Monday, 26 October 2020

VITABU MLO KAMILI

 VITABU NI MLO KAMILI .


Habari ndugu msomaji wa blogu yetu pendwa na karibu katika safu hii ya kila wiki ya   vitabu na uchambuzi na leo tukiangazia  namna ambavyo vitabu ni chakula ambacho kina virutubisho vyote muhimu kwa afya ya mafanikio yetu , karibu. 


Usomaji wa vitabu ni utamaduni wa kawaida katika nchi za ulaya  lakini ni utamaduni mpya na usiopendwa na wengi katika nchi za Africa  licha ya kuwa uhamasishaji dhidi ya usomaji vitabu unazidi kukua Africa lakini wasomaji bado sio wengi  wa kuridhisha, leo naungana na wahamasishaji dhidi ya usomaji vitabu kukueleza kuwa maarifa ya vitabuni ni chakula cha ajabu sana, watalaam wa afya lishe wanahimiza kila siku kula chakula chenye karibu virutubisho vyote muhimu ili kuujenga mwili   na ili kupata mlo huo itakukagharimu  kuandaa menu yenye vyakula hivyo    kisha uende sokoni kununua na baadaye kuvipika na mwishoni kufurahia mlo huo  mezani .


Kwenye vitabu ni tofauti kidogo ndani ya kitabu kimoja mwandishi anakuwa kafanya maandalizi yeye kwa kufanya utafiti wa kutosha na kisha kukuwekea kwenye kitabu kimoja hivyo unapo kaa mezani na kitabu tayari upo kwenye mlo kamili wa maarifa  yaliyoandaliwa kwa weredi wa kutosha. Napoleon Hill mwandishi wa kitabu cha THINK AND GROW RICH  aliandika kitabu hicho miaka imepita  ( kabla ya vita ya pili ya Dunia)  lakini  bado ni mlo kamili mpaka sasa unajua kwa nini ni mlo kamili?  Maandalizi ya kuandika kitabu hicho yalifanyika kwa miaka isiyopungua ishirini kwa mwandishi kufanya mahojiano na watu mbali mbali waliofanikiwa ikiwemo mgunduzi maarufu wa bulbu Thomas Edson, unajisikaje kusoma kitabu kiliichoandaliwa kwa takribani miaka 25? tena kikiwa na mbinu za Thomas Edson ambaye hakukuta tamaa kwa kufanya majaribio zaidi ya 999 na kufanikiwa kwenye jaribio la 1000 .


Napoleon hill katupa mlo kamili kwenye kitabu chake aliyoandika miaka hiyo mpaka sasa ukiyasoma  bado ni chakula chenye virutubisho muhimu kwako, machache kati ya mengi ambayo mwandishi alijihakikishia kutoka kwa watu waliyofanya ni kutojipa ukomo wa uvumilivu  hili ni jambo muhimu sana miaka yote  kwa sababu tunashindwa kufikia malengo sio kwa sababu hatujui njia za kupita la hasha muda mwingine ni kwa sababu tunaishia njiani lakini njia ndiyo yenyewe, tunapata mbinu moja muhimu ya kutoichoka safari isemayo kabla hujakata tamaa jiambie nitafanya mara tano tena zaidi mfano umefanya biashara imekufa kabla ya kusema sitofanya tena biashara jiambie nitafanya tena mara tano zaidi nione matokeo. 


Kusoma vitabu ni tabia ya hekima  ya kujilisha kimaarifa  ambapo pishi linakuwa tayari limepikwa na mwandishi inabaki ni wewe kukaa mezani na kula chakula hicho chenye virutubisho vyote muhimu, mwandishi Napoleon hill katika kufanya utafiti wake wa kutuandalia mlo kamili  anatoa mbinu nyingine nzuri sana inayofanya kazi mpaka sasa nayo ni kuacha tabia ya kuaga kila mtu kabla ya kusafiri, mwandishi anasema unapotaka kuthubutu jambo jipya na ukataka ruhusa kutoka kwa watu wako wa karibu inawezekana idadi kubwa itakuonea huruma na hatimaye kukukataza usifanye kwa sababu ni hatari hivyo ukiwa na tabia ya kuaga kila mtu unaweza usiende uendapo kwani utakatazwa ni bora wengine waone matokeo ndio uwaambie uliwezaje , nenda kisha utarudi baadaye kuwaambia kuwa uliondoka . Thomas Edson aliweza kuthubutu mara elfu moja sio kwa sababu alikuwa na moyo mgumu wa kutokota tamaa kuliko watu wote Duniani la hasha pia hata tabia ya kutoaga kila mtu ilimsaidia wengi walikuja kuona tu matokeo.


Mwandishi bado akaendelea kutuonyesha kuwa vitabu ni mlo kamili kwa kutuletea mbinu zilizotumiwa na Henry Ford ( mwana mapinduzi katika ulimwengu wa magari) , mwandishi katika mahojiano na kampuni ya Ford hakuwa mchoyo kuziweka mbinu  wazi kwenye kitabu chake cha think and grow rich , moja ya mbinu aliyotuwekea ni  kufikiria kwa kuendana na nyakati kwa sababu sio mtu wa kwanza kugundua gari lakini alichokifanya ni ugunduzi wa gari kutokana na mahitaji ya jamii  na vipato vyao.Henry Ford alifariki mwaka 1947 lakini mpaka leo bado ujuzi wake na mfumo wake unatumiwa na watu mbalimbali wanaofanikiwa huoni kama vitabu ni mlo kamili? Mpaka sasa bado ukisoma kitabu cha think and grow rich unapata chakula ambacho hakijachachcha kutoka kwa mwandishi aliyetumia muda mrefu kukuandalia. 



Nyuma ya vitabu kuna maandalizi ya kutosha hadi kuja kukisoma wewe hivyo waandishi wanaingia gharama za kukutafutia viini lishe vyote muhimu na kukuwekea kwenye kitabu kimoja kazi ibaki kwako kula na kufanyia kazi, vitabu ni hazina na utajiri .


Makala hii imeandikwa Saul Kalivubha, Mwanasayansi tiba katika maabara za binadamu na mwalimu. 

0652 134707

1 comment: