KIJASUSI WAPE USHINDI WALEWE ILI WAACHE KUKUFUATILIA BALI WASHANGAZWE KWA MATOKEO.
Jasusi yoyote Duniani huwa habishani na mtu zaidi atakubaliana na wewe ili uvimbe kichwa lakini moyoni mwake hajakubali na kitachokushangaza ni matokeo.
Hii ni mbinu moja wapo ya kuishi na watu ambao hawataki wengine wafanikiwe kwa kujiona wao ndio wanajua kila kitu , ukisema ujionyeshe ni zaidi yao kwa maneno watakufuatilia sana ili kuzima harakati zako hivyo wewe wape ushindi tu .
Sifa kubwa ya wajuaji kama hao huwa wanapenda sana sifa na kuonekana wao ni zaidi ya yeyote na siri kubwa kuhusu watu hawa huwa wanalewa sifa yaani wakipewa sifa tu tayari wanajisahau hivyo tumia madhaifu haya kuishi nao.
Ukiwapa ushindi watakuona wewe ni bwana mdogo tu na hata siku moja hutokuwa juu sasa kipindi wanashangalia kwa kukuona hivyo wewe pambana kwani hawatakuwa na umakini kwako wakijua tu wewe ni wa kushindwa.
Wakikwambia wao ndio wa mjini na hakuna wa kuwashnda wewe wakubalie kuwa ni kweli wapo hivyo ila ki uhalisia unawaona kabisa hawana lolote ila majigambo tu na huo utakuwa muda mzuri sana kufanya vitu vikubwa bila wao kukufuatilia.
Kwanini hawakufuatilii? Kwa sababu umwapa ushindi hivyo wanajiona washindi na kukuona wa kushindwa tu, Tumia huo muda vizuri.
#Mwanasayansi Saul kalivubha
#Fikia Ndoto zako
+255652 134707
No comments:
Post a Comment