Sunday, 1 January 2023

KUNA TOFAUTI KATI YA MTU MASKINI NA MTU AMBAYE HANA PESA 

 KUNA TOFAUTI KATI YA MTU MASKINI NA MTU AMBAYE HANA PESA 

Na Mwanasayansi Saul Kalivubha ✍ 

Mtu anaweza kuwa hana kabisa pesa hata shilingi mia lakini asiwe MASKINI na mtu anaweza kuwa anakula tu vizuri na kila kitu cha ndani lakini akawa MASKINI 😔  Mwanasayansi kakuchanganya? 😄 🤣 

Hapana nipo sahihi ✍ 

Umaskini ni IMANI lakini kukosa pesa ni MAPITO , Unaweza pitia kipindi cha kukosa pesa lakini imani yako ni ya KITAJIRI 

Umaskini ni imani kama zilivyo imani nyingine tu za kiroho mfano uislam na Ukristo ulivyo na waumini ndivyo ilivyo hata kwenye Umaskini kuna waumini wake wamo humo ndio maana sio kazi rahisi kuaga Umaskini, narudia tena sio kazi rahisi kuaga Umaskini kama ilivyo ngumu kumbadilisha muislamu kuwa mkristo  au kinyume chake, unajua sababu? Ni kwa sababu tu kila muumini ameshika mizizi ya dini yake hivyo sio rahisi kuiachia kirahisi. 

Umaskini huanzia kwenye akili ya mtu ndio maana watu maskini huwa wana viashiria vya kufanana kwa sababu tu wapo imani moja, je wajua viashiria? ( Dalili za umaskini)


#Ni watu wa visingizio

#Ni watu wa kuridhika na maisha ya kujaza tumbo tu

#Huamini kuwa wanaoshindwa wametoa rushwa au ni wenye imani za kishirikina 

#Kila jambo wanasema ni mpango wa Mungu hata ambalo  ni matokeo ya uzembe wao

Hizo ni dalili chache kati ya nyingi za muumini wa UMASKINI yawezekana unazo chache au zote kati ya hizo basi jijue wewe ni muumini wa UMASKINI tayari 😔 

Unaweza kutoka humo? Ndio inawezekana kutoka humo japo sio rahisi kama nilivyokwisha kusema kuwa sio rahisi kubadili imani 😔 nguvu kubwa inatakiwa 

Lazima kwanza ukubali kuwa wewe ni maskini upo kwenye imani hiyo sasa unatakiwa kuanza taratibu kuzikana imani hizo za kimaskini ili uhame kutoka imani hiyo uende kwenye imani ya UTAJIRI 

UTAJIRI ni imani pia yenye waumini wachache lakini na misingi ya imani yao ipo kinyume na misingi ya umaskini hivyo ni rahisi tu kuwa humo kama tu utaikana misingi ya umaskini 


Nikutakie mwaka mpya mwema ndugu yangu 


+255652 134707

No comments:

Post a Comment