pesa katika sehemu kuu tatu ;BAJETI,AKIBA NA UWEKEZAJI....Kabla ya kuanza somo letu hili ni vizuri ukaelewa kwanza  maana ya Saikolojia kwa ufupi.
SAIKOLOJIA sio neno geni sana,ila kwa ufupi lina maana ya elimu ya tabia ,sababu zinazofanya utokeaji wa tabia na madhara ya tabia......kwa leo tujifunze tabia ambazo pesa inahitaji ili iweze kukaa mikononi kwako.......karibu tujifunze.



 BAJETI.
Bajeti ni muongozo ambao unahusisha mapato na matumizi ya pesa,ni watu wachache sana ambao wanatumia pesa kwa kufata bajeti,maana rahisi ni kwamba watu wengi hawana malemgo kwenye maisha yao ya kesho,haijalishi kipato chako ni cha ukubwa gani,lazima utengeneze bajeti ya kuonyesha pesa unayoingiza,matumizi unayotumia na akiba unayoweka.......Mambo muhimu sana ya kuzingatia kabla ya kupanga bajeti ni haya; Ukubwa wa pesa unayoingiza,  malengo yako yanayohitaji pesa ,  mazimgira yako(familia yako) na ufahamu matumizi ya lazima na yale yasiyo ya lazima....Mambo hayo machache yatakusaidia uishi maisha yanayo endana na bajeti yako ila yenye mchango mkubwa kwenye malengo yako ya kesho.



AKIBA.
Akiba ni pesa ambayo unahifdhi kabla ya kuanza matumizi yoyote ya pesa na kwa lengo maalumu,lazima uwe na malengo kisha ndio uanze kuweka akiba,Ukiona unashindwa kuweka akiba jitahidi upitie bajeti yako vizuri na kisha uanze kupunguza matumizi yasiyo ya lazima au kununua  vitu vyenye bei ya kawaida .....kiufupi lazima uishi maisha ya kawaida kwa sasa ili kesho uishi maisha ya tofauti,.....Kuna watu wanajidanganya kwmba kuweka akiba lazima uwe na kpato kikubwa,jibu ni hapana.....nakumbuka kuna kipindi nilikuwa naingiza laki moja kwa mwezi ila nilifanikiwa kupanga bajeti hadi kuweka akiba ya laki sita kwa mwaka,hivyo nikawa na jeuri ya kufanya kitu bora zaidiya kile cha kuingiza laki moja kwa mwezi.



UWEKEZAJI.
Ukiwa na bajeti nzuri utakuwa na uwezo wa kuweka akiba,usiweke akiba kama huna kitu cha kufanya kesho,utaitumia pesa yako ovyo,weka akiba kwa lengo flani,ili ile akiba ianze kukuzalishia pesa,......njia nzuri ya kutumia akiba ni kuwekeza au kufanyia biashara.....kwa hiyo ni vizuri kuwa na elimu ya pesa,elimu ya kile unachotaka kuwekeza na ukubali kuishi maisha ya kawida kwa muda flani.


            See you at the top
               Saul kalivubha
                  0652 134707