Wednesday, 31 May 2017

SIRI YA NNE YA URAFIKI

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa mafunzo ya elimu ya maisha kwa lengo la kufikia ndoto zetu,nashukuru mungu kwa kuendelea kunipigania mimi pamoja na wewe...........karibu.


KUSUDI LA SOMO.
Lengo la somo letu la leo ni kujifunza siri ya nne ya urafiki ambayo ni uvumilivu,ili tuwe pamoja jifunze kwanza SIRI YA TATU kwa kubofya hapa.SIRI YA TATU,..........ikumbukwe tu rafiki ana sehemu kubwa sana kwenye ndoto zetu,hii ndio sababu ya mimi kufundisha somo hili.

SIRI YA NNE YA URAFIKI(UVUMILIVU).
Uvumilivu ni uwezo wa kuzitawala hisia zitokanazo na mambo yasiyo pendeza,hisia ambazo zikiruhusiwa zinaweza kuwa hanzo cha matokeo hasi(negatives effects).........kwenye urafiki pia kuna mambo ambayo yanahitaji kuvumiliwa,ndani ya urafiki kuna mambo yasiyopendeza yenye lengo la kuimarisha urafiki,mtu usipo kuwa mvumilivu unaweza kuwapotezamarafiki wengi sana wasio na hatia..............

Uvumilivu katika urafiki unahitajika sana hasa kwenye hali kuu mbili zifatazo:



  • MADHAIFU;watu wengi wanaingia kwenye urafiki wakiwa na picha ya madhaifu machache waliyo yaona kabla ya kuanza urafiki,ila kuna madhaifu mengine ya ndani ambayo huwezi kuyaona hadi uingie kwenye urafiki,......usipokuwa mvumilivu ,madhaifu haya ya ndani yana nguvu kubwa ya kuvunja urafiki.

  • CHANGAMOTO:Changamoto ni moja ya sehemu muhimu sana ya urafiki,ni sehemu ambayo inahitaji uvumilivu wa hali ya juu,pia ni sehemu ambayo inahitaji matumizi ya hekima na busara,maanakila changamoto ina jambo la kufundisha kwenye urafiki wako.....kuna usemi mmoja unasema "Kama upo kwenye urafiki usio na changamoto yoyote ile,kaa chini ufikirie tena mara ya pili"

              See you at the top.
          Scientist Saul kalivubha.
                (0652 134707)

Wednesday, 24 May 2017

SIRI YA TATU YA URAFIKI.

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya mafunzo ya maisha, ....nashukuru Mungu kwa kuendelea kutupigania hadi sasa.......karibu.

KUSUDI LA SOMO. 
Lengo la somo letu hili la leo ni kuendelea kujifunza siri za urafiki, na leo tupo kwenye siri ya tatu ambayo ni kujiamini.......karibu tujifunze. ..jifunze siri ya pili kwanza siri ya pili ya urafiki

               SIRI YA TATU YA URAFIKI.
Kujiamini ni hali ya kujiona mkamilifu..kujiona upo kwenye mazingira sahihi ya kufanya jambo flani, ....kinyume chake ni kutojiamini ..kujiona mwenye mapungufu au kujiona huna vigezo vinavyotakiwa......ina madhara gani kwenye urafiki? ......sina tatizo na mtu anayejiamini. ..ila kwa asiye jiamini karibu tujifunze. ........

Mtu asiye jiamini kwenye urafiki anakuwa muda wote anahisi kuachwa au kumpoteza rafiki yake. ...hali hii ina madhara gani? 
Hali ya kutojiamini inasababisha mtu atumie nguvu kubwa kuendesha urafiki, kutumia nguvu kubwa ni pamoja na kutumia sifa ya ziada. ..

Mtu asiye jiamini lazima atafute sifa ya kujiongezea ili aweze kujiona mkamilifu. ....hivyo urafiki wake unakuwa umejengeka ndani ya sifa yake ya ziada na sio uhalisia wake. ...

Wanasikolojia wanashauri kwamba, ukiona una tatizo la kutojiamini ni bora ukalitatatua kwanza kabla ya kuingia kwenye urafiki. .mbali na hivyo utasumbuka sana. ...
         
             See you at the top. 
           scientist Saul kalivubha. 
            (0652 134 707 )




Thursday, 18 May 2017

SIRI YA PILI YA URAFIKI


karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya mafunzo ya maisha. ...nashukuru Mungu kwa neema yake kwangu. .........karibu tujifunze.

Kusudi la somo.
Lengo la somo letu hili ni kujifunza siri ya pili ya urafiki. ....Nimeona vyema kufundisha somo hili kwa sababu najua urafiki una sehemu kubwa sana kwenye mafanikio yetu. ....karibu.

SIRI YA PILI YA URAFIKI. 
Tuangalie siri ya pili ya urafiki. ..unaweza kujifunza siri ya kwanza ya urafiki kwa kuandika kalivubha blog siri ya kwanza ya urafiki. ....kisha ndio uendelee na mimi kwenye somo hili.
(siri yakwanzayaurafiki )...

Siri ya pili ya urafiki ni hii USIFANYE URAFIKI KWA MAJARABIO...........

Moja ya sababu inayofanya urafiki upungue thamani ni kubadilika kwa mazingira ambayo yalitumika kutengeneza urafiki. ...kwa nini mazingira yabadilike? ......kuna watu ambao wana tabia ya kufanya majarabio ya urafiki. ...wengi wao hufanya hivyo ili kuangalia kama urafiki huo una weza kutimiza mahitaji yake. .....

Urafiki wa aina yoyote ile una changamoto zake. ...hivyo mtu anayeingia kwenye urafiki kwa majarabio hawezi kuvumilia changamoto. .....mara nyingi watu wanaingia kwenye urafiki kwa majarabio wana sifa kuu tatu.

1.Sio wavumilivu wa changamoto.

2.muda wote wanawaza kubadili marafiki.

3.Wanatumia nguvu kubwa kuanzisha urafiki. ....hufanya hivi kwa sababu wanakuwa wanataka waone kama watatimiza malengo yao ..kama hapana basi wabadili marafiki  ...........
Jiandae kupata kitabu cha SIRI ZA URAFIKI  .
     
                      See You At The Top.
                        Saul kalivubha.
                         (065123707 )



Monday, 15 May 2017

SIRI YA KWANZA YA URAFIKI.

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya mafunzo ya maisha, nashukuru Mungu kwa kuendelea kutupigania hadi sasa ......karibu.

Kusudi la somo.
Leo nataka tujifunze siri moja ya urafiki ambayo wengi hawajui, au wanaijua lakini hawaitumii. ....mwalimu wangu aliwahi kuniambia kwamba, ikiwa una ujuzi usio kusaidia, ...huna cha kujivunia. ....karibu tuendelee.

         SIRI YA KWANZA YA URAFIKI(SIFA YA ZIADA ).

Kwa nini urafiki? ..... utafiti unaonyesha mafanikio yetu yapo ndani ya rafiki zetu wa karibu. ...hii ndio sababu ya mimi kuandika somo hili. .....Siri ya kwanza ni ipi?
Siri ya kwanza kwenye urafiki ni ...sifa ya ziada .....

Sifa ya ziada ni ni sifa ambayo mtu anajiongezea kwa lengo la kumvutia rafiki yake. ..  hali hutokea mwanzoni mwa urafiki, .....nini madhara yake?

Kuna watu wapo kwenye urafiki mzuri, ila urafiki huo unaendeshwa na sifa ya ziada ambayo mmoja katika urafiki huo anaitumia. .Mtu ambaye anaitumia sifa ya ziada kuendesha urafiki, anatumia nguvu kubwa sana. ...tena nguvu anayoitumia ina mrudisha sana nyuma kimafanikio na ina mpa madhara ya kisaikolojia. ......!

Je, una uwezo wa kuyaishi maisha yaliyobebwa na sifa ya ziada?

Kila siku tunashuhudia kuvunjika kwa urafiki ambapo sababu kubwa ni mmoja wapo kwenye urafiki kupoteza sifa ya ziada aliyojipatia. ...
Tiba pekee kabla ya kuwa na rafiki, hakikisha unaishi maisha yako. ....be you, be smart. (ishi maisha yako, kuwa nadhifu )....utapata rafiki aina yako.

                See you at the top.
         scientist Saul kalivubha.
            (0652 134 707 )



Friday, 5 May 2017

KUTOJIAMINI NI SUMU YA MAFANIKIO

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya mafunzo ya maisha kwa lengo la kufikia ndoto zetu. ...Leo tuna somo mpya la madhara ya kutojiamini katika kufikia ndoto zetu. ..karibu.

kusudi  la somo.
Lengo la somo letu hili ni kujifunza jinsi gani hali ya kutojiamini inaweza kuzuia ndoto zako za mafanikio. .... Somo letu limelenga hasa sehemu ya .Maana ya kutojiamini. Ukielewa vizuri maana ya kutojiamini,utajitambua upo upande upi,na mafanikio kwako yapo kwa asilimia ngapi,nimejitahidi kufafanua maana ya kutojiamini na uhusiano wake kwenye mafanikio.....karibu.

        MAANA YA KUTOJIAMINI.
Kunarafiki yangu mmoja aliwahi kuniambia kuwa ukoo wao sio wa biashara hivyo hata akianzisha biashara hatafanikiwa. .je ni sahihi?
Mtu mwingine alisema .." Hata asome vipi hawezi kufaulu kwa ufaulu wa kiwango cha daraja A (grade A)"...umewahi kujiona ukiwa kwenye hali ya kushindwa? .....Nini maana ya KUTOJIAMINI..?


Kutojiamini ni hali ya mtu kujiona mwenye mapungufu, hali hiyo humfanya mtu huyo kuona watu wengine wana uwezo wa juu kuliko yeye. ........Nini maana yake? Tujaribu kuangalia ufafanuzi wa hali ya kutojiamini kupitia maelezohaya hapa chinI. ..

1.Wanasikolojia wana zungumzia hali ya kutojiamini kama vita anayokuwa nayo mtu dhidi ya watu wengine ambaoanaamini kuwa wana uwezo dhidi ya kile anachofanya /anachotaka kukifanya. ...Upo katika hali hiyo?
Kuwa katika vita na watu wasiotambua kama unapambana nao ndio chanzo cha mtu kupunguza kujiaminI. ..maana hali hiyo humfanya mtu ajione yupo upande wa kushindwa muda wote.

2. kutojiamini inaweza kuwa pia hali ambayo mtu anajiona mwenye kuhitaji sifa flani ili akubalike kwenye jamii. ....Hali hii humfanya mtu huyo kujiongezea sifa ya ziada ili akidhi hisia zake, ...hapa ndipo watu wasiojamini huanza kutumia nguvu kubwa kupamba sifa kivuli ili tu aondokane  na hali ya kujiona mwenye mapungufu. ..je unaweza kuitunza sifa uliyojiongezea muda wote wa maisha?

3.Kutojiamini  inaweza pia  kuwa hali ya mtu kuamini zaidi matokeo ambayo yametokana na Kazi za watu wengine....kwa hiyo muda wote mtu asiyejiamini...anakuwa anaishi maisha ya watu wengine ambao mtu huyo anakuwa amewapa uwezo wa ushindi. .. hali hii humfanya mtu asiyejiamini asijaribu jambo lolote lile kwa kutumia mawazo yako. ....je unaweza kufikia ndoto zako kwa kuishi maisha yakutegemea juhudi za watu wengine?
.

Kutojiamini ni tatizo ambalo linatajwa kama chanzo kikubwa cha wivu ambao umepelekea mahusiano mengi ya mapenzi kufa,kama sio mapenzi kufa basi itamfanya mtu asiye jiamini kuwa mtumwa wa mapenzi.


Kutojiamini kwa ujumla ni hali ambayo ukiwa inayo itakufanya uwe unaishi maisha ya watu wengine,maana utakuwa unajiona mwenye mapungufu muda wote,.......unajua tatizo la kujiona mwenye mapungufu muda wote?..Tatizo lake kubwa ni kushindwa kujaribu,mana kulingana na mapungufu unayohisi ni mengi kwako ,utajenga imani ya kukosea kwa kila jambo linalokuhitaji kujaribu,na kumbuka tu ni ngumu kufanikiwa kama una hofu ya kujaribu.
....
                 
              See you at the top.
            scientist Saul kalivubha.
              0652 134707.
         
                 




Wednesday, 26 April 2017

KUANGUKA KWA MTU ALIYEFANIKIWA

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya maisha, ni imani yangu kuwa  Mungu anaendelea kukupigania. ...karibu tujifunze.

 KUSUDI LA SOMO. 
Leo nataka tujifunze somo la kuanguka kwa mtu aliyefanikiwa, unaweza kuhisi tofauti kidogo kwa kuona somo hili kwenye blog hii. ..ila ni hali ambayo wewe pia unaweza kuwa shahidi kwa kuona baadhi ya watu wakipoteza mafanikio yao makubwa....kwa hiyo nataka tuangalie baadhi ya sababu zinazofanya watu wapoteze mafanikio yao, kwa kujua sababu hizo itakuwa msaada kwetu kulinda mafanikio yetu. 
Zipo sababu nyingi ila leo nataka tuangalie sababu kuu tatu......karibu. 

SABABU ZA KUANGUKA KWA MTU ALIYEFANIKIWA.
1.Marafiki wapya;siku zote mtu aliyefanikiwa huwa anakuwa
 tofauti na wengine, mafanikio yake yanavuta watu wengi kuwa karibu yake, watu hao ni pamoja na wale ambao waliona kuwa hawezi kipindi alipoanza safari ya mafanikio. .....hiki ni kipindi kigumu sana kwa mtu aliyefanikiwa, ni kipindi kigumu kwake kwa sababu ya ugumu wa kutambua nani rafiki wa kweli kwake, ....  mafanikio yake hupotea pale atapoanza kushirikiana na rafiki wanaoshangalia mafanikio yake na kusahau rafiki waliomfaraji kwenye shida. ..siku zote rafiki anayeshagalia mafanikio yako huwa sio rafiki mzuri, maana kufata mafanikio yako na sio uhalisia wako
2.Kulewa sifa;  sifa ni sehemu ya lazima kwamafanikio yako. .tatizo sio kusifiwa, tatizo ni kuzitawala hisia za furaha itokanayo na sifa. ....Wanasikolojia tunaamini kuwa tabia nyingi zitokanazo na sifa huwa ni za uharibifu na majivuno. ..mtu aliyefanikiwa akianza kuziishi tabia zitokanazo na kusifiwa anakuwa kwenye wakati mgumu sana wa kusahau alipotoka na kubadili njia ya kumpeleka aendapo. ...hatari yake ni kupoteza mafanikio yake. 

3.Kukosa maandalizi kabla; Kuna watu wanafanikiwa bila kujiandaa kuyaishi maisha ya mafanikio, ..maisha ya mafanikio yana changamoto zake,  mtu aliyefanikiwa kuipitia. .lazima watu wasifie tena kubwa sana. ..ni muhimu mtu ukafahamu wapi unaelekea, na nini utakibeba, kutambua hilo itakusaidia kuwa makini na mambo ambayo yapo nje ya kuendeza mafanikio yako. ..kinyume chake ni kupoteza mafanikio.

Kufikia ndoto zako sio kushinda, ushindi ni kuendeza mafanikio yako. ..
Tukutane wiki ijayo. 
                       
                  See you at the top. 
                  scientist Saul kalivubha. 
                    0652 134707. 
      

Friday, 21 April 2017

SIRI ZA UVUMILIVU -3

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya maisha, ...nashukuru Mungu kwa uzima wangu na wako pia. Karibu kwenye sehemu hii ya tatu na mwisho wa somo letu la siri za uvumilivu....karibu tuendelee.

KUSUDI LA SOMO.
 lengo la somo letu hili ni kujifunza siri zilizopo kwenye uvumilivu, na somo letu lina sehemu tatu. 1.maana ya uvumilivu. 2. faida za uvumilivu. 3.hasara za kukosa uvumilivu. ..Leo nataka tujifunze hasara zipi zinaweza kutokana na ukosefu wa uvumilivu. ...Kabla ya kuendelea ingia Google search na kuandika kalivubha blog siri za uvumilivu. ..hiyo itakusaidia kuendana na sehemu hii ya mwisho.

3.HASARA ZA KUKOSA UVUMILIVU .

Mambo karibia yote yenye matokeo mazuri yanahitaji uvumilivu ili kuweza kufanikiwa kupata matokeo hayo mazuri. .....nataka tujifunze hasara za uvumilivu kwenye sehemu hizi tatu. .mahusiano ,biashara na mafanikio kwa ujumla. .....karibu tuendelee. 

MAHUSIANO; Rafiki yangu mmoja aliwahi kuniambia kuwa anahisi kuwa anabahati mbaya, kwani huwa hadumu kwenye mahusiano. ..utafiti unadhibitisha kuwa watu wengi wameacha watu sahihi sababu tu ya kukosa uvumilivu, ..Mahusiano yana changamoto zake, na hii hutokana na mahusiano kuhusisha watu wenye asili tofauti....kumbe kuna mazingira yatahitaji uvumilivu dhidi ya madhaifu, uvumilivu dhidi ya mabadiliko ya hisia ambayo yanaweza kuwa chanzo cha maamuzi mabovu.

BIASHARA. Kosa ambalo wengi tunalifanya kwenye biashara ni kutengeneza imani ya kupata mafanikio ya haraka. ...Hili ni kosa kwa sababu biashara karibu zote zinahitaji muda wa kutosha ili kutoa faida kamili, huo muda wa kutosha unahitaji mtu mvumilivu, ...pia kwenye biashara kuna hasara, na mara nyingine kuna kuanza upya, yote hayo yanahitaji uvumilivu wa kutosha. .ukikosa uvumilivu ni ngumu kufanikiwa katika biashara...

MAFANIKIO KWA UJUMLA; kufanikiwa kwa ujumla ni kuwa kwenye hatua ambayo ni matokeo ya kushinda maumivu ya UVUMILIVU. ...Msanii wa filamu maarufu kwa jina la Sylivester Stalone Rambo aliwahi kusema alijaribu zaidi ya mara 70 na kushindwa mara zote, ila kilicho msaidia ni uvumilivu wake, hadi sasa ni muigizaji maarufu dunianI. inahitaji uvumilivu wa hali ya juu katika safari yetu ya KUFIKIA NDOTO ZETU. ...Ukikosa uvumilivu ni ngumu kufanikiwa kwa jambo lolote lile. ....jiulize ni maamuzi gani uliyafanya kwa kukosa uvumilivu? 
 Karibu wiki ijayo.

            See you at the top. 
scientist Saul kalivubha 
                0652 134707.