MAMBO MUHIMU YA KUJIULIZA KABLA YA KUCHUKUA MKOPO
Mikopo ni mkombozi kwa watu wa tabaka zote wenye kipato kidogo na matajiri pia hivyo sio kitu kibaya bali ni sehemu ya kujikomboa kiuchumi, mikopo hutolewa na taasisi nyingi za kifedha na hata zisizo za kifedha kuna mashirika na makampuni nayo hutoa mikopo vilevile, lakini mikopo yote hiyo huwa na masharti na sharti kubwa ni riba pamoja na ukomo wa muda wa kulipa huo mkopo na kabla ya mteja kukopeshwa lazima ukidhi vigezo ikiwemo pamoja na mteja kukubaliana na masharti kwa kutia saini fomu ya maridhiano hayo .
Makazini kuna kila aina ya watu katika suala la mafanikio na maamuzi pia, kuna ambao tayari wanahatua fulani katika maendeleo na kuna ambao bado kwanza wanaanza nikimaanisha waajiriwa wapya na wengine sio waajiriwa wapya bali kipato chao sio kikubwa kiasi cha kufanya mambo makubwa ya kifedha hivyo na hapo ndipo suala la kujilinganisha na waliowatungulia kunaanza lakini kosa huja pale ambapo hamasa ya kufanya vitu vikubwa ndani ya muda mfupi inamuandama mfanyakazi na bila kufikiria mara ya pili anaamua kuchukua mkopo ulio nje ya uwezo wake.
Mfanyakazi kabla hujachukua mkopo kwanza hakikisha una ufahamu wako timamu na umejihakikishia kuwa masharti ya mkopo husika na muda husika wa ukomo wa mkopo wako umejiridhisha kuwa hakuna madhara makubwa utapata bali faida kubwa hapo sasa waweza chukua mikopo huo na isiwe una shauku ya kutaka mafanikio makubwa au ukawa umejilinganisha na wafanyakazi wenzako ukajiona uko nyuma kimafanikio sasa unataka uchukue mkopo ili ukimbizane nao kwa sababu hizo ikiwa ndio unazo basi hustahili kuchukua huo mkopo acha kabisa.
Kabla ya kuchukua mkopo utambue kuwa kuna makato mengine yanafanyika kwenya mshahara wako wa msingi hivyo mkopo utakuja kuongeza asilimia ya makato yako kama ilikuwa unakatwa asilimia kumi sasa itakuwa pengine asilimia ishirini hivyo utaweza kuishi kwa mshahara wa asilimia themanini mpaka hapo utakapomaliza kukatwa na wadeni wako?
Jambo lingine muhimu la kuzingatia ni kuwa huo mkopo unachukua kwa ajili ya kutimizia jambo fulani sasa ikiwa ungeweka akiba ungefikisha kiasi sawa na mkopo unaotoka kuuchukua kwa miaka hiyo ambayo utamaliza kuulipa? ikiwa ndio basi tambua huo mkopo uko ndani ya uwezo wako na ikiwa huoni ikiwa hivyo jitafakari upya kabla ya kuingia huo mkataba wa mkopo.
Kutokana na majukumu kuongezeka kila siku na kipato kuwa kilekile sio vibaya kufikiria mikopo kama suluhisho la kutatua uhuru wako kiuchumi hilo ni wazo zuri lakini isiwe ni kwa mihemko ukifanya kwa mihemko utajikuta kwenye matatizo na majuto ya kuulipa huo mkopo na pengine ukaingiwa na msongo wa mawazo hadi mwishowe ukaamua kujikatisha uhai wako wa thamani na wakati ikiwa ungekaa vizuri na akili yako ungepata maamuzi sahihi kabla ya kuuchukua huo mkopo.
Ikiwa ni mkopo unahitaji kwa ajili ya biashara basi jitahidi uwe na uhakika na wazo lako la biashara kwa kufanya utafiti wa kutosha kujiridhisha kabla ya uanzishaji huo na ikiwezekana usitumie pesa yote ya mkopo kwenye biashara bali anza kwa kiasi fulani kisha uende unaongeza mtaji taratibu kwa sababu mara nyingi biashara ikiwa unaanza huwa ni za majaribio chako zitakuwa nyingi sana na inaweza kufa na kuanza tena upya hivyo lazima ujihami katika hilo pia
Mwanasayansi Saul Kalivubha
+255652 134707
No comments:
Post a Comment