Sunday, 25 June 2017

SIRI YA SABA YA URAFIKI

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya mafunzo maisha na jinsi ya kufikia ndoto zetu,nashukuru Mungu kwa kuendelea kutupigania hadi sasa ,hongera sana kwa kuwa na afya njema,kwa wale wagonjwa poleni sana ila Mungu niwetu sote.

KUSUDI LA SOMO.
Leo nataka tuendelee na somo letu la urafiki,kabla ya kuendelea na siri ya saba, jifunze kwanza     ( SIRI YA SITA),Kisha tuendelee na siri ya saba ya urafiki ambayo ni tasmini ya uchaguzi wa rafiki,.....karibu tujifunze.

SIRI YA SABA YA URAFIKI(TASMINI YA UCHAGUZI).

Kuwa na rafiki flani ni ni matokeo ya uchaguzi uliofanya,hakuna kulazimisha kwenye mambo ya urafiki,huwa ni hiari ya muhusika,je uchaguzi wako una matokeo gani?

Kila uchaguzi lazima uwe na matokeo,matokeo ya uchaguzi ndio sehemu ambayo tunaitumia kupima kufanya evaluation(tasmini) ya usahihi wa mtu katika uchaguzi wake,....hii ni sehemu ambayo kila mtu anapaswa kuifanya yeye binafsi, je nini kinafata baada ya tasmini ya matokeo?

Matokeo ya uchaguzi wa rafiki yana sehemu ya kuvumilikika ambayo ni moja ya madhaifu ya binadamu, ila matokeo yanaweza kuwa pia hayaruhusu urafiki uendelee,hapa lazima uchukue maamuzi magumu,bila hivyo itakuwa ngumu kwako kufikia ndoto zako......


Zoezi la tasmini ya matokeo ya urafiki huwa ni ngumu kidogo, maana kuna watu wanachukua maamuzzi magumu kwa kukwepa changamoto za urafiki tu ,kwa hiyo inahitaji umakini sana katika zoezi hili,,,,,,
Jiulize swali hili,....matokeo ya uchaguzi wa rafiki uliyrnaye yana endana na ndoto zako?,kama sio ,unafanya nini kwemye urafiki huo?

Habari ya kusikitisha kwenye urafiki ni kwamba,watu wengi wanaweza kugundua hawapo kwenye njia sahihi,ila wakwa wanajifariji ,mwisho wa siku wanafanya maamuzi magumu tayari walisha poteza thamani yao,,,,,,,fanya tasmini,chukua maamuzi sahihi.....

                          See you at the top
                        Scientist Saul kalivubha.
                               0652 134707

No comments:

Post a Comment