Friday, 7 April 2017

SIRI ZA UVUMILIVU -1.

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya maisha, nashukuru Mungu kwa kuendelea kutupigania, ...karibu.
Leo nataka tujifunze somo la uvumilivu kwenye harakati zetu za kuelekea ndoto zetu.


KUSUDI LA SOMO.

somo letu la siri za uvumilivu limelenga kufundisha sehemu zifatazo. 1.maana ya uvumilivu. 2. faida za uvumilivu. 2.Hasara za kukosa uvumilivu. ..karibu kwenye sehemu ya kwanza ya somo hili.


1.MAANA YA UVUMILIVU.

Kuna watu ambao wana tumia neno uvumilivu ila hawajui maana yake, kuna watu wengine wanajua maana yake ila wanashindwa kuliishi neno uvumilivu hasa pale wanapokutana na mazingira yenye kuhitaji uvumilivu. nimetumia mifano kulifafanua neno uvumilivu, karibu tujifunze.



  • Uvumilivuni ni uwezo wa kutawala hisia zako kipindi unapopata matokeo tofauti na makusudio yako, Wanasikolojia wanazunguwa kuwa moja ya zoezi gumu ni kutawala hisia zako kipindi unapopata matokeo tofauti na makusudio yako. .....hii inasababishwa na tabia ya binadam kupenda kila kitu kifanyike ndani ya uhitaji wake. ....ila kuna mazingira ambayo lazima uweke uvumilivu , ....sio kila kitu utakipata ndani ya muda unaohitaji wewe,  ukiweza kutawala hisia zako kipindi hicho utakuwa umeliishi neno uvumilivu.



  • .Uvumilivu ni uwezo wa kutawala hisia zako kipindi watu  (rafiki zetu ) wanaposhindwa kutufanyia kama tunavyohitaji. ....maamuzi ambayo wengi tumefanya hasa pale rafiki zetu wanapofanya tofauti na tutakavyo huwa ni maamuzi yaliyokosa uvumilivu, ni maamuzi ya kubadili  (badala ya maamuzi ya kusubiri wakati mwingine )......uwezo wa kutawala hisia zako ndani ya mazingira hayo ni tafasiri ya kuliishi neno uvumilivu. .



  • .Uvumilivu ni UPENDO, kipimo cha Upendo kipo kwenye uvumilivu, ukiona umeshindwa kufanya uvumilivu wajambo flani kuna uwezekano mkubwa kuwa huna Upendo wa dhati na jambo hilo linalohitaji kuvumiliwa...



Kuliishi neno uvumilivu ni zoezi ngumu, ila matokeo ya kutoliishi neno hilo ni wengi wetu kupoteza ndoto zao. .lazima tuwe wavumilivu ili tuweze KUFIKIA NDOTO ZETU. ......jiulize swali hilI, Utabadilisha maamuzi mangapi? ..maana matokeo ya kukosa uvumilivu ni kubadili mawazo.
Tukutane wiki ijayo katika sehemu ya pili.    

                     See you at the top.
                    scientist Saul kalivubha.
                       0652 134 707.


1 comment: