PAGES

Showing posts with label URAFIKI. Show all posts
Showing posts with label URAFIKI. Show all posts

Friday, 16 February 2018

KWA NINI RAFIKI YAKO HAKUAMINI?

Tarehe 22 FEBRUARY ni siku ambayo nasherehekea siku ya kuzaliwa kwangu......pamoja na furaha yote ya siku hiyo,huwa ni siku pia ambayo nimejiwekea utaratibu wa kukumbuka mambo ambayo yalitokea kwenye safari yangu ya maisha......kiufupi safari yangu kwa asilimia kubwa ilikuwa ya maumivu......hapo ndipo nakumbuka nafasi ya rafiki katika maisha yangu........karibu.

KUSUDI LA SOMO.

Lengo la somo hili ni kutaka kutoa majibu ya kwa nini huna imani na rafiki yako?.....au kwa nini yeye hakuamini?.....hii ni vita kubwa sana ambayo inayumbisha urafiki wa watu wengi na kusababisha kifo cha urafiki..........karibu.

KWA NINI HUNA IMANI NARAFIKI YAKO?.......Sabubu za kwa nini humuanini rafiki yako zipo sawa na kwa nini yeye hakuamini.........hivyo ngoja nielezee sababu zinazo fanya ukose imani na rafikiyako.....kisha utazigeuzia upande wa pili.

1.HISTORIA YAKE.......kufahamu historia ya rafiki yako sio vibaya.na inaweza isiwe hatari kabisa kwa yeye kuptia historia hiyo...tatizo liko wapi?.........hadi wewe kukubali kuwa na urafiki na mtu unayejua historia yake,ni wazi uliamini kuwa kabadilika....lakini kubadilika kwake haina maana kuwa attaishi bila madhaifu yoyote yale........kosa lipo pale ambapo utaanza  kuunganisha madhaifu yake ya kawaida na maisha aliyopitia.....ukiruhusu hali hiyo,nakuhakakishia,hutomuamini hata kidogo,utakuwa mtu wa wasiwasi tu muda wote......ukiona huna busara ya kubeba historia ya nyuma ya rafiki yako,au umejiaminisha kuwa bado hajabadilika......kuwa mbali.

2.HISTORIA YAKO,.....Usipokuwa mwenye hekima na busara,kile unachokitenda au umechotendewa au kuona wengine wakitendewa,kitakufanya uamini watu wote duniani wapo hivyo.....hali hii ukiiruhusu,itakufanya ujihami.....unajua madhara ya kujihami?.......KWANZA wewe mwenyewe utakuwa sio muaminifu,pili, rafiki yako utampa uhusika wako ....hutomuamini pia........kuna kipindi inabidi uishi bila hamasa za nje,hamasa ambazo ni za mawazo hasi.,,,zitakufanya uingiwe na ugonjwa wa kutoamini watu wasio na hatia............

 Hapa nakumbuka utafiti wangu ambao niliufanya ili kugundua ni kwa namna gani watu hawana imani na marafiki zao sababu zilizosababisha hivyo........nilitumia marafiki wa jinsia tofauti,,,,wavulana kumi ambao nilwaulizwa wanajisikiaje ikitokea simu ya rafiki wake wa kike  haitapokelewa au itakuwa busy(kutumika)  pindi wakiwatafuta.......maatokeo yalikuwa hivi:

SITA walisema ,wakikuta hali hiyo,watahisi kusalitiwa,wawili walisema watajisikia vibaya tu.....wengine wawili wa mwisho walisema hiyo ni hali ya kawaida tu......kwa ufupi utafiti huo unaonyesha ni namna gani uaminifu umepungua ......nilivyofatilia zaidi kwa marafiki hao sita ndipo nikapata somo hili la leo......ndani ya sababu hizo mbili kuna sababu ndogo ndogo nyingi.....


Makala hii imeandikwa na Saul Kalivubha.....Mkurugenzi wa label ya FIKIA NDOTO ZAKO.

                                  06552 134707.


Sunday, 16 July 2017

SIRI YA KUMI YA URAFIKI.

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya mafunzo ya maisha na jinsi ya kufikia ndoto zetu,nina imani wewe hapo ni mzima wa afya,kama ni mgonjwa usijali,Mungu yupo kwa ajili yetu wote.


  KUSUDI LA SOMO.
Lengo la somo letu la leo ni kujifunza siri ya kumi ya urafiki ambayo ni UKWELI ,ila kabla ya kuendelea mbele ni vyema ukapitia na kujifunza kwanza siri ya tisa ya urafiki(SIRI YA TISA YA URAFIKI).


           SIRI YA KUMI  YA URAFIKI   (UKWELI).
Kwenye urafiki kuna kuwekana wazi mambo,ila kabla ya kuweka wazi mambo yako kwa rafiki yako lazima kwanza uwe umejihakikishia uaminifu wa kutosha ,ila wakati mwingine kuna watu wapo kwenye urafiki kwa kuficha ukweli,wanatumia uongo kutengeneza ukaribu wao....je hii ni sahihi?


Wanasaikolojia wa mambo ya mahusiano wanazungumza kwamba ...Watu wanatafuta wasiyoyafahamu,hawana shida na wanayoyafahamu,,,hii tafasiri yake ni kwamba rafiki yako anatafuta mambo ambayo hayafahamu kutoka kwako,inaweza kuwa umemdanganya jambo fulani,siku akilifahamu lazima sura ya urafiki wenu ubadilike,...jifunze kuwa mkweli.


Ni bora kumficha mtu jambo kuliko kumdanganya,sababu za kumficha mtu jambo zinaweza kuwa zina maana kubwa kuliko sababu za kumdanganya mtu,,,,,kumdanganya maana yake umemwambia ukweli wenye hila ndani yake,umetafuta kuaminiwa kwa njia isiyosahihi.



Ukiona rafiki yako amekukwepa kwa sababu umemwambia ukweli,jua huyo sio mtu mzuri kwako,maana ukweli una thamani kubwa sana kwenye urafiki wa kweli,urafiki ambao una lengo la kufikia mafanikio makubwa.


Tatuzo ukisha anza na uongo tu kwenye urafiki wako,itakufanya kila siku uendelee kutengeneza uongo wa kudumisha uomgo wa mwanzo....urafiki wa aina hiyo una umuhimu gani?, ukijiona mjanja wa kudanganya ,tambua thamani yako inashuka,pia unapoteza muda wako kudanganya na kuendeleza uongo wako.



Kitabu cha SIRI ZA URAFIKI kinaelekea kuwa tayari,utakipata kwa mawakala wa fikia ndoto zako....


                           See you at the top.
                    Scientist Saul kalivubha.
                              0652 134707

Monday, 10 July 2017

SIRI YA TISA YA URAFIKI

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa mafunzo ya maisha na jinsi ya kufikia ndoto zetu,nashukuru Mungu kwa uzimab wake kwangu ,pia ni imani yangu kuwa wewe ni mzima........karibu.



   KUSUDI LA SOMO.

Tunaendelea na somo letu la siri za urafiki,leo ni siri ya tisa ambayo ni mipaka ya ufahamu,...kabla yakuendelea na somo letu hili,ni vyema ukajifunza kwanza siri ya nane ya urafiki(SIRI YA NANE).,karibu tuendelee.



SIRI YA TISA YA URAFIKI(MIPAKA YA UFAHAMU).

Katika urafiki ni jambo la kawaida sana kufahamu habari za rafiki yako,swala hili ni zuri sana ikiwa unataka kufahamu habari hizo kwa lengo la kudumisha urafiki,ila kuna habari zingine za rafiki yako zinaumiza,kama hauna ujasiri,badala ya urafiki kuimarika,utavunjika......kabla ya kuanza kuzifatilia habari za rafiki yako jitahidi kufahamu haya.

  • Weka mipaka,hakikisha unafahamu mambo yenye fada tu katika ujenzi wa urafiki.
  • Kuwa makini na chanzo cha habari, sio kila chanzo cha taarifa za rafiki yako ni chanzo sahihi.
  • usifatilie habari za rafiki kama kumpeleleza,akijua urafiki wenu utapoteza uaminifu,kuwa mpole na taratibu tu utafahamu mengi kuhusu yeye.
  • Fanyia kazi mambo utayo yafahamu kwa rafiki yako kwa lengo la ujenzi na sio kwa leng la kumuhukumu rafiki yako.


Mwamdishi mmoja wa mambo ya saikolojia aliwahi kuandika kanuni moja muhimu sana ,kanuni hiyo ni hii   "Msongo wa mawazo(Stress) unaongezeka,kila ufahamu unapoongezeka"
Kanuni hii inasaidia kupunguza kufahamu mambo yasiyokuhusu,watu wengi kwenye urafiki wanaishi kwa mawazo kwa sababu tu walifatilia mambo yasiyo wahusu ya rafiki zao.


Kuna mambo sio lazima uyafahamu kutoka kwa rafiki yako,utaumiza kichwa bure tu,tena kibaya zaidi hakuna uwezo wa kuyabadilisha mambo hayo,tena kuyafahamu kwako hakuna faida yoyote kwenye uraki wako .....


                        See you at the top.
                            Saul kalivubha
                               0652 134707.

Sunday, 2 July 2017

SIRI YA NANE YA URAFIKI.

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya mafunzo ya maisha, nashukuru Mungu kwa uzima wangu na wako pia. ......Karibu sana kwenye muendelezo wa somo letu la urafiki, nina imani kuna kitu unajifunza. ..karibu.

LENGO LA SOMO. 
Lengo la somo letu la leo ni kujifunza siri ya nane ya urafiki kulingana na mpangilio wangu, siri hiyo ni  Jichunguze tabia yako. ... .Unaweza pitia kwanza SIRI YA SABA, kisha uje tuwe wote. .....karibu tuendelee.

SIRI YA NANE  (JICHUNGUZE TABIA YAKO ).

Urafiki unapitia mazingira mengi sana, kila mazingira huwa yanahitaji style  (mfumo ) wa kuishi ili kuhakikisha urafiki unaendelea na thamani yake.Ila kuna kipindi mtu anaona rafiki yake kabadilika tabia, amekuwa na tabia mpya ambayo hapo nyuma hakuwa nayo.

  • Je umewahi kukutwa na hali hiyo? 
  • Urafiki wako ulikuwa na sura gani baada ya hali hiyo? 
  • Unafikiri chanzo chake ni nini? 
Ni hali ya kawaida sana kusikia mtu akilaumu kuhusu kubadilika kwa tabia ya rafiki yake, tena kwa sababu nyingi za kujiona yeye mshindi na kumfanya rafiki yake kuwa mwenye hatia. ..
Tabia inatoka wapi?
Kila tabia lazima itanguliwe na mazingira flani, mazingira ambayo ndio chanzo cha tabia hiyo, hakuna tabia inayo tokea bila kusababishwa. ....!
Inawezekana tabia ya rafiki yako imetokana na mazingira yako, mazingira uliyoyajenga kwa huyo rafiki yako. Hakikisha kabla ya maamuzi ya kumpoteza rafiki yako kwa kigezo cha kuwa na tabia mpya,Jichunguze kwanza wewe, Jichunguze tabia yako, inawezekana wewe ndio chanzo.

Kumpoteza rafiki zako bila kujifanyia uchunguzi kwanza, ni kosa kubwa sana, unaweza usidumu na rafiki yoyote kwa sababu tu hujafanya mabadiliko ya tabia yako. .
Tukutane wiki ijayo.

            See you at the top.
           scientist Saul kalivubha.
               0652 134 707.
0

Sunday, 25 June 2017

SIRI YA SABA YA URAFIKI

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya mafunzo maisha na jinsi ya kufikia ndoto zetu,nashukuru Mungu kwa kuendelea kutupigania hadi sasa ,hongera sana kwa kuwa na afya njema,kwa wale wagonjwa poleni sana ila Mungu niwetu sote.

KUSUDI LA SOMO.
Leo nataka tuendelee na somo letu la urafiki,kabla ya kuendelea na siri ya saba, jifunze kwanza     ( SIRI YA SITA),Kisha tuendelee na siri ya saba ya urafiki ambayo ni tasmini ya uchaguzi wa rafiki,.....karibu tujifunze.

SIRI YA SABA YA URAFIKI(TASMINI YA UCHAGUZI).

Kuwa na rafiki flani ni ni matokeo ya uchaguzi uliofanya,hakuna kulazimisha kwenye mambo ya urafiki,huwa ni hiari ya muhusika,je uchaguzi wako una matokeo gani?

Kila uchaguzi lazima uwe na matokeo,matokeo ya uchaguzi ndio sehemu ambayo tunaitumia kupima kufanya evaluation(tasmini) ya usahihi wa mtu katika uchaguzi wake,....hii ni sehemu ambayo kila mtu anapaswa kuifanya yeye binafsi, je nini kinafata baada ya tasmini ya matokeo?

Matokeo ya uchaguzi wa rafiki yana sehemu ya kuvumilikika ambayo ni moja ya madhaifu ya binadamu, ila matokeo yanaweza kuwa pia hayaruhusu urafiki uendelee,hapa lazima uchukue maamuzi magumu,bila hivyo itakuwa ngumu kwako kufikia ndoto zako......


Zoezi la tasmini ya matokeo ya urafiki huwa ni ngumu kidogo, maana kuna watu wanachukua maamuzzi magumu kwa kukwepa changamoto za urafiki tu ,kwa hiyo inahitaji umakini sana katika zoezi hili,,,,,,
Jiulize swali hili,....matokeo ya uchaguzi wa rafiki uliyrnaye yana endana na ndoto zako?,kama sio ,unafanya nini kwemye urafiki huo?

Habari ya kusikitisha kwenye urafiki ni kwamba,watu wengi wanaweza kugundua hawapo kwenye njia sahihi,ila wakwa wanajifariji ,mwisho wa siku wanafanya maamuzi magumu tayari walisha poteza thamani yao,,,,,,,fanya tasmini,chukua maamuzi sahihi.....

                          See you at the top
                        Scientist Saul kalivubha.
                               0652 134707

Sunday, 18 June 2017

SIRI YA SITA YA URAFIKI

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya mafunzo ya maisha,nashukuru Mungu kwa kuendelea kutupigania,maana nina imani kuwa na wewe ni mzima,.....karibu tujifunze.

Kusudi la somo.

Leo ni muendelezo wa siri za urafiki,tunaendelea na siri ya sita ya urafiki ambayo ni utatuzi wa migogoro,kabla ya kuendelea mbele ni vyema ukajifunza kwanza  SIRI YA TANO ,Karibu tujifunze.

UTATUZI WA MIGOGORO YA URAFIKI.

Jambo la kufahamu kwenye urafiki ni kwamba ,unakutana na mtu ambaye hujazaliwa naye,ana madhaifu yake na pengine ana historia yake ya maisha tofauti na yako.......lazima kuna migogoro itatokea tu ndani ya urafiki,,,,,jaribu kujibu maswali haya kabla ya kuendelea mbele......je umewahi kuingia kwenye mgogoro na rafiki zako?,ulifanya maamuzi gani ?.baada ya maamuzi hayo urafiki wenu ulipata sura gani?

Migogoro kwenye urafiki ni muhimu sana kwani ni dalili ya kuonyeha hali ya kutokuwa sawa sehemu flani,ila inaweza kuwa na madhara ya kudumu kwa wahusika endapo watashindwa kutambua sababu za utokeaji wa migogo hiyo,

Uwezo wa utatuzi wa migogoro ya urafiki bila kuharibu thamani ya muhusika ndio kipimo kizuri cha uwezo wa uendeshaji wa urafiki.


Mambo muhimu ya kuzingatia kwenye utatuzi wa migogoro.
  1. Kabla ya maamuzi yoyote hakikisha unajua chanzo cha tatizo .
  2. Usipende kuonekana mshindi,ili kumudu hili hakikisha unatawala hisia zako za hasira ili usifanye maamuzi yenye msingi wa hasira.
  3. Kama kosa lipo kwa rafiki yako,vaa uhusika ili upime yeye angefanya maamuzi gani juu yako.
  4. Usipende kutumia ushauri wa watu wengine katika kutatua mgogoro unaokuhusu wewe.
  5. Hakikisha unajua tafasiri ya kila changamoto kwenye urafiki wako,ili ufanye maamuzi ambayo hayana majuto.


Kumbuka tu ili uweze kufikia ndoto zako ni muhimu uwe kwenye system ya marafiki waliobeba kusudi lako,ila kuwa na rafiki ambaye kabeba kusudi lako sio tafasiri ya kutokuwa na migogoro.

                   See you at the top.
     scientist SAUL KALIVUBHA.
                   0652 134 707.

Sunday, 11 June 2017

SIRI YA TANO YA URAFIKI

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya maisha, nashukuru Mungu kwa afya yangu pamoja na wewe. ....karibu.

  KUSUDI LA SOMO.
Lengo la somo la leo ni kuendelea na sehemu ya tano ya siri ya Urafiki. ..ni vyema ukajifunza sehemu ya nne SIRI YA NNE  kisha uendelee na siri ya tano( SIRI YA NNE)..... lengo la kufundisha urafiki ni kutaka tufahamu jinsi ya kuishi na marafiki kwa lengo la kufikia ndoto zetu ...maana mafanikio yako yapo kwa rafiki yako. ...karibu.

SIRI YA TANO YA URAFIKI.
Siri ya tano ya urafiki ni  mawasiliano .Kwenye mawasiliano tuangalie kwenye upande mmoja tu. jinsi mawasiliano yanavyoweza kuvunja urafiki. ....nafikiri utakuwa tayari umeshuhudia urafiki ukivunjika kwa sababu ya mawasiliano. ....au inaweza kuwa umekutwa na tatizo hili la kupoteza marafiki kwa kigezo cha mawasiliano. ....
Mawasiliano yanaweza kavunja urafiki kupitia sehemu hizi.

  • Mawasiliano mabovu, ..hapa nina maanisha kiwango cha chini cha mawasiliano au mawasiliano ambayo hayana hisia za Upendo. ....kila mazingira yana aina yake ya mawasiliano na kiwango chake, ukiwa kwenye mazingira yenye kuhitaji mawasiliano kwa wingi ila wewe ukafanya chini ya kiwango , urafiki utakuwa unaelekea kwenye hatari ya kuvunjika. ....jitahidiutambue aina ya urafiki uliyonayo, mazingira mliyopo. .ili ufanye mawasiliano yanayostahili. 
  • Mawasiliano hupoteza thamani ya habari, ...utafiti wa kisaikolojia unaonyesha kwamba habari inavyozidi kupita mikononi kwa watu wengi ndio inavyozidi kupungua uhalisia wake, ila kuna watu bila kufanya utafiti wa kina wamekuwa wakifanya maamuzi ya kudumu kwa kupitia taarifa imeyopitia mikononi kwa watu wengi. ..hali hii imefanya watu wengi kupoteza marafiki .....fanya tasmini kabla ya maamuzi, unavyozidi kuwa mbali na chanzo cha habari ndivyo ukweli wa taarifa unavyozidi kupungua. .....
             Seeyou at the top. 
        scientist Saul kalivubha. 
          (0652 134 707)






Wednesday, 31 May 2017

SIRI YA NNE YA URAFIKI

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa mafunzo ya elimu ya maisha kwa lengo la kufikia ndoto zetu,nashukuru mungu kwa kuendelea kunipigania mimi pamoja na wewe...........karibu.


KUSUDI LA SOMO.
Lengo la somo letu la leo ni kujifunza siri ya nne ya urafiki ambayo ni uvumilivu,ili tuwe pamoja jifunze kwanza SIRI YA TATU kwa kubofya hapa.SIRI YA TATU,..........ikumbukwe tu rafiki ana sehemu kubwa sana kwenye ndoto zetu,hii ndio sababu ya mimi kufundisha somo hili.

SIRI YA NNE YA URAFIKI(UVUMILIVU).
Uvumilivu ni uwezo wa kuzitawala hisia zitokanazo na mambo yasiyo pendeza,hisia ambazo zikiruhusiwa zinaweza kuwa hanzo cha matokeo hasi(negatives effects).........kwenye urafiki pia kuna mambo ambayo yanahitaji kuvumiliwa,ndani ya urafiki kuna mambo yasiyopendeza yenye lengo la kuimarisha urafiki,mtu usipo kuwa mvumilivu unaweza kuwapotezamarafiki wengi sana wasio na hatia..............

Uvumilivu katika urafiki unahitajika sana hasa kwenye hali kuu mbili zifatazo:



  • MADHAIFU;watu wengi wanaingia kwenye urafiki wakiwa na picha ya madhaifu machache waliyo yaona kabla ya kuanza urafiki,ila kuna madhaifu mengine ya ndani ambayo huwezi kuyaona hadi uingie kwenye urafiki,......usipokuwa mvumilivu ,madhaifu haya ya ndani yana nguvu kubwa ya kuvunja urafiki.

  • CHANGAMOTO:Changamoto ni moja ya sehemu muhimu sana ya urafiki,ni sehemu ambayo inahitaji uvumilivu wa hali ya juu,pia ni sehemu ambayo inahitaji matumizi ya hekima na busara,maanakila changamoto ina jambo la kufundisha kwenye urafiki wako.....kuna usemi mmoja unasema "Kama upo kwenye urafiki usio na changamoto yoyote ile,kaa chini ufikirie tena mara ya pili"

              See you at the top.
          Scientist Saul kalivubha.
                (0652 134707)

Wednesday, 24 May 2017

SIRI YA TATU YA URAFIKI.

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya mafunzo ya maisha, ....nashukuru Mungu kwa kuendelea kutupigania hadi sasa.......karibu.

KUSUDI LA SOMO. 
Lengo la somo letu hili la leo ni kuendelea kujifunza siri za urafiki, na leo tupo kwenye siri ya tatu ambayo ni kujiamini.......karibu tujifunze. ..jifunze siri ya pili kwanza siri ya pili ya urafiki

               SIRI YA TATU YA URAFIKI.
Kujiamini ni hali ya kujiona mkamilifu..kujiona upo kwenye mazingira sahihi ya kufanya jambo flani, ....kinyume chake ni kutojiamini ..kujiona mwenye mapungufu au kujiona huna vigezo vinavyotakiwa......ina madhara gani kwenye urafiki? ......sina tatizo na mtu anayejiamini. ..ila kwa asiye jiamini karibu tujifunze. ........

Mtu asiye jiamini kwenye urafiki anakuwa muda wote anahisi kuachwa au kumpoteza rafiki yake. ...hali hii ina madhara gani? 
Hali ya kutojiamini inasababisha mtu atumie nguvu kubwa kuendesha urafiki, kutumia nguvu kubwa ni pamoja na kutumia sifa ya ziada. ..

Mtu asiye jiamini lazima atafute sifa ya kujiongezea ili aweze kujiona mkamilifu. ....hivyo urafiki wake unakuwa umejengeka ndani ya sifa yake ya ziada na sio uhalisia wake. ...

Wanasikolojia wanashauri kwamba, ukiona una tatizo la kutojiamini ni bora ukalitatatua kwanza kabla ya kuingia kwenye urafiki. .mbali na hivyo utasumbuka sana. ...
         
             See you at the top. 
           scientist Saul kalivubha. 
            (0652 134 707 )




Thursday, 18 May 2017

SIRI YA PILI YA URAFIKI


karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya mafunzo ya maisha. ...nashukuru Mungu kwa neema yake kwangu. .........karibu tujifunze.

Kusudi la somo.
Lengo la somo letu hili ni kujifunza siri ya pili ya urafiki. ....Nimeona vyema kufundisha somo hili kwa sababu najua urafiki una sehemu kubwa sana kwenye mafanikio yetu. ....karibu.

SIRI YA PILI YA URAFIKI. 
Tuangalie siri ya pili ya urafiki. ..unaweza kujifunza siri ya kwanza ya urafiki kwa kuandika kalivubha blog siri ya kwanza ya urafiki. ....kisha ndio uendelee na mimi kwenye somo hili.
(siri yakwanzayaurafiki )...

Siri ya pili ya urafiki ni hii USIFANYE URAFIKI KWA MAJARABIO...........

Moja ya sababu inayofanya urafiki upungue thamani ni kubadilika kwa mazingira ambayo yalitumika kutengeneza urafiki. ...kwa nini mazingira yabadilike? ......kuna watu ambao wana tabia ya kufanya majarabio ya urafiki. ...wengi wao hufanya hivyo ili kuangalia kama urafiki huo una weza kutimiza mahitaji yake. .....

Urafiki wa aina yoyote ile una changamoto zake. ...hivyo mtu anayeingia kwenye urafiki kwa majarabio hawezi kuvumilia changamoto. .....mara nyingi watu wanaingia kwenye urafiki kwa majarabio wana sifa kuu tatu.

1.Sio wavumilivu wa changamoto.

2.muda wote wanawaza kubadili marafiki.

3.Wanatumia nguvu kubwa kuanzisha urafiki. ....hufanya hivi kwa sababu wanakuwa wanataka waone kama watatimiza malengo yao ..kama hapana basi wabadili marafiki  ...........
Jiandae kupata kitabu cha SIRI ZA URAFIKI  .
     
                      See You At The Top.
                        Saul kalivubha.
                         (065123707 )



Monday, 15 May 2017

SIRI YA KWANZA YA URAFIKI.

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya mafunzo ya maisha, nashukuru Mungu kwa kuendelea kutupigania hadi sasa ......karibu.

Kusudi la somo.
Leo nataka tujifunze siri moja ya urafiki ambayo wengi hawajui, au wanaijua lakini hawaitumii. ....mwalimu wangu aliwahi kuniambia kwamba, ikiwa una ujuzi usio kusaidia, ...huna cha kujivunia. ....karibu tuendelee.

         SIRI YA KWANZA YA URAFIKI(SIFA YA ZIADA ).

Kwa nini urafiki? ..... utafiti unaonyesha mafanikio yetu yapo ndani ya rafiki zetu wa karibu. ...hii ndio sababu ya mimi kuandika somo hili. .....Siri ya kwanza ni ipi?
Siri ya kwanza kwenye urafiki ni ...sifa ya ziada .....

Sifa ya ziada ni ni sifa ambayo mtu anajiongezea kwa lengo la kumvutia rafiki yake. ..  hali hutokea mwanzoni mwa urafiki, .....nini madhara yake?

Kuna watu wapo kwenye urafiki mzuri, ila urafiki huo unaendeshwa na sifa ya ziada ambayo mmoja katika urafiki huo anaitumia. .Mtu ambaye anaitumia sifa ya ziada kuendesha urafiki, anatumia nguvu kubwa sana. ...tena nguvu anayoitumia ina mrudisha sana nyuma kimafanikio na ina mpa madhara ya kisaikolojia. ......!

Je, una uwezo wa kuyaishi maisha yaliyobebwa na sifa ya ziada?

Kila siku tunashuhudia kuvunjika kwa urafiki ambapo sababu kubwa ni mmoja wapo kwenye urafiki kupoteza sifa ya ziada aliyojipatia. ...
Tiba pekee kabla ya kuwa na rafiki, hakikisha unaishi maisha yako. ....be you, be smart. (ishi maisha yako, kuwa nadhifu )....utapata rafiki aina yako.

                See you at the top.
         scientist Saul kalivubha.
            (0652 134 707 )