Monday, 6 October 2025

MAMBO YA KUFANYA ILI KUVUKA KIPINDI CHA KUKATALIWA BILA WEWE KUDHURIKA

Kukataliwa sio kitu kigeni kwa sababu uzoefu unaonyesha karibu kila mtu ameshaonja kipindi hiki na hata kama bado basi kuna siku utakipitia .

Inaweza kuwa ndugu, marafiki, makazini au katika mahusiano kote kuna kakataliwa .

Ni kipindi kigumu sana kukabiliana nacho kwa sababu ki asili binadamu tunapenda kukubaliwa hivyo ianapotokea kukataliwa maumivu yake huwa ni makali sana bila kuwa na  ukomavu athari huwa kubwa ikiwemo na kujitoa/kutoa uhai .

UFANYEJE SASA UKIWA KWENYE KIPINDI HICHO?

1.Kubali ukweli (Ukiruka hii hatua utakuwa unajidanganya kuwa uko sawa ila ki uhalisia bado unateseka hivyo lazima ukubali kuwa HAKUTAKI)

2.Ondoa matumaini kuwa kuna siku ATAJIRUDI ( Usiwe na hayo matumaini kwa kuamini ipo siku atajirudi ukaanza kuwa unamtumia meseji mara unamjulia hali au kuendelea kumshirikisha mambo yako kwa tumaini kuwa atakuonea huruma arudi , utateseka)

3.Usitake umsahau kwa kutafuta mbadala wake( kosa kubwa sana hili )

4.Wekeza nguvu kwenye mambo mengine na futa matukio ambayo yatafanya umkumbuke ikiwemo picha kama mlipiga wote au kusikia nyimbo ambazo mlizipenda kwa pamoja)

5.Usijione mwenye kasoro za kukataliwa ( usianze kutafuta sababu za kujiona hufai)

6.Usianzishe maigizo ya kuaminisha watu kuwa upo sawa na soko lako lipo juu 

7.Muda ndio kidonge cha mwisho kumaliza maumivu yako( Huwezi kuwa sawa kesho itachukua muda hivyo kubali hilo)

8.SHUKURU MUNGU KUKATALIWA KWA SABABU KUNA SEHEMU KAKUANDALIA YA KUKUBALIWA 🙏 


NB : KUCHELEWA KUKUBALI KUKATALIWA NI KUENDELEA KUJICHELEWESHA WEWE MWENYEWE 😔 

#Mwanasayansi Saul kalivubha 

#Fikia Ndoto Zako 

+255652 134707

Thursday, 26 June 2025

UTULIVU NI JICHO LA TATU KUKUPA MAAMUZI SAHIHI HASA KWENYE NYAKATI ZA KUVURUGWA

 

Walioachwa kwenye mahusiano wakakurupukia mengine haraka wakiwa kwenye hali ya  kuvurugwa wengi  wao walijikuta wakikosea tena vibaya zaidi ya mwanzo.

Waliofumania wenzi wao au kusikia taarifa mbaya dhidi ya wenzi wao na wakafanya maamuzi wakiwa kwenye hali ya kuvurugwa wengi walijikuta kwenye maamuzi mabaya na yenye majuto kama vile kuua au kujiua.

Waliojibizana wakiwa kwenye hali ya kuvurugwa wengi walijikuta wakiongea maneno ya hovyo na yaliyokosa hekima kiasi cha kujipotezea heshima. 


Furaha na huzuni vyote vinaweza kupoteza utulivu wako na utulivu ukipotea basi tarajia maamuzi ya hovyo kwa asilimia kubwa. 

Adui wabobevu wanalijua hilo ndio maana wakitaka kukushambulia kirahisi basi watatafuta namna ya kukuvuruga na kukushinikiza ufanye maamuzi ukiwa kwenye huo mvurogo wakiamini ni lazima utakosea tu.

Utulivu ndio silaha pekee kwenye nyakati kama hizo na hapo utapata jicho la tatu la kuona hali halisi na maamuzi gani uchukue .

#Mwanasayansi Saul kalivubha 

#Fikia Ndoto Zako

#Mitandaoni @Fikia Ndoto Zako