Wednesday 26 April 2017

KUANGUKA KWA MTU ALIYEFANIKIWA

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya maisha, ni imani yangu kuwa  Mungu anaendelea kukupigania. ...karibu tujifunze.

 KUSUDI LA SOMO. 
Leo nataka tujifunze somo la kuanguka kwa mtu aliyefanikiwa, unaweza kuhisi tofauti kidogo kwa kuona somo hili kwenye blog hii. ..ila ni hali ambayo wewe pia unaweza kuwa shahidi kwa kuona baadhi ya watu wakipoteza mafanikio yao makubwa....kwa hiyo nataka tuangalie baadhi ya sababu zinazofanya watu wapoteze mafanikio yao, kwa kujua sababu hizo itakuwa msaada kwetu kulinda mafanikio yetu. 
Zipo sababu nyingi ila leo nataka tuangalie sababu kuu tatu......karibu. 

SABABU ZA KUANGUKA KWA MTU ALIYEFANIKIWA.
1.Marafiki wapya;siku zote mtu aliyefanikiwa huwa anakuwa
 tofauti na wengine, mafanikio yake yanavuta watu wengi kuwa karibu yake, watu hao ni pamoja na wale ambao waliona kuwa hawezi kipindi alipoanza safari ya mafanikio. .....hiki ni kipindi kigumu sana kwa mtu aliyefanikiwa, ni kipindi kigumu kwake kwa sababu ya ugumu wa kutambua nani rafiki wa kweli kwake, ....  mafanikio yake hupotea pale atapoanza kushirikiana na rafiki wanaoshangalia mafanikio yake na kusahau rafiki waliomfaraji kwenye shida. ..siku zote rafiki anayeshagalia mafanikio yako huwa sio rafiki mzuri, maana kufata mafanikio yako na sio uhalisia wako
2.Kulewa sifa;  sifa ni sehemu ya lazima kwamafanikio yako. .tatizo sio kusifiwa, tatizo ni kuzitawala hisia za furaha itokanayo na sifa. ....Wanasikolojia tunaamini kuwa tabia nyingi zitokanazo na sifa huwa ni za uharibifu na majivuno. ..mtu aliyefanikiwa akianza kuziishi tabia zitokanazo na kusifiwa anakuwa kwenye wakati mgumu sana wa kusahau alipotoka na kubadili njia ya kumpeleka aendapo. ...hatari yake ni kupoteza mafanikio yake. 

3.Kukosa maandalizi kabla; Kuna watu wanafanikiwa bila kujiandaa kuyaishi maisha ya mafanikio, ..maisha ya mafanikio yana changamoto zake,  mtu aliyefanikiwa kuipitia. .lazima watu wasifie tena kubwa sana. ..ni muhimu mtu ukafahamu wapi unaelekea, na nini utakibeba, kutambua hilo itakusaidia kuwa makini na mambo ambayo yapo nje ya kuendeza mafanikio yako. ..kinyume chake ni kupoteza mafanikio.

Kufikia ndoto zako sio kushinda, ushindi ni kuendeza mafanikio yako. ..
Tukutane wiki ijayo. 
                       
                  See you at the top. 
                  scientist Saul kalivubha. 
                    0652 134707. 
      

Friday 21 April 2017

SIRI ZA UVUMILIVU -3

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya maisha, ...nashukuru Mungu kwa uzima wangu na wako pia. Karibu kwenye sehemu hii ya tatu na mwisho wa somo letu la siri za uvumilivu....karibu tuendelee.

KUSUDI LA SOMO.
 lengo la somo letu hili ni kujifunza siri zilizopo kwenye uvumilivu, na somo letu lina sehemu tatu. 1.maana ya uvumilivu. 2. faida za uvumilivu. 3.hasara za kukosa uvumilivu. ..Leo nataka tujifunze hasara zipi zinaweza kutokana na ukosefu wa uvumilivu. ...Kabla ya kuendelea ingia Google search na kuandika kalivubha blog siri za uvumilivu. ..hiyo itakusaidia kuendana na sehemu hii ya mwisho.

3.HASARA ZA KUKOSA UVUMILIVU .

Mambo karibia yote yenye matokeo mazuri yanahitaji uvumilivu ili kuweza kufanikiwa kupata matokeo hayo mazuri. .....nataka tujifunze hasara za uvumilivu kwenye sehemu hizi tatu. .mahusiano ,biashara na mafanikio kwa ujumla. .....karibu tuendelee. 

MAHUSIANO; Rafiki yangu mmoja aliwahi kuniambia kuwa anahisi kuwa anabahati mbaya, kwani huwa hadumu kwenye mahusiano. ..utafiti unadhibitisha kuwa watu wengi wameacha watu sahihi sababu tu ya kukosa uvumilivu, ..Mahusiano yana changamoto zake, na hii hutokana na mahusiano kuhusisha watu wenye asili tofauti....kumbe kuna mazingira yatahitaji uvumilivu dhidi ya madhaifu, uvumilivu dhidi ya mabadiliko ya hisia ambayo yanaweza kuwa chanzo cha maamuzi mabovu.

BIASHARA. Kosa ambalo wengi tunalifanya kwenye biashara ni kutengeneza imani ya kupata mafanikio ya haraka. ...Hili ni kosa kwa sababu biashara karibu zote zinahitaji muda wa kutosha ili kutoa faida kamili, huo muda wa kutosha unahitaji mtu mvumilivu, ...pia kwenye biashara kuna hasara, na mara nyingine kuna kuanza upya, yote hayo yanahitaji uvumilivu wa kutosha. .ukikosa uvumilivu ni ngumu kufanikiwa katika biashara...

MAFANIKIO KWA UJUMLA; kufanikiwa kwa ujumla ni kuwa kwenye hatua ambayo ni matokeo ya kushinda maumivu ya UVUMILIVU. ...Msanii wa filamu maarufu kwa jina la Sylivester Stalone Rambo aliwahi kusema alijaribu zaidi ya mara 70 na kushindwa mara zote, ila kilicho msaidia ni uvumilivu wake, hadi sasa ni muigizaji maarufu dunianI. inahitaji uvumilivu wa hali ya juu katika safari yetu ya KUFIKIA NDOTO ZETU. ...Ukikosa uvumilivu ni ngumu kufanikiwa kwa jambo lolote lile. ....jiulize ni maamuzi gani uliyafanya kwa kukosa uvumilivu? 
 Karibu wiki ijayo.

            See you at the top. 
scientist Saul kalivubha 
                0652 134707.
             

       

Wednesday 12 April 2017

SIRI ZA UVUMILIVU -2

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya maisha, ni imani yangu kuwa Mungu katimiza mapenzi yake kwetu sote. ......

KUSUDI LA SOMO
.
Lengo la somo letu la leo ni kuendelea na sehemu ya pili ya siri za uvumilivu,Kumbuka tu somo letu lina sehemu tatu. 1.maana ya uvumilivu. 2.faida za uvumilivu. 3.hasara za kukosa uvumilivu.
Ni vizuri kama utafatilia sehemu ya kwanza kwa kuingia Google search na kuandika kalivubha blog siri za uvumilivu utaletewa sehemu hiyo. ....karibu tuendelee.

     2.FAIDA ZA UVUMILIVU.

Kwenye maisha tunayoishi kuna hali kuu mbili zinazochanganya watu wengi sana katika kufanya maamuzi, hali hizo ni kupata kitu kwa wakati na kupata kitu nje ya wakati .Ili kuweza kuzitawala hali zote hizo mbili bila kufanya maamuzi hatarishi inahitaji uvumilivu. Nmejaribu kuelezea faida za uvumilivu kupitia hali zifatazo.

1.Kukwepa hasara, katika mazingira tunayopitia kuelekea ndoto zetu kuna faida na hasara tuzipatazo kama matokeo ya yale tufanyayo. .....zipo hasara zinakuja kama changamoto, ila zipo hasara huja kama matokeo ya kupoteza uvumilivu, .......mara nyingi mtu akishindwa kutawala hisia zake kwenye mazingira yasiyo ya kawaida hujikuta amefanya maamuzi yasiyo ya kawaida ambayo ni HASARA.


2.Kujiongezea thamani ; Wanasikolojia tuna amini kuwa mtu mwenye uvumilivu huwa ana tabia ya kunyamaza pia kwenye mazingira yenye kuhitaji uvumilivu, hii huongeza thamani ya mtu huyo kwenye jamii, maana anakuwa amefanikisha kuzitawala hisia zako ambazo zingepelekea matokeo mabovu kulingana na maamuzi yenye kukosa uvumilivu. ....

3.Kutimiza ndoto;   kila mtu mwenye kujitambua lazima awe na ndoto za maisha, ....ila taarifa isiyo pendeza masikioni kwa wengi ni kwamba.  ili kufanikisha ndoto zako huwa inahitaji muda mrefu kidogo. ....taarifa hiyo sio nzuri kwa wengi maana watu wengi hupenda njia za mkato ktk kuelekea ndoto zao,  ila kwa kuwa swala la kufikia ndoto zetu linahitajI muda wale wavumilivu tu ndo wamekuwa wakifikia ndoto zao.

Kumbuka kuwa uvumilivu sio Kazi rahisi, lazima uumie, ila ukiweza kubeba maumivu ya UVUMILIVU , kuna uwezekano ukaziishi ndoto zako.

     karibu tena katika sehemu ya tatu na ya mwisho wiki ijayo.

                   
                    See you at the top.
               scientist Saul kalivubha.
                         (0652 134 707 )

Friday 7 April 2017

SIRI ZA UVUMILIVU -1.

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya maisha, nashukuru Mungu kwa kuendelea kutupigania, ...karibu.
Leo nataka tujifunze somo la uvumilivu kwenye harakati zetu za kuelekea ndoto zetu.


KUSUDI LA SOMO.

somo letu la siri za uvumilivu limelenga kufundisha sehemu zifatazo. 1.maana ya uvumilivu. 2. faida za uvumilivu. 2.Hasara za kukosa uvumilivu. ..karibu kwenye sehemu ya kwanza ya somo hili.


1.MAANA YA UVUMILIVU.

Kuna watu ambao wana tumia neno uvumilivu ila hawajui maana yake, kuna watu wengine wanajua maana yake ila wanashindwa kuliishi neno uvumilivu hasa pale wanapokutana na mazingira yenye kuhitaji uvumilivu. nimetumia mifano kulifafanua neno uvumilivu, karibu tujifunze.



  • Uvumilivuni ni uwezo wa kutawala hisia zako kipindi unapopata matokeo tofauti na makusudio yako, Wanasikolojia wanazunguwa kuwa moja ya zoezi gumu ni kutawala hisia zako kipindi unapopata matokeo tofauti na makusudio yako. .....hii inasababishwa na tabia ya binadam kupenda kila kitu kifanyike ndani ya uhitaji wake. ....ila kuna mazingira ambayo lazima uweke uvumilivu , ....sio kila kitu utakipata ndani ya muda unaohitaji wewe,  ukiweza kutawala hisia zako kipindi hicho utakuwa umeliishi neno uvumilivu.



  • .Uvumilivu ni uwezo wa kutawala hisia zako kipindi watu  (rafiki zetu ) wanaposhindwa kutufanyia kama tunavyohitaji. ....maamuzi ambayo wengi tumefanya hasa pale rafiki zetu wanapofanya tofauti na tutakavyo huwa ni maamuzi yaliyokosa uvumilivu, ni maamuzi ya kubadili  (badala ya maamuzi ya kusubiri wakati mwingine )......uwezo wa kutawala hisia zako ndani ya mazingira hayo ni tafasiri ya kuliishi neno uvumilivu. .



  • .Uvumilivu ni UPENDO, kipimo cha Upendo kipo kwenye uvumilivu, ukiona umeshindwa kufanya uvumilivu wajambo flani kuna uwezekano mkubwa kuwa huna Upendo wa dhati na jambo hilo linalohitaji kuvumiliwa...



Kuliishi neno uvumilivu ni zoezi ngumu, ila matokeo ya kutoliishi neno hilo ni wengi wetu kupoteza ndoto zao. .lazima tuwe wavumilivu ili tuweze KUFIKIA NDOTO ZETU. ......jiulize swali hilI, Utabadilisha maamuzi mangapi? ..maana matokeo ya kukosa uvumilivu ni kubadili mawazo.
Tukutane wiki ijayo katika sehemu ya pili.    

                     See you at the top.
                    scientist Saul kalivubha.
                       0652 134 707.