Thursday, 5 January 2017

MAAMUZI

Nimshukuru kwa kunipigania kila siku, hadi sasa nipo salama. .....ni vyema kama na wewe una utaratibu wa kumshukutu Mungu.....

KUSUDI LA SOMO. 

Leo nataka  tujifunze machache kuhusu  Maamuzi......karibu tujifunze,

                  MAAMUZI. .....

 Mwandishi :Saul kalivubha.

Maamuzi kwa mtazamo wangu huwa nasema. ....Maamuzi ni miguu,  usipofanya maamuzi huwezi piga hatua. ..
Mazingira tunayoishi yamebeba mambo mengi,...ili kupiga hatua lazima tuchague machache kati ya mengi. ...maamuzi ni kuchagua pia na ni changamoto kubwa sana kwenye mafanikio yetu. ...

                  MAMBO YA KUFAHAMU KUHUSU MAAMUZI. 
Unapofanya maamuzi, fahamu kuna hatua itafata ambayo ni utekelezaji, kabla ya utekelezaji  ni bora ukatasmini upya maamuzi yako. hii nafaida kubwa, maana mara nyingi mtu hufanya maamuzi kulingana na hali aliyonayo muda huo. .....inawezekana maamuzi yako sio halisi ila ya hali uliyokuwa nayo tu. ....je hali hiyo ikitoweka bado utaona upo kwenye maamuzi sahihi? 

Sifa kubwa ya maamuzi sahihi ni kuwa na matokeo yenye changamoto, Hapa ndipo wengi hujikuta wakibadilisha msimamo. ....Maamuzi sahihi ni chukizo kubwa kwa rafiki zako wanaotamani usitembee, changamoto zitaanzia kwa wao kupinga utekelezaji wa maamuzi yako. Kwa sababu wengi wetu hufanya maamuzi ili kufurahisha watu, tukiona rafiki zetu huchukia maamuzi yetu na sisi hubadili msimamo wetu. ......usiogope kupoteza rafiki walio kinyume na wewe,kumbuka tu bila maamuzi huwezi kupiga hatua. 

Kama una ugonjwa wa kukata tamaa hakikisha unafanya maamuzi ya kutibu ugonjwa huo kabla ya kufanya maamuzi mengine. ....almost watu wote waliokata tamaa huwa maamuzi yao ni sahihi kwao ila huwa hayana mafanikio. ......mtu aliyekata tamaa huwa na imani flani akilini mwake, hivyo imani yake ndio hutwala maamuzi yake.Imani ya mtu aliyekata tamaa ni  ni HOFU. .....ukifanya maamuzi ukiwa na hali ya hofu jiandae kupokea matokeo yenye kukatisha tamaa zaidi ya mwanzo. 


Ukishindwa kufanya maamuzi, mazingira yatafakufanyia maamuzi. ....wapo watu ambao hawajui waendapo wala watokapo. ..ni vigumu kusema jambo hili sio sahihi na huku sahihi hulijui,hivyo ukiwa kwenye hali hiyo tayari umetoa kibali cha mazingira kukufanyia maamuzi. 
Tatizo hili wanalo wengi, ili ujue kama una tatizo hilo jaribu kutasmini maamuzi unayofanya ukiwa kwenye mkusanyiko wa watu. .....jiulize hayo maamuzi ni yako au ni influence za wanaokuzunguka? ............


Watu ambao mazingira yamewafanyia maamuzi ila bado wanahisi ni maamuzi yao kuna uwezekano kuwa hawapo sehemu sahihi  (iwe  kwenye mahusiano, ndoa, biashara nk).
Jitahidi uwe makini kwenye maamuzi. 


                             See you at the top.
                      scientist Saul kalivubha.
                                  0652 134707.


10 comments:

  1. ni vyema kuhakksha ktk kila unachoamua moyo wako kwanz unaamani nacho, ndpo kitakua na matokeo chanya,, na kumbuka kua kila litokealo ktk sphere ya maisha yako,, kinahitaji ww ukitolee maamuz,, kumb kufanya maamuz hakuepukki ila hakikisha n chanya,,

    ReplyDelete
  2. thanks to adhere on my share,,

    ReplyDelete
  3. asante sana KK maana bila kuwa na maamzi ya busara MTU hawezipiga hatua

    ReplyDelete
  4. Nimeielewa hyo maana maamuzi ndo msingi wa kila kitu

    ReplyDelete
  5. Thanks brother
    Nimejifunza kitu

    ReplyDelete