Sunday, 8 January 2023

JIFUNZE TOFAUTI KATI YA WIVU NA KUTOJIAMINI

 JIFUNZE TOFAUTI KATI YA WIVU NA KUTOJIAMINI KWENYE MAHUSIANO 

Na Mwanasayansi Saul Kalivubha ✍ 

Wivu kwa maana rahisi ni kutojiamini , unahisi kuna watu wenye sifa zaidi yako watakuibia mpenzi wako 😔 Wivu hukoleza mapenzi 😊 

Kutojiamini ni wivu uliopitiliza kiasi , muda wote unahisi umpendaye ana njama mbaya dhidi yako kiasi cha kila siku kuwa na migogoro isiyoisha 

Kutojiamini ni sumu ya mahusiano.Wafikiri sababu zake ni nini? Na utajijuaje ikiwa una tatizo hili ?  Karibu darasani 

DALLI ZA KUTOJIAMINI 

Asipojibu meseji kwa wakati tayari unahisi kafanya makusudi 😔 

Asipoitikia simu yako wewe unajua yupo anafanya kitu kibaya 😔 

Ukimpigia simu akiwa anaongea na mtu mwingine tayari unahisi yupo anakusaliti 😢

Siku haiishi bila kumuwazia mabaya yaani unahisi kama vile hakupendi au anakudharau 😔 

Muda wote unahisi kama anakudanganya tu hakuna siku unamuamini 😔 

Unakuwa mwepesi kukasirika kwa vitu vidogo vidogo tu

Hujui bahati mbaya kila kitu kwako unaona ni njama mbaya aliyoipanga kukufanyia 😔 

Akiwa na marafiki zake tayari unahisi anakusaliti au wanamshaurii mabaya kukuhusu wewe 😔


Weka alama ya tick kwenye dalili inayokusumbua ikiwa kila migogoro ya mahusiano yako chanzo ni dalili zaidi ya nusu kati ya hizo kuna uwezekano mkubwa kati yenu kuna tatizo la Kutojiamini .Kutojiamini kuna leta migogoro na ni ngumu kuwa na mahusiano yenye afya nzuri ikiwa kati yenu kuna migogoro ambayo chanzo chake  kikubwa ni Kutojiamini .

Mbona hata dalili za wivu ni kama zinafanana na za Kutojiamini?  Swali zuri sana hilo ni kweli kabisa dalili pia za wivu ni kama hizo hizo sema kama nilivyokwiaha kusema juu kwenye utangulizi kuwa wivu ni Kutojiamini kuliko na kiasi na huwa hakuna migogoro kwenye wivu wa mapenzi bali hukuza mahusiano yenu ya mapenzi , bila wivu wa kiasi mahusiano huwa hayana raha. 


Kwenye wivu kuna upendo lakini kwenye kutojiamini  kuna upendo wa mashaka ndio maana kutojiamini ni chanzo kingine cha kuvunja mahusiano au kufanya watu wakuogope kwa sababu tu ya migogoro kila siku, hakuna anayependa migogoro ya kila siku .

Kutojiamini chanzo chake ni nini?  Kuna vyanzo vingi vya tatizo hilo yawezekana ikawa ni sababu za kimazingira au za kuzaliwa nazo( kurithi). Tuone sababu chache zifuatazo:

Kuwa na historia ya kusalitiwa : Mara nyingi tatizo la Kutojiamini linaonekana kwa watu ambao wana historia ya kusalitiwa na wenzi waliowapenda sana hivyo wanakuwa hawana imani tena watu , na mara nyingi tatizo linakuwa kubwa kama muhusika ataamua kuingia kwenye mahusiano mapya bila kupona kwa jeraha lake la kwanza hivyo matokeo yake anakuwa anaishi na mtu wa pili kama vile ni mtu yule wa kwanza.Tiba ya  tatizo hilo ikiwa chanzo ni hiki basi tiba yake ni kujiponya majeraha kabla ya kuingia kwenye mahusiano mapya. 

Chanzo kingine ni tabia yako ya kutafuta ukamilifu wa 100%; Tatizo hili ndio chanzo cha kutoamini kuwa kuna bahati mbaya ndio maana mwenzio akifanya vitu bahati mbaya tayari unajua ni makusudi kakufanyia na tayari ni mgogoro huo , hutaki kumuona kama na yeye ni binadamu bali unamuona kama ni malaika ambaye hakosei hata kidogo.  Tiba yake hapa  ni kujifunza kupuuzia baadhi ya vitu vinavyotokea kwenye mahusiano yako muhimu tu visiwe vina madhara makubwa kwenye safari yenu , kuna mambo unaweza kuyapuuzia na yasilete madhara kwenye mahusiano yenu lakini ukikata kufuatilia kila kitu lazima mtakuwa na migogoro mingi sana kwenye mahusiano yenu .

Chanzo kingine ni kuathiriwa na huyo umpendaye yaani unayempenda anakuwa na historia ya kukusaliti hivyo tayari kumuamini tena inakuwa ngumu hivyo anakujengea tabia ya Kutojiamini tena na matokeo yake ni kuwa na mashaka dhidi ya matendo yake. Tiba ya hapa inachukua muda wa kutosha na lazima yeye ndiye akutibu kwa kukuaminisha kuwa kaacha tabia zake za awali .

Chanzo kingine ni urithi; Tayari umezaliwa upo hivyo tu yaani una tatizo la Kutojiamini la kuzaliwa nalo , hapa kuna tiba kutoka pande mbili ambazo ni kutoka kwako na anayekupenda. Lazima ujikubali kuwa una tatizo na kujidhibiti pale uwezapo  na huyo akupendaye inabidi ajue kuwa una kasoro hiyo Hivyo lazima ajifunze kuishi na wewe. 

Makala hii imeandikwa na Mwanasayansi Saul Kalivubha 

Mafunzo yetu yapo mitandaoni kote kwa jina la fikiandotozako 

Pia kitabu cha siri za urafiki kinapatikana soft copy ( nakala tete) kwa Tsh4000 tu , ukilipa utatumiwa muda huo huo 


+255652 134707

Friday, 6 January 2023

KILA MTU ANA MTU WA HADHI YAKE  😊 MATESO YAPO PALE UTAPOWANG'ANG'ANIA WASIO WA HADHI YAKO 😢 

 KILA MTU ANA MTU WA HADHI YAKE  😊 MATESO YAPO PALE UTAPOWANG'ANG'ANIA WASIO WA HADHI YAKO 😢 

Na Mwanasayansi Saul Kalivubha ✍ 

Bila shaka kichwa cha andiko kimekusisimua 😄 kama ni kweli basi nawe tayari upo kwenye kundi la watu ambao wanasumbuliwa na watu 😔 Mwanasayansi kakuvuruga? 😔  haya twende darasani ✍

Kuna watu hata kwa nini hamuwezi kukaa kiti kimoja mkaelewana kwa sababu tu mna hadhi tofauti  mpaka mmoja apande/ashuke kwenye hadhi ya mwingine ndio mtakaa pamoja na kuelewana, wewe una hadhi gani? watu gani unawakumbatia? Ndugu yangu ukitaka mahusiano yakutese wakumbatie watu mnaopishana hadhi 😔

Kwa mfano wewe kwa sasa hadhi yako ni kuhudumia shilingi elfu kumi kwa mwezi wafikiri utaweza kukaa na mtu mwenye hadhi ya kuhudumiwa milioni moja kwa mwezi?  kwa namna yoyote hapo haiwezekani tu kabisa mpaka ajishushe kwenye hadhi yako au wewe upande kwenye hadhi yake tofauti na hivyo utatumia nguvu kubwa mpaka kukopa au kuuza rasilimali zako ili tu uendane naye lakini ukweli ni kuwa unaweza kufanikiwa mwanzoni tu lakini baadaye utashindwa na utabaki hovyo sana  

Huo ni mfano tu mmoja lakini ipo mifano mingi kwenye maisha ya kila siku ambapo watu hujikuta kwenye mateso kwa sababu tu ya kuwakumbatia watu wenye hadhi tofauti.  Ukiona hudumu sana na watu kwenye mahusiano yoyote yale kaa chini jitafakari sio ukimbilie kusema wewe una mkosi la hasha yawezekana una kasoro hii ya kuwakumbatia watu mnaopishana hadhi na mwisho wa siku unakuwa mtu wa kulaumu tu na wakati mchawi ni tabia yako hiyo.

Utajuaje hadhi yako? Swali nzuri sana hili , ni kweli ni lazima kwanza ujitambue hadhi yako kwa sasa ni ipi na sio kazi ngumu hata muhimu ni kujiangalia kwenye maeneo haya matatu WEWE NI NANI, UNATAKA NINI NA UNA MUDU KIPI.   Kama unajitambua kwenye hayo na bado matokeo ni yale yale basi yawezekana pia wewe ni mbishi hutaki kujikubali kuwa wewe ni nani ndio maana unalazimisha wasio na hadhi yako.

Siku utakokubali kuwa kuna watu tu sio hadhi yako ndipo utayaona mahusiano ni mazuri kwa sehemu 😊 na utaona ukipendwa na kuheshimiwa 😊 lakini huyaoni hayo kwa sababu upo na watu ambao sio hadhi yako unaumia tu kila siku na kucheleweshwa na usipokuwa makini utakumbuka shuka tayari ni asubuhi 😔  Fanya tu maamuzi magumu ya kuwaacha watu wa ambao sio hadhi yako ili upatane na wenye hadhi yako au tulia kwanza ukuze hadhi yako ndio upate wenye hadhi sawa.

Kuna watu huwapati na hutowapata kwa sababu tu sio hadhi yako na unapoteza muda kwenye hilo. Kuna msemo unasema kuwa embe halianguki mbali na mti wake , huu ni msemo wenye hekima na wahenga waliifikiria mbali kwenye hilo maana sio kazi rahisi ukute embe chini kusiko na mti wake labda tu liwe limetupwa 😄  na kwa nini litupwe ? Ila ukiona embe chini kikawaida kuna mti wake pembeni ndio sawa na maisha yetu ukiona wawili wanaendana kuna uwezekano mkubwa wakawa na hadhi moja tofauti na hivyo basi kuna mmoja amekubali kuwa mtumwa wa mwingine 😔 Sasa kwa nini ukubali kuwa mtumwa? na wakati wa hadhi yako yupo tu na mngefurahia maisha tu

Tafuta mtu wa hadhi yako ndio sasa taratibu muanze kupanda hadhi pamoja na kama utapata mtu asio wa hadhi yako mkaendana basi pia shukuru Mungu na hii huwa inatokea lakini ni mara chache sana 


Makala hii imeandikwa na Mwanasayansi Saul Kalivubha 

+255652134707


Madarasa yetu yapo Instagram  kwa jina la  fikiandotozako 

Sunday, 1 January 2023

KUNA TOFAUTI KATI YA MTU MASKINI NA MTU AMBAYE HANA PESA 

 KUNA TOFAUTI KATI YA MTU MASKINI NA MTU AMBAYE HANA PESA 

Na Mwanasayansi Saul Kalivubha ✍ 

Mtu anaweza kuwa hana kabisa pesa hata shilingi mia lakini asiwe MASKINI na mtu anaweza kuwa anakula tu vizuri na kila kitu cha ndani lakini akawa MASKINI 😔  Mwanasayansi kakuchanganya? 😄 🤣 

Hapana nipo sahihi ✍ 

Umaskini ni IMANI lakini kukosa pesa ni MAPITO , Unaweza pitia kipindi cha kukosa pesa lakini imani yako ni ya KITAJIRI 

Umaskini ni imani kama zilivyo imani nyingine tu za kiroho mfano uislam na Ukristo ulivyo na waumini ndivyo ilivyo hata kwenye Umaskini kuna waumini wake wamo humo ndio maana sio kazi rahisi kuaga Umaskini, narudia tena sio kazi rahisi kuaga Umaskini kama ilivyo ngumu kumbadilisha muislamu kuwa mkristo  au kinyume chake, unajua sababu? Ni kwa sababu tu kila muumini ameshika mizizi ya dini yake hivyo sio rahisi kuiachia kirahisi. 

Umaskini huanzia kwenye akili ya mtu ndio maana watu maskini huwa wana viashiria vya kufanana kwa sababu tu wapo imani moja, je wajua viashiria? ( Dalili za umaskini)


#Ni watu wa visingizio

#Ni watu wa kuridhika na maisha ya kujaza tumbo tu

#Huamini kuwa wanaoshindwa wametoa rushwa au ni wenye imani za kishirikina 

#Kila jambo wanasema ni mpango wa Mungu hata ambalo  ni matokeo ya uzembe wao

Hizo ni dalili chache kati ya nyingi za muumini wa UMASKINI yawezekana unazo chache au zote kati ya hizo basi jijue wewe ni muumini wa UMASKINI tayari 😔 

Unaweza kutoka humo? Ndio inawezekana kutoka humo japo sio rahisi kama nilivyokwisha kusema kuwa sio rahisi kubadili imani 😔 nguvu kubwa inatakiwa 

Lazima kwanza ukubali kuwa wewe ni maskini upo kwenye imani hiyo sasa unatakiwa kuanza taratibu kuzikana imani hizo za kimaskini ili uhame kutoka imani hiyo uende kwenye imani ya UTAJIRI 

UTAJIRI ni imani pia yenye waumini wachache lakini na misingi ya imani yao ipo kinyume na misingi ya umaskini hivyo ni rahisi tu kuwa humo kama tu utaikana misingi ya umaskini 


Nikutakie mwaka mpya mwema ndugu yangu 


+255652 134707

Monday, 3 October 2022

 USISUBIRI PESA IPUNGUE NDIO UWEKE NIDHAMU YA MATUMIZI

Matumizi ya pesa bado ni changamoto kwa watu wengi na matokeo yake hujikuta katika ukosefu wa pesa wa mara kwa mara na hii sio kwa waajiwa tu hata waliojiajiri kwenye mambo yao binafsi  bado hujikuta kwenye kipindi kigumu cha ukosefu wa pesa sio kwa sababu haikuwepo la hasha ni kwa sababu ilikuwepo lakini ikatumiwa bila kuzingatia matumizi sahihi kutokana na kipato. Ukipata muda tulivu ukajitafakari utagundua kuwa pindi upatapo pesa matumizi yako yanakuwa juu na hupungua kadri pesa inavyopungua yaani kwa lugha rahisi  ni kuwa nidhamu yako ya matumizi ya pesa inaongezeka kadri unavyoishiwa pesa. 

Pesa ni nguvu ya kihisia ambapo usipoitawala itakutawala yenyewe kwa kukupa maamuzi mengi na hapo utakosa utulivu hali ambayo itafanya upoteze nidhamu ya matumizi ndio maana mshahara ukiingia unaweza jikuta unafanya manunuzi bila kuangalia ukubwa wa gharama kwa sababu unajua pesa ipo lakini ukianza kusikia mfuko umepwaya ndio utarudisha makini wa matumizi kwa mfano mwanzo ulilipwa laki tano na ilipofikia mfukoni umebaki na laki moja ndio utaanza kuipigia mahesabu hiyo laki moja kuangalia kama itakufikisha mwezi mwingine, je kwa nini hukufikiria hivyo tangu ukiwa na laki tano? 

Nidhamu ya pesa ni kuheshimu pato lako kwanza na pili ni kuheshimu matumizi sahihi yaliyo ndani ya kipato chako kama ulipanga kununua kitu cha shilingi mia ndio itakuwa sawa kulingana na kipato chako basi fanya hivyo lakini ulinunua kwa shilingi Mia mbili ujue umekula na pesa ya siku fulani hivyo jiandaye siku hiyo kukosa pesa la sivyo iwe ni dharura ndio tumia lakini kama si dharura yatakiwa ujidhibiti dhidi ya matumizi ya pesa pale tu unapoipata, changamoto ya pesa ni kuwa ukitumia pesa ndogo unaona kawaida tu lakini mwisho wa siku ukijumlisha unakuta kama ungehifadhi ungekuwa mbali sana kifedha hivyo nidhamu ukianza na kuheshimu matumizi yako yaliyo ndani ya kipato chako utakuwa kwenye kiwango kizuri cha kuweka akiba. 

Nidhamu binafsi katika matumizi ya pesa inajengwa na lengo kuu ulilonalo la kesho hapo ndio utakuwa unatumia pesa ukikumbuka kesho hivyo utakuwa ukijikumbusha kila kabla ya matumizi ambayo si salama kulingana na kipato chako na utakuwa na nidhamu muda wote, lazima uwe na nidhamu au ukose nidhamu lakini ukubali kupoteza lengo kuu la kesho na njia nzuri nyingine ni kuigawa pesa yako kwa siku utagundua unaingiza shilingi ngapi kila siku na kisha angalia matumizi yako kila siku yanaendana na pato lako la siku? Kwa kuanzia na hapo utajirekebisha kimatumizi na utaheshimu matumizi sahihi ya pesa. 

Pesa ikiwa nyingi itakupa upofu wa kuamini kuwa huwezi kuishiwa hivyo kila matumizi yakujiayo kichwani utayafanya na hapo ndio mwanzo wa kutumia hovyo pesa  mpaka baadaye ikipungua ndio itakutoa upofu uone kuwa kuna hatari itokanayo na ukosefu wa pesa kwa sababu pesa uliyonayo haitoshi kukufikisha msimu mwingine wa pesa kumbe kuna kuna nguvu kubwa inatakiwa uwe nayo awali ili kudhibiti hisia za pesa zisikutawale. 

Kujua unataka nini pia ni moja wapo wa ujenzi mzuri wa nidhamu ya pesa kwa sababu utajizuia dhidi ya matumizi ambayo sio ya msingi kwako na hayapo ndani ya bajeti yako kwa kipato chako na aina yako ya safari uliyonayo, kutojua nini unataka itakuingiza kwenye matumizi yasiyo sahihi kwa sababu kila utakachokiona kinavutia utahitaji kukinunua. Pesa isikuendeshe bali unatakiwa wewe ndio uipangie majukumu  na ukiona unalemewa basi jitahidi usiwe unatembea na pesa nyingi mfukoni hii ni njia nzuri pia ya kuitawala pesa kwa sababu huwezi kufanya manunuzi yasiyo na mpangilio, tunafanya manunuzi yasiyo na mpangilio kwa sababu tunakuwa na pesa au urahisi wa kuipata pesa. Usikumbushwe na matatizo bali jikumbushe mwenyewe kuwa kuna siku changamoto zitatokea na uhitaji wa pesa utatakiwa na sio usubiri matatizo yakufikie ndio uone umuhimu wa kutunza akiba kabla. 

Njia nyingine nzuri itakayokifanya uwe na nidhamu ya pesa wakati wote ni kupunguza matumizi yasiyo na lazima na kujenga utaratibu wa kununua vitu vya jumla kuliko vya reja reja  na pia kusimamia lengo kuu kwa msimu kwa mfano kila mwaka uwe na lengo kuu la kufanya hivyo kwa namna yoyote utajibana ubaki na pesa ya kufanikisha lengo hilo  maana ukitumia hovyo pesa basi uwe tayari pia kulipoteza lengo hilo 


Mwanasayansi Saul Kalivubha 

0652 134707

Thursday, 28 July 2022

NAMNA YA KUWEKA NIDHAMU YA PESA

NIDHAMU YA MATUMIZI SAHIHI YA PESA 

Matumizi ya pesa bado ni changamoto kwa watu wengi na matokeo yake ni hujikuta katika ukosefu wa pesa mara kwa mara na hii sio kwa waajiwa tu hata waliojiajiri kwenye mambo binafsi  bado hujikuta kwenye kipindi kigumu cha ukosefu wa pesa sio kwa sababu haikuwepo la hasha ni kwa sababu ilikuwepo lakini ikatumiwa bila kuzingatia matumizi sahihi kutokana na kipato. Ukipata muda tulivu ukajitafakari utagundua kuwa pindi upatapo pesa matumizi yako yanakuwa juu na hupungua kadri pesa inavyopungua yaani kwa lugha rahisi  ni kuwa nidhamu yako ya matumizi ya pesa inaongezeka kadri unavyoishiwa pesa. 

Pesa ni nguvu ya kihisia ambapo usipoitawala itakutawala yenyewe kwa kukupa maamuzi mengi na hapo utakosa utulivu hali ambayo itafanya upoteze nidhamu ya matumizi ndio maana mshahara ukiingia unaweza jikuta unafanya manunuzi bila kuangalia ukubwa wa gharama kwa sababu unajua pesa ipo lakini ukianza kusikia mfuko umepwaya ndio utarudisha makini wa matumizi kwa mfano mwanzo ulilipwa laki tano na ilipofikia mfukoni umebaki na laki moja ndio utaanza kuipogia mahesabu hiyo laki moja kuangalia kama itakufikisha mwezi mwingine, je kwa nini hukufikiria hivyo tangu ukiwa na laki tano? 

Nidhamu ya pesa ni kuheshimu pato lako kwanza na pili ni kuheshimu matumizi sahihi yaliyo ndani ya kipato chako kama ulipanga kununua kitu cha shilingi mia ndio itakuwa sawa kulingana na kipato chako basi fanya hivyo lakini ulinunua kwa shilingi Mia mbili ujue umekula na pesa ya siku fulani hivyo jiandaye siku hiyo kukosa pesa la sivyo iwe ni dharura ndio tumia lakini kama si dharura yatakiwa ujidhibiti dhidi ya matumizi ya pesa pale tu unapoipata, changamoto ya pesa ni kuwa ukitumia pesa ndogo unaona kawaida tu lakini mwisho wa siku ukijumlisha unakuta kama ungehifadhi ungekuwa mbali sana kifedha hivyo nidhamu ukianza na kuheshimu matumizi yako yaliyo ndani ya kipato chako utakuwa kwenye kiwango kizuri cha kuweka akiba. 

Nidhamu binafsi katika matumizi ya pesa inajengwa na lengo kuu ulilonalo la kesho hapo ndio utakuwa unatumia pesa ukikumbuka kesho hivyo utakuwa ukijikumbusha kila kabla ya matumizi ambayo si salama kulingana na kipato chako na utakuwa na nidhamu muda wote, lazima uwe na nidhamu au ukose nidhamu lakini ukubali kupoteza lengo kuu la kesho na njia nzuri nyingine ni kuigawa pesa yako kwa siku utagundua unaingiza shilingi ngapi kila siku na kisha angalia matumizi yako kila siku yanaendana na pato lako la siku? Kwa kuanzia na hapo utajirekebisha kimatumizi na utaheshimu matumizi sahihi ya pesa. 

Pesa ikiwa nyingi itakupa upofu uuamini kuwa huwezi kuishiwa hivyo kila matumizi yakujiayo kichwani utayafanya na hapo ndio mwanzo wa kutumia hovyo pesa  mpaka baadaye ikipungua ndio itakutoa upofu uone kuwa kuna hatari itokanayo na ukosefu wa pesa kwa sababu pesa uliyonayo haitoshi kukufikisha msimu mwingine wa pesa kumbe kuna kuna nguvu kubwa inatakiwa uwe nayo awali ili kudhibiti hisia za pesa zisikutawale. 

Kujua unataka nini pia ni moja wapo wa ujenzi mzuri wa nidhamu ya pesa kwa sababu utajizuia dhidi ya matumizi ambayo sio ya msingi kwako na hayapo ndani ya bajeti yako kwa kipato chako na aina yako ya safari uliyonayo, kutojua nini unataka itakuingiza kwenye matumizi yasiyo sahihi kwa sababu kila utakachokiona kinavutia utahitaji kukinunua. 


Mwanasayansi Saul Kalivubha 

0652 134707

Saturday, 30 April 2022

MAISHA HAYA HAPA

UNATAFUTA MAISHA? HAYA HAPA.

Kumekuwa na semi nyingi kuhusu maisha na karibia kila siku watu hutoa majibu kuwa wametingwa na harakati za kutafuta maisha  lakini swali ni je unajua unachokitafuta?  Unayajua maisha?  
Maisha ni uhai hivyo kama wewe sio mfu basi tayari una maisha kwa sababu ungekuwa huna maisha ungekuwa kaburini leo ila kwa kuwa unapumua tayari maisha unayo yafaa ushukuru Mungu kwanza kwa hilo la wewe kuwa na uhai mpaka sasa ni nafasi ya upendeleo kwako.
Unatafuta nini? Unachotafuta ni vitu ambavyo vitafanya maisha yako yaendelee kuwepo ambapo vitu hivyo vipo kwenye makundi makubwa mawili  ambayo ni vitu vya msingi kwa uhai na vitu vya zaidi ya uhai .
Vitu vya msingi kwa uhai ndivyo huitwa mahitaji ya lazima ili kuulinda uhai wako  na ukifanikiwa vitu hivyo tayari hiyo ni hatua ya awali ya mafanikio kwa sababu ukiwa na hivyo akili itaacha kuwa na msongo wa mawazo juu ya vitu hivyo na sasa itaanza kuwazia hatua ya pili ambayo ni mafanikio zaidi ya kuwa hai .
Mahitaji ya msingi kulinda uhai wako ni kama vile  Chakula, malazi na mavazi . Bila chakula huwezi kuwa na uhai kwa sababu mwili unahitaji chakula ili usipoteze uhai  , bila malazi pia unakuwa kwenye hatari kubwa ya kuupoteza uhai kwa sababu ni rahisi kushambuliwa na wanyama wakali na endapo utalala nje na hatimaye kuupoteza uhai na bila ya mavazi pia ni hatari kwa sababu ni hatari kushambuliwa na vimelea vya magonjwa na hata kupoteza kujiamini kwa sababu tu unatembea utupu ilihali wengine wamevaa. 
Unaweza kumudu Chakula?
 Unaweza kujimudu sehemu ya kuishi?
 Unaweza kujimudu mavazi?  
Kama maswali yote matatu kwako majibu ni ndiyo basi hongera sana hiyo ni hatua kubwa sana kimafanikio inayolinda uhai na kama majibu yako kwa maswali yote matatu ni hapana basi bado kwa namna moja utakuwa bado ni tegemezi na kama umri wako kisheria ushavuka utegemezi basi mapambano yaendelee kutafuta kwanza vitu hivyo vitatu ili uweze kujimudu kwanza na kisha uanze kuwazia hatua ya pili ya mafanikio. 
Hatua ya pili ya mafanikio inategemea na hiyo ya kwanza, ukishakuwa una uwezo wa kujimudu tayari  sasa hatua ya pili itakuwa kutafuta zaidi ya uhai na hiyo ndio hatua ya kuacha alama kwenye maisha yako , hatua hiyo ya pili ni kuliishi kusudi la kuumbwa kwako hivyo kama uliumbwa kuwa mchezaji wa mpira basi simamia vizuri eneo lako , kama uliumbiwa kuwa mwimbaji basi simamia vizuri eneo hilo kwa ufupi tu tuseme kuwa hatua ya pili ni kuishi ulichoumbiwa  .

Mafanikio mazuri ni muungano wa hatua zote mbili ambazo  ni uwezo wa kujimudu na uwezo wa kuishi kusudi la kuumbwa. Hatua ya kwanza ya kujimudu kwenye chakula, malazi na mavazi inahitaji ubunifu wa hali ya juu sana la sivyo utashindwa kuivuka hatua hiyo na muda wote utakuwa unapambana kwa ajili  ya mwili wako tu na sio kwa mapendeleo zaidi, unahitaji ujenge mfumo utakaofanya uwe unapata mahitaji yako bila wewe kujishughurisha moja kwa moja kwa mfano unaweza kuwa na biashara ambayo itakuwa inajiendesha ili kukupatia pesa ya chakula, malazi na mavazi  lli kipindi biashara hiyo inaendelea wewe unakuwa busy na kupambania hatua ya pili ya mafanikio. 
Karibia kila siku inatakiwa uwe unajitathmini kujiona ni hatua gani upo? na mipango ipi umeweka ili kuvuka  hatua ya kwanza.

Upo hatua gani wewe? 

#Mwanasayansi Saul Kalivubha. 
#Fikiandotozako.
+255652134707

Saturday, 9 April 2022

NAMNA YA KUTIBU MAJERAHA YA KIHISIA

 TIBA YA HISIA ZILIZOJERUHIWA. 

HISIA ni msukumo ambao unahitaji kutimilizwa , mfano  mtu ukiwa na hisia za kupenda utafurahi ukipendwa, ukiwa na hisia za hasira utataka ufanye jambo fulani kuimaliza hasira n.k, sasa tunapata picha kuwa kila kwenye hisia kuna jambo litatakiwa kufanywa ili kutimiliza lengo la hisia.Tuangalie kisa  hiki ambapo najua kwa namna moja au nyingine utakuwa umewahi kuwa muhanga, mmepanga kukutana na rafiki yako mnayependana kweli   mara ghafla siku moja kabla anakutumia ujumbe kuwa hatoweza kuja tena siku hiyo kapatwa na dharura  hivyo mpaka siku nyingine kama wewe utajisikiaje? Kwa jibu la haraka utajisikia vibaya na sababu kubwa sio kuwa kakupotezea muda kama wengi wanavyodai la hasha ni kwa sababu ujio wake kwako ulikuwa ni tiba ya hisia fulani ambazo tayari zilikupanda pale tu mlipokubaliana  kukutana  tena kibaya zaidi mkiwa mna mahusiano ya kimapenzi ndio utatumia zaidi  kwa sababu kajeruhi hisia zako. 

Tumeona kuwa kila kwenye hisia kuna jambo linatakiwa hivyo lisipofanyika basi hisia zako zitakuwa zimejeruhiwa. Jeraha la kihisia ( psychological trauma)   linatofautiana ukubwa kutokana na aina ya hisia iliyojeruhiwa  mfano hasira uliyonayo dhidi ya mtu unayemdai na unataka uonane naye umwambie bayana endapo hutaonana naye utaumia lakini muda sio mrefu jeraha lake litapona utaendelea na maisha lakini hisia za kupenda ikitokea umempenda mtu  lakini mwenzako akawa msaliti na mwisho mkavunja uhusiano hilo jeraha lake  kupona sio rahisi na litakuathiri sana kama utakosa mbinu za kujitibu.

Bila shaka umewahi kuona watu wakiwa na tabia mpya punde tu baada ya kukutwa na maswaibu fulani, ulevi, wizi, uhuni , kuchelewa kuoa/kuolewa kwa kutoamini tena mahusiano  n.k, hayo ni moja ya matokeo ya kushindwa kujitibu majeraha ya hisia zilizojeruhiwa au  kujitibu kwa mbinu zisizo sahihi  kwa sababu baada ya hisia kujeruhiwa  kinachofuata  ni muhusika kutafuta tabia mpya itakayomsaidia kusahau maumivu  sasa hapo ndipo kuna tatizo  wengi huchagua tabia ambayo ndio badala ya kuwatibu ndio inawakandamiza zaidi mfano baada ya mtu kuachwa kwenye mahusiano anaamua kutokuwa tena muaminifu au kutowaamini tena watu tabia ambayo inamfanya aendelee kuteseka kwa sababu ataachwa tena kwa kukosa uaminifu. 

Hisia zinapojeruhiwa jitahidi ukubali kwanza hali  na pia katika machaguzi ya tabia mpya itayokufanya ujione sawa usichague vilevi  na wala usichague kulipiza kisasi bali chagua kujiboresha zaidi ili hata ikitokea tena basi sababu nyingi zisilalie kwako , fuata hatua hizi :

1.ikubali hali. 

2.Usianzishe tabia za kujisaulisha kwa muda  mfano kuanza ulevi n.k,bali tafuta tabia itayokuboresha zaidi 

3. Jipe muda mrefu wa kujiboresha ukiwa bora itakujengea kujiamini. 

4.Ukiridhika kuwa umejiboresha sasa unaweza kuendelea na maisha mengine na ukiweza epuka vichocheo vitavyokufanya ukumbuke namna ulivyojeruhiwa kihisia.

Saul Kalivubha ,Mwanasayansi tiba  

            +255652 134707