Thursday, 1 August 2024

MASKINI ATABAKI KUWA MASKINI TU KAMA ATAENDELEA KUWA NA MARAFIKI MASKINI 😔

 MASKINI ATABAKI KUWA MASKINI TU KAMA ATAENDELEA KUWA NA MARAFIKI MASKINI 😔


Hii sio makala nzuri kwa maskini ambao wameridhika na hali hiyo  hivyo kama umeridhika na umaskini basi acha kabisa kusoma ila kama upo kwenye vita ya kujikwamua kama mimi basi inawezekana ikawa makala yenye mwanzo mpya kwako. 

Ukipokea simu kutoka kwa maskini iwe ni ukoo wako au rafiki zako huko kijijini kama sio ya kukuomba pesa basi itakuwa ya majungu tu, mtaongea majungu kisha mtaagana na baada ya hapo kila mmoja atabaki anatafakari hayo majungu mpaka usiku utafika mtalala na siku itakuwa imeisha hivyo , kweli hapo umaskini utaisha?


Ajabu ni kuwa huyo aliyekupigia simu kwa zaidi ya nusu akikupa majungu siku ikitokea fursa inayohitaji mtu wa sifa yako hatokupa na siku ukijua ukamuuliza atakwambia hakuwa na salio ( vocha ) siku hiyo , Inashangaza na kuchekesha kidogo .



Umaskini ukiwa damuni huwa wahusika wanapendana wakiwa na umaskini wao ila wana wivu mkali siku wakisikia una mipango ya kutaka kuagana na umaskini.

Ukitaka kujua hilo wapelelee habari nzuri maskini rafiki zako utachopkea kwa asilimia kubwa ni kukatishwa tu tamaa kwa kupewa mifano ya watu waliokuwa kama wewe ila wanashindwa na na huo ni ujumbe kwako kuwa achana na mipango hiyo na kwa sababu unaogopa usiwapoteze marafiki zako basi unaamua kuwasikiliza na kughairi harakati zako za kuagana na umaskini. 

Waepuke maskini wa namna hiyo kwa kila hali , hili haliwezekani kwa maskini wanaopenda kuwa maskini ila ni rahisi kwa maskini ambao wapo kwenye harakati za kujikomboa ndio maana awali nilikatunguliza hii makala haiwahusu maskini walioridhika kwa umaskini wao.

KWANINI UWAEPUKE MASKINI?

Kwa sababu wengi wao ( sio wote) watakuwa wanakujaza majungu tu na sio kukupa fursa( njia za kujikwamua)  na usipokuwa makini watakufanyia kitu kibaya endapo wakijua una mipango mizuri ya kuwa tajiri.


Mwanasayansi Saul kalivubha 

Instagram @fikia ndoto zako 

+255652 134707

No comments:

Post a Comment