Tuesday, 27 February 2024

IFIKE MUDA UJANJARUKE NA WEWE KATAA KUFANYWA FURSA ISIYO NA FAIDA KWAKO

 IFIKE MUDA UJANJARUKE NA WEWE KATAA KUFANYWA FURSA ISIYO NA FAIDA KWAKO. 


1.Unakubalije kuwa na mtu ambaye kila akikutafuta basi ana shida. 

2.Unakubalije kuhusiana na mtu ambaye bila wewe kumtafuta basi mahusiano ndio yanakufa .

3.Unakubalije kuwa na rafiki ambaye anataka umtimizie mambo yake kila anapotaka la sivyo anakuchukia 

4.Unakubalije kuwa mtu wa kuonewa hovyo hovyo?


WATU WA HOVYO WANAWEZA KUWA KIKWAZO KWAKO KUFANIKIWA. 


Kuna watu lazima ufanye tu maamuzi magumu ya kuwaepuka na hapo ndipo utagundua kuwa walikuchelewesha kwa sababu utaanza kuona matokeo chanya kwako.


Taarifa isiyopendeza ni kuwa kuna watu wamekusoma vya kutosha na wamekuona hujielewi hivyo wanakutumia kama mtatuzi wa shida zao huku wewe ukiendelea kuangamia taratibu. 


Kila siku jifunze kuhusu watu bila kusahau kuwatathimini marafiki zako ili ujue nani yupo kwako kweli na nani yupo kwako kukutumia hovyo. 


Mwanasayansi Saul kalivubha

Fikia Ndoto zako 

+255652 134707

No comments:

Post a Comment