Thursday, 12 January 2017

JITAMBUE 1

 Nashukuru Mungu kwa uzima wangu, bila shaka wewe pia ni mzima wa afya. Ni utamaduni mzuri sana kuwa na ibada ya kumshukuru Mungu kwa makuu yake.

KUSUDI LASOMO
.Tukiwa bado tupo kwenye safari ya maisha nimeona vyema tujifunze somo la KUJITAMBUA. Somo hili litakuwa na sehemu tatu.

   1.SIFA ZA MTU ASIYE JITAMBUA.

  2.MADHARA YA KUTOJITAMBUA.
                        3.JINSI YA KUTIBU UGONJWA WA KUTOJITAMBUA.


Kujitambua kwa maana (definition) rahisi ni kufahamu vizuri mazingira yako, ..kufahamu mazingira yako tu haitoshi, kufahamu kwa nini upo kwenye mazingira hayo ndo Kujitambua kamili.
Kuna uwezekano kuwa watu wengi wapo maeneo yasiyo sahihi kwa sababu tu hawajitambui, na wataendelea kuwa maeneo hayo sababu  ya tatizo la kutofanya TASMINI.


                         SIFA ZA MTU ASIYE JITAMBUA

Kutojitambua
ni tatizo ambalo wengi wetu tunalo,ila ukiwa hujakutana na mazingira ya kulichochea tatizo hilo ni vigumu kuona dalili zake. ......na mara nyingi mtu mwenye tatizo hilo huwa hakubali kama analo. ....

zifatazo ni baadhi ya sifa za mtu aliye na tatizo la KUTOJITAMBUA.

KUTOKUWA NA MALENGO : hii inaweza kuwa ni sifa kuu ya mtu asiye jitambua,  neno malengo kwake anakuwa analisika tu. Kumbuka tu usipokuwa na malengo huwezi kujua usahihi wa eneo ulilopo, kila jambo kwako utaona sahihi ila mazingira yakibadilika kidogo utaona sio eneo sahihi kwako.

 KUTOKUWA NA RATIBA; mtu asiye jitambua huishi kwa ratiba za watu wengine,  kama huna ratiba ya kuongoza maisha yako ni ngumu  kuwa na mipaka ya kulinda muda wako. .....kila ratiba ya nje itakuwa inafanya mabadiliko kwako...kumbuka tu watu hupenda sehemu rahisi, kila wakiwa na free time hutafuta sehemu rahisi ya kupumzikia. ...mtu asiye jitambua huwa busy kwenye free za watu wengine.


KUWA TAYARI KUACHIA ALICHO NACHO; ..Ni jambo jema mtu kufanya tasmini na kubadili mazingira  (endapo akigundua hayupo sehemu sahihi ,ila hii ni tofauti kwa mtu asiye jitambua, ..mtu huyu yupo tayari kuacha sehemu salama na kuelekea pasipo salama,  hii mara nyingi hutokana na tabia kutojiamini (tabia ya mtu asiye jitambua ).....ni vigumu kuamini kitu ulicho nacho na wakati hujui sahihi ni kipi, na ukikosa imani na ulicho nacho just muda wote utakuwa na mawazo ya kukiacha.


KUISHI KWA MAZOEA;  mtu asiye jitambua huishi kwa mazoea, muda wote yeye anakuwa anaamini kufanya mafanikio mwisho wa safari yake,  kwa kuwa amepoteza kujitambua,mtu huyu
hana sababu za kwanini yupo  pale alipo. ....swali zuri la kujiuliza siku zote ni " upo hapo ulipo kwa sababu wengine wapo or upo kwa sababu lipo kusudi la wewe kuwepo hapo ?"


KUKOSA UVUMILIVU; mtu asiye jitambua hana uvumilivu hata kidogo, hii hutokana na kutojua  umuhimu au hasara wa alicho nacho, ni vigumu kuvumilia na huku hujui kwa nini unavumilia. ......wavumilivu ni wale wanao tambua mazingira yao vizuri.


      KUTOJITAMBUA ni ugonjwa wa kuzuia mafanikio, ugonjwa huu tafasiri yake ni sawa na msafiri ambaye huchukua maamuzi ya kupanda gari bila kujua aendapo.

.......welcome again next session on next week.

                 See you at the top.
             Scientist Saul kalivubha.
                 0652 134707


3 comments:

  1. ukishayafaham mazngra hayo,, utakua na good control of that by understanding :ur needs,, feelings,, altitude,, emotion,, ur weaknesses & strengths,, kip unapenda na kip hupend,, hayo yote hutokana na kujitambua ambako ndiko kunakoleta upekee baina yetu na kujiamn kua nnachowaza na kufanya n cha tofaut,, raise ur self awareness,,

    ReplyDelete