Saturday, 31 December 2016

ANZA KWA MAFANIKIO

Nawasalimu nikiwa nimejaa nguvu ya Mungu wetu,nina imani nyie wote ni wazima.  Moja ya vitu ambavyo wengi wetu tunatamani, ni ujuzi wa kuanza safari ili tufike salama. Leo nataka tujifunze machache ambayo yanaweza kukusaidia kuanza mwaka wako vizuri.
Mwisho mazuri, sometimes hutegemea mwanzo mzuri pia. Unaweza anza safari yako kwa kufanya hayo :

                                     WEKA MALENGO
Andika ambayo unatarajia uyafikie ndani ya muda umeojipangia, kupanga malengo sio Kazi rahisi, hakikisha mazingira ya nje hayawi kivutio cha wewe kuweka malengo, usiweke malengo sababu upo kwenye kundi ambalo ili uendano nalo lazima utimize kama walivyo wao. Jitahidi sana kesho yako iwe na asilimia nyingi za maamuzi yako.


                                        TENGENEZA MAZINGIRA KULINGANA NA MALENGO YAKO.
Kuweka malengo sahihi ni wachache wanaweza fanya, kuishi katika mazingira yenye kubeba malengo inawezekana ni 1 ya 10 wanaoweza fanya. Tambua kila malengo yana mazingira yake,huwezi kusema una malengo kuibadilisha kesho yako ikiwa rafiki tu wa karibu haijui kesho yake. ........kuishi katika mazingira yenye malengo yako ni kutangaza vita na walio kinyume na wewe. .........ndo mana sio zoezi rahisi, linahitaj ujasiri.

                                  TENGENEZA MIPAKA
Huwezi fanikiwa kama huna mipaka ambayo watu wanaifahamu.....mipaka nina maanisha uwezo wa kutoingiliwa zaidi ya kawaida. .......usipokuwa na mipaka, huwezi control ratiba zako,utakuwa unafanya ratiba za wengine, wengi watakupenda kwa urahisi wako ila mwisho wa siku utapata ugonjwa wa kulizika na kisicho sahihi.

                                        AMUA KUENDELEA.
Unaweza timiza yote hapo juu ila usifanikishe malengo yako,  huwezi kutimiza malengo yako endapo hujaamua kuendelea, kuamua kuendelea ni kuanza kufata hatua za kutimiza malengo yako. .........ukihitaji ufaulu mzuri lazima uamue kusoma kwa juhudi.

                          TASMINI MALENGO YAKO.
Swali zuri kwa mwenye malengo ya kweli ni hili. ......"kwa nini nimeweka malengo haya? "
Kuna sababu nyingi zinazofanya watu waweke malengo yao, ila sio kila sababu iliyokusukuma ipo sahihi, ni vyema kama utakuwa na muda mzuri wa kuhakiki malengo yako.


NB: Wanaofanikiwa mara nyingi ni wale wenye sifa ya uvumilivu na wenye rafiki wa kweli.
        Swali zuri jiulize. .....rafiki yako yupo tayari kuwa na wewe kwa Upendo ulele endapo utamtangulia kufanikiwa?

See you at the top
Scientist Saul kalivubha
Tembelea blog hii jumatano na jumapili kwa masomo mapya.


     

7 comments:

  1. it's real interesting brother god bless you.........keep it up

    ReplyDelete
  2. kazi yako ni njema sana,Endelea Mwandishi Mwenzangu.Mwenyezi Mungu atutangulie tufikie Malengo yetu ya Uandishi

    ReplyDelete
    Replies
    1. Amen mwana harakati marwa. Hii Kazi ni bila wewe mimi si kitu kabisa

      Delete
  3. Ujumbe mzur unagusa unaelimisha,unaonya nimepata vitu vingi mungu azid kukutia nguvu uendeleee kutupa vitu vizur na vya kujenga kama iv

    ReplyDelete