Monday, 12 March 2018

JINSI YA KUONGEZA THAMANI KWENYE BIDHAA YAKO.

Karibu sana kwenye blog hii inayotoa mafunzo ya maisha na jinsi ya kufikia ndoto zako,hongera kwa hali uliyo nayo,ipo sababu ya wewe kuwa ivyo.


KUSUDI LA SOMO.
Somo hili ni majibu ya watu ambao kila siku wanaogopa kufanya biashara au kuwekeza kwenye kitu ambacho tayari kinafanywa na wengine,kwa hofu ya kupata soko la kutosha.....karibu upate majibu. Kabla hujaendelea mbele,jifunze( JINSI YA KUTENGENEZA SOKO)........Karibu tuendelee.


JINSI YA KUONGEZA THAMANI KWENYE BIDHAA YAKO.

Mwaka 2016 nilifanya utafiti wenye lengo la kugundua sababu zinazofanya wanakijiji wengi waendelee kulima bila kupata mafanikio ya kutosha,utafiti huu niliufanya kwenye kijiji kimoja mkoani Morogoro,,,,,pamoja na mengi niliyoyapata,yapo mambo mambo muhimu matatu ambayo wengi wetu tunakosea hadi kufanya soko liwe changamoto kubwa.


Jitahidi uongeze thamani ya pili kwenye bidhaa yako.mfano,kama una unaona kila mtu ana duka la mbolea,wewe fanya kinyume toa ushauri wa jinsi ya kutumia hiyo mbolea......watu watakuja kupata ushauri huo,wakiridhika ,ni ngumu wakanunue mbolea sehemu nyingine tofauti na kwako.


Usiingize bidhaa yako sokoni ukiwa na shida inayohitaji utatuzi wa haraka.....utajikuta unatumia mbinu ya kuishusha thamani ya bidhaa yako kwa kuiuza kwa bei ya chini,....wanakijiji wengi huingia kwenye kilimo ili watatue matatizo yao kwa haraka,mwisho wa siku wanajikuta wanauza mazoa yao kwa bei yoyote ile,tena wanauza haraka baada tu ya kuvuna......!


Ifanye bidhaa yako kuwa adimu,unaifanya vipi?......hapa unafanya bidhaa yako iwe inapatikana kwa utaratibu ambao wengi hawaufanyi,fatilia wateja wnapata usumbufu gani hadi kuja kuipata bidhaa yako......wapunguzie usumbufu huo....mfano badala ya kuwauzia sabuni kwenye gazeti,wauzie kwenye mfuko mweusi.


Makala hii imeandikwa na Saul Kalivubha,mkurugenzi wa label ya fikia ndoto zako.

0652 134707

No comments:

Post a Comment