Sunday, 25 June 2017

SIRI YA SABA YA URAFIKI

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya mafunzo maisha na jinsi ya kufikia ndoto zetu,nashukuru Mungu kwa kuendelea kutupigania hadi sasa ,hongera sana kwa kuwa na afya njema,kwa wale wagonjwa poleni sana ila Mungu niwetu sote.

KUSUDI LA SOMO.
Leo nataka tuendelee na somo letu la urafiki,kabla ya kuendelea na siri ya saba, jifunze kwanza     ( SIRI YA SITA),Kisha tuendelee na siri ya saba ya urafiki ambayo ni tasmini ya uchaguzi wa rafiki,.....karibu tujifunze.

SIRI YA SABA YA URAFIKI(TASMINI YA UCHAGUZI).

Kuwa na rafiki flani ni ni matokeo ya uchaguzi uliofanya,hakuna kulazimisha kwenye mambo ya urafiki,huwa ni hiari ya muhusika,je uchaguzi wako una matokeo gani?

Kila uchaguzi lazima uwe na matokeo,matokeo ya uchaguzi ndio sehemu ambayo tunaitumia kupima kufanya evaluation(tasmini) ya usahihi wa mtu katika uchaguzi wake,....hii ni sehemu ambayo kila mtu anapaswa kuifanya yeye binafsi, je nini kinafata baada ya tasmini ya matokeo?

Matokeo ya uchaguzi wa rafiki yana sehemu ya kuvumilikika ambayo ni moja ya madhaifu ya binadamu, ila matokeo yanaweza kuwa pia hayaruhusu urafiki uendelee,hapa lazima uchukue maamuzi magumu,bila hivyo itakuwa ngumu kwako kufikia ndoto zako......


Zoezi la tasmini ya matokeo ya urafiki huwa ni ngumu kidogo, maana kuna watu wanachukua maamuzzi magumu kwa kukwepa changamoto za urafiki tu ,kwa hiyo inahitaji umakini sana katika zoezi hili,,,,,,
Jiulize swali hili,....matokeo ya uchaguzi wa rafiki uliyrnaye yana endana na ndoto zako?,kama sio ,unafanya nini kwemye urafiki huo?

Habari ya kusikitisha kwenye urafiki ni kwamba,watu wengi wanaweza kugundua hawapo kwenye njia sahihi,ila wakwa wanajifariji ,mwisho wa siku wanafanya maamuzi magumu tayari walisha poteza thamani yao,,,,,,,fanya tasmini,chukua maamuzi sahihi.....

                          See you at the top
                        Scientist Saul kalivubha.
                               0652 134707

Sunday, 18 June 2017

SIRI YA SITA YA URAFIKI

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya mafunzo ya maisha,nashukuru Mungu kwa kuendelea kutupigania,maana nina imani kuwa na wewe ni mzima,.....karibu tujifunze.

Kusudi la somo.

Leo ni muendelezo wa siri za urafiki,tunaendelea na siri ya sita ya urafiki ambayo ni utatuzi wa migogoro,kabla ya kuendelea mbele ni vyema ukajifunza kwanza  SIRI YA TANO ,Karibu tujifunze.

UTATUZI WA MIGOGORO YA URAFIKI.

Jambo la kufahamu kwenye urafiki ni kwamba ,unakutana na mtu ambaye hujazaliwa naye,ana madhaifu yake na pengine ana historia yake ya maisha tofauti na yako.......lazima kuna migogoro itatokea tu ndani ya urafiki,,,,,jaribu kujibu maswali haya kabla ya kuendelea mbele......je umewahi kuingia kwenye mgogoro na rafiki zako?,ulifanya maamuzi gani ?.baada ya maamuzi hayo urafiki wenu ulipata sura gani?

Migogoro kwenye urafiki ni muhimu sana kwani ni dalili ya kuonyeha hali ya kutokuwa sawa sehemu flani,ila inaweza kuwa na madhara ya kudumu kwa wahusika endapo watashindwa kutambua sababu za utokeaji wa migogo hiyo,

Uwezo wa utatuzi wa migogoro ya urafiki bila kuharibu thamani ya muhusika ndio kipimo kizuri cha uwezo wa uendeshaji wa urafiki.


Mambo muhimu ya kuzingatia kwenye utatuzi wa migogoro.
  1. Kabla ya maamuzi yoyote hakikisha unajua chanzo cha tatizo .
  2. Usipende kuonekana mshindi,ili kumudu hili hakikisha unatawala hisia zako za hasira ili usifanye maamuzi yenye msingi wa hasira.
  3. Kama kosa lipo kwa rafiki yako,vaa uhusika ili upime yeye angefanya maamuzi gani juu yako.
  4. Usipende kutumia ushauri wa watu wengine katika kutatua mgogoro unaokuhusu wewe.
  5. Hakikisha unajua tafasiri ya kila changamoto kwenye urafiki wako,ili ufanye maamuzi ambayo hayana majuto.


Kumbuka tu ili uweze kufikia ndoto zako ni muhimu uwe kwenye system ya marafiki waliobeba kusudi lako,ila kuwa na rafiki ambaye kabeba kusudi lako sio tafasiri ya kutokuwa na migogoro.

                   See you at the top.
     scientist SAUL KALIVUBHA.
                   0652 134 707.

Sunday, 11 June 2017

SIRI YA TANO YA URAFIKI

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya maisha, nashukuru Mungu kwa afya yangu pamoja na wewe. ....karibu.

  KUSUDI LA SOMO.
Lengo la somo la leo ni kuendelea na sehemu ya tano ya siri ya Urafiki. ..ni vyema ukajifunza sehemu ya nne SIRI YA NNE  kisha uendelee na siri ya tano( SIRI YA NNE)..... lengo la kufundisha urafiki ni kutaka tufahamu jinsi ya kuishi na marafiki kwa lengo la kufikia ndoto zetu ...maana mafanikio yako yapo kwa rafiki yako. ...karibu.

SIRI YA TANO YA URAFIKI.
Siri ya tano ya urafiki ni  mawasiliano .Kwenye mawasiliano tuangalie kwenye upande mmoja tu. jinsi mawasiliano yanavyoweza kuvunja urafiki. ....nafikiri utakuwa tayari umeshuhudia urafiki ukivunjika kwa sababu ya mawasiliano. ....au inaweza kuwa umekutwa na tatizo hili la kupoteza marafiki kwa kigezo cha mawasiliano. ....
Mawasiliano yanaweza kavunja urafiki kupitia sehemu hizi.

  • Mawasiliano mabovu, ..hapa nina maanisha kiwango cha chini cha mawasiliano au mawasiliano ambayo hayana hisia za Upendo. ....kila mazingira yana aina yake ya mawasiliano na kiwango chake, ukiwa kwenye mazingira yenye kuhitaji mawasiliano kwa wingi ila wewe ukafanya chini ya kiwango , urafiki utakuwa unaelekea kwenye hatari ya kuvunjika. ....jitahidiutambue aina ya urafiki uliyonayo, mazingira mliyopo. .ili ufanye mawasiliano yanayostahili. 
  • Mawasiliano hupoteza thamani ya habari, ...utafiti wa kisaikolojia unaonyesha kwamba habari inavyozidi kupita mikononi kwa watu wengi ndio inavyozidi kupungua uhalisia wake, ila kuna watu bila kufanya utafiti wa kina wamekuwa wakifanya maamuzi ya kudumu kwa kupitia taarifa imeyopitia mikononi kwa watu wengi. ..hali hii imefanya watu wengi kupoteza marafiki .....fanya tasmini kabla ya maamuzi, unavyozidi kuwa mbali na chanzo cha habari ndivyo ukweli wa taarifa unavyozidi kupungua. .....
             Seeyou at the top. 
        scientist Saul kalivubha. 
          (0652 134 707)






Wednesday, 31 May 2017

SIRI YA NNE YA URAFIKI

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa mafunzo ya elimu ya maisha kwa lengo la kufikia ndoto zetu,nashukuru mungu kwa kuendelea kunipigania mimi pamoja na wewe...........karibu.


KUSUDI LA SOMO.
Lengo la somo letu la leo ni kujifunza siri ya nne ya urafiki ambayo ni uvumilivu,ili tuwe pamoja jifunze kwanza SIRI YA TATU kwa kubofya hapa.SIRI YA TATU,..........ikumbukwe tu rafiki ana sehemu kubwa sana kwenye ndoto zetu,hii ndio sababu ya mimi kufundisha somo hili.

SIRI YA NNE YA URAFIKI(UVUMILIVU).
Uvumilivu ni uwezo wa kuzitawala hisia zitokanazo na mambo yasiyo pendeza,hisia ambazo zikiruhusiwa zinaweza kuwa hanzo cha matokeo hasi(negatives effects).........kwenye urafiki pia kuna mambo ambayo yanahitaji kuvumiliwa,ndani ya urafiki kuna mambo yasiyopendeza yenye lengo la kuimarisha urafiki,mtu usipo kuwa mvumilivu unaweza kuwapotezamarafiki wengi sana wasio na hatia..............

Uvumilivu katika urafiki unahitajika sana hasa kwenye hali kuu mbili zifatazo:



  • MADHAIFU;watu wengi wanaingia kwenye urafiki wakiwa na picha ya madhaifu machache waliyo yaona kabla ya kuanza urafiki,ila kuna madhaifu mengine ya ndani ambayo huwezi kuyaona hadi uingie kwenye urafiki,......usipokuwa mvumilivu ,madhaifu haya ya ndani yana nguvu kubwa ya kuvunja urafiki.

  • CHANGAMOTO:Changamoto ni moja ya sehemu muhimu sana ya urafiki,ni sehemu ambayo inahitaji uvumilivu wa hali ya juu,pia ni sehemu ambayo inahitaji matumizi ya hekima na busara,maanakila changamoto ina jambo la kufundisha kwenye urafiki wako.....kuna usemi mmoja unasema "Kama upo kwenye urafiki usio na changamoto yoyote ile,kaa chini ufikirie tena mara ya pili"

              See you at the top.
          Scientist Saul kalivubha.
                (0652 134707)

Wednesday, 24 May 2017

SIRI YA TATU YA URAFIKI.

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya mafunzo ya maisha, ....nashukuru Mungu kwa kuendelea kutupigania hadi sasa.......karibu.

KUSUDI LA SOMO. 
Lengo la somo letu hili la leo ni kuendelea kujifunza siri za urafiki, na leo tupo kwenye siri ya tatu ambayo ni kujiamini.......karibu tujifunze. ..jifunze siri ya pili kwanza siri ya pili ya urafiki

               SIRI YA TATU YA URAFIKI.
Kujiamini ni hali ya kujiona mkamilifu..kujiona upo kwenye mazingira sahihi ya kufanya jambo flani, ....kinyume chake ni kutojiamini ..kujiona mwenye mapungufu au kujiona huna vigezo vinavyotakiwa......ina madhara gani kwenye urafiki? ......sina tatizo na mtu anayejiamini. ..ila kwa asiye jiamini karibu tujifunze. ........

Mtu asiye jiamini kwenye urafiki anakuwa muda wote anahisi kuachwa au kumpoteza rafiki yake. ...hali hii ina madhara gani? 
Hali ya kutojiamini inasababisha mtu atumie nguvu kubwa kuendesha urafiki, kutumia nguvu kubwa ni pamoja na kutumia sifa ya ziada. ..

Mtu asiye jiamini lazima atafute sifa ya kujiongezea ili aweze kujiona mkamilifu. ....hivyo urafiki wake unakuwa umejengeka ndani ya sifa yake ya ziada na sio uhalisia wake. ...

Wanasikolojia wanashauri kwamba, ukiona una tatizo la kutojiamini ni bora ukalitatatua kwanza kabla ya kuingia kwenye urafiki. .mbali na hivyo utasumbuka sana. ...
         
             See you at the top. 
           scientist Saul kalivubha. 
            (0652 134 707 )




Thursday, 18 May 2017

SIRI YA PILI YA URAFIKI


karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya mafunzo ya maisha. ...nashukuru Mungu kwa neema yake kwangu. .........karibu tujifunze.

Kusudi la somo.
Lengo la somo letu hili ni kujifunza siri ya pili ya urafiki. ....Nimeona vyema kufundisha somo hili kwa sababu najua urafiki una sehemu kubwa sana kwenye mafanikio yetu. ....karibu.

SIRI YA PILI YA URAFIKI. 
Tuangalie siri ya pili ya urafiki. ..unaweza kujifunza siri ya kwanza ya urafiki kwa kuandika kalivubha blog siri ya kwanza ya urafiki. ....kisha ndio uendelee na mimi kwenye somo hili.
(siri yakwanzayaurafiki )...

Siri ya pili ya urafiki ni hii USIFANYE URAFIKI KWA MAJARABIO...........

Moja ya sababu inayofanya urafiki upungue thamani ni kubadilika kwa mazingira ambayo yalitumika kutengeneza urafiki. ...kwa nini mazingira yabadilike? ......kuna watu ambao wana tabia ya kufanya majarabio ya urafiki. ...wengi wao hufanya hivyo ili kuangalia kama urafiki huo una weza kutimiza mahitaji yake. .....

Urafiki wa aina yoyote ile una changamoto zake. ...hivyo mtu anayeingia kwenye urafiki kwa majarabio hawezi kuvumilia changamoto. .....mara nyingi watu wanaingia kwenye urafiki kwa majarabio wana sifa kuu tatu.

1.Sio wavumilivu wa changamoto.

2.muda wote wanawaza kubadili marafiki.

3.Wanatumia nguvu kubwa kuanzisha urafiki. ....hufanya hivi kwa sababu wanakuwa wanataka waone kama watatimiza malengo yao ..kama hapana basi wabadili marafiki  ...........
Jiandae kupata kitabu cha SIRI ZA URAFIKI  .
     
                      See You At The Top.
                        Saul kalivubha.
                         (065123707 )



Monday, 15 May 2017

SIRI YA KWANZA YA URAFIKI.

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya mafunzo ya maisha, nashukuru Mungu kwa kuendelea kutupigania hadi sasa ......karibu.

Kusudi la somo.
Leo nataka tujifunze siri moja ya urafiki ambayo wengi hawajui, au wanaijua lakini hawaitumii. ....mwalimu wangu aliwahi kuniambia kwamba, ikiwa una ujuzi usio kusaidia, ...huna cha kujivunia. ....karibu tuendelee.

         SIRI YA KWANZA YA URAFIKI(SIFA YA ZIADA ).

Kwa nini urafiki? ..... utafiti unaonyesha mafanikio yetu yapo ndani ya rafiki zetu wa karibu. ...hii ndio sababu ya mimi kuandika somo hili. .....Siri ya kwanza ni ipi?
Siri ya kwanza kwenye urafiki ni ...sifa ya ziada .....

Sifa ya ziada ni ni sifa ambayo mtu anajiongezea kwa lengo la kumvutia rafiki yake. ..  hali hutokea mwanzoni mwa urafiki, .....nini madhara yake?

Kuna watu wapo kwenye urafiki mzuri, ila urafiki huo unaendeshwa na sifa ya ziada ambayo mmoja katika urafiki huo anaitumia. .Mtu ambaye anaitumia sifa ya ziada kuendesha urafiki, anatumia nguvu kubwa sana. ...tena nguvu anayoitumia ina mrudisha sana nyuma kimafanikio na ina mpa madhara ya kisaikolojia. ......!

Je, una uwezo wa kuyaishi maisha yaliyobebwa na sifa ya ziada?

Kila siku tunashuhudia kuvunjika kwa urafiki ambapo sababu kubwa ni mmoja wapo kwenye urafiki kupoteza sifa ya ziada aliyojipatia. ...
Tiba pekee kabla ya kuwa na rafiki, hakikisha unaishi maisha yako. ....be you, be smart. (ishi maisha yako, kuwa nadhifu )....utapata rafiki aina yako.

                See you at the top.
         scientist Saul kalivubha.
            (0652 134 707 )