Monday 22 February 2021

MIAKA 29 YA SAUL KALIVUBHA

 Karibu katika blogu yetu ya fikiandotozako na kama ilivyo ada leo nitajibu maswali ambayo yaliuzwa katika siku yangu ya kumbukizi ya kuzaliwa tarehe 22 February , maswali yalikuwa jumla 150 na nilipitia yote ijapo yalikuwa sehemu mbili tu 

Mahusiano 

Mafanikio binafsi 

Mahusiano, hapa maswali yalikuwa mengi sana zaidi ya robo tatu yalikuwa ni maswali ya mahusiano sikushangaa sana kuulizwa maswali mengi namna hiyo kwa sababu mfumo wangu wa maisha moja ya eneo ambalo silionyeshi wazi ni mahusiano na mafanikio yangu binafsi.

Kwa sasa watu wengi hupima mahusiano ya mtu mitandaoni na ukifuatilia kurasa zangu sijawahi chapisha ( post) chapisho lolote iwe picha au maneno yenye viashiria vya mahusiano huo ni utaratibu wa mtu mwenyewe kwangu upo hivyo sina maana kuwa anayeweka wazi mitandaoni anakosea la hasha.Wengi waliuliza nitaowa lini na nitamuoa nani? 

Katika mahojiano fulani niliwahi kuzungumza kuwa siku nikitoa kitabu changu cha tatu itakuwa sambamba na harusi yangu na tayari michakato ya kutoa kitabu hicho cha jina la NTAOWA BILA UCHUMBA ipo mbioni kwa hiyo sina haja ya kusema siku bali tusubirie, nani nitamuoa?  nikijibu swali hilo itakuwa nimerudi kule kule kupost ( chapisha mirandaoni) hivyo mniwie radhi kwa hilo siku ikifika kwa mwenye kutaka kumjua atamjua. 

Sipendi sana kuweka maisha binafsi mitandaoni kwa sababu kuu mbili;

1.Maisha binafsi sio biashara niitangaze 

2.Huduma zangu mitandaoni sio kuwaambia watu ninaishije bali kuwaonyesha matokeo ya ninavyoishi ikiwemo kuhamasisha kwa kilicho ndani ya uwezo wangu 

Mafanikio binafsi,watu walitaka kujua uandishi umenipa nini mpaka sasa ni kweli nina miaka minne sasa kwenye tasnia hii na kwanza kabisa kama mafanikio kwangu ni kujiweka kwenye orodha ya watu kama msaidizi wa mafanikio yao hayo ndio mafanikio zaidi kwangu lakini pia mafanikio ya kiuchumi kwa uandishi yapo pia kwa sababu kuna kipindi nimeishi karibia mwaka sina kazi yoyote tofauti na uandishi na maisha yaliendelea,pia kupitia uandishi niliweza kununua mshamba nikalima na kiasi fulani nikaingiza kwenye ujenzi wa nyumba yangu.Nimedokeza machache na kuvunja utaratibu wangu wa kutoweka wazi maisha binafsi bali nimefanya hivyo kama hamasa kwa watu kuwa hatuapaswi kuchoka na safari 

Maisha ya uandishi ni kipaji hivyo tokea nitambue hilo nikaamua kuayapa nafasi kwangu kwa sababu kuna watu wanauliza naweza vipi ilihali nimesoma afya? Inawezekana kabisa ni suala la nidhamu tu nikiwa kwenye mambo ya afya nakuwa makini huko nikitoka mashmabulizi huamia kwenye uandishi. Uandishi nina ufanya kama sehemu ya maisha lakini miaka ya mbele itakuwa ndio shughuli yangu kuu.

Mashairi ni kipaji? Mashairi ni kipaji ijapo pia mtu anaweza kusomea hivyo kwangu ni kipaji lakini baadaye nikajiboresha huko zaidi kupitia vitabu

Kwanini riwaya ya NTAOWA BILA UCHUMBA?  hiyo ni hadithi tu ambayo nimeamua kuiandika na sina maana kuwa nitaowa bila uchumba na pengine zama zetu hizi ikawa ngumu kufanya hivyo kwa sababu inahitaji muda kukaa na mlengwa ili mufahamiane katika mbili tatu kisha ndio hatua nyingine ifuate lakini kwenye hadithi hiyo nilimaanisha  hakuna haja ya uchumba bandia .

Kila mtu anatamani kufikia eneo fulani kimafanikio na hiyo ndio chachu inayochochea upambanaji wa mtu husika kama hauko tayari kuyasaliti malengo yako lazima kila siku ujitume 


Mwanasayansi Saul Kalivubha 

0652 134707