Kukataliwa sio kitu kigeni kwa sababu uzoefu unaonyesha karibu kila mtu ameshaonja kipindi hiki na hata kama bado basi kuna siku utakipitia .
Inaweza kuwa ndugu, marafiki, makazini au katika mahusiano kote kuna kakataliwa .
Ni kipindi kigumu sana kukabiliana nacho kwa sababu ki asili binadamu tunapenda kukubaliwa hivyo ianapotokea kukataliwa maumivu yake huwa ni makali sana bila kuwa na ukomavu athari huwa kubwa ikiwemo na kujitoa/kutoa uhai .
UFANYEJE SASA UKIWA KWENYE KIPINDI HICHO?
1.Kubali ukweli (Ukiruka hii hatua utakuwa unajidanganya kuwa uko sawa ila ki uhalisia bado unateseka hivyo lazima ukubali kuwa HAKUTAKI)
2.Ondoa matumaini kuwa kuna siku ATAJIRUDI ( Usiwe na hayo matumaini kwa kuamini ipo siku atajirudi ukaanza kuwa unamtumia meseji mara unamjulia hali au kuendelea kumshirikisha mambo yako kwa tumaini kuwa atakuonea huruma arudi , utateseka)
3.Usitake umsahau kwa kutafuta mbadala wake( kosa kubwa sana hili )
4.Wekeza nguvu kwenye mambo mengine na futa matukio ambayo yatafanya umkumbuke ikiwemo picha kama mlipiga wote au kusikia nyimbo ambazo mlizipenda kwa pamoja)
5.Usijione mwenye kasoro za kukataliwa ( usianze kutafuta sababu za kujiona hufai)
6.Usianzishe maigizo ya kuaminisha watu kuwa upo sawa na soko lako lipo juu
7.Muda ndio kidonge cha mwisho kumaliza maumivu yako( Huwezi kuwa sawa kesho itachukua muda hivyo kubali hilo)
8.SHUKURU MUNGU KUKATALIWA KWA SABABU KUNA SEHEMU KAKUANDALIA YA KUKUBALIWA 🙏
NB : KUCHELEWA KUKUBALI KUKATALIWA NI KUENDELEA KUJICHELEWESHA WEWE MWENYEWE 😔
#Mwanasayansi Saul kalivubha
#Fikia Ndoto Zako
+255652 134707