Friday, 24 February 2017

HOFU YA KUSHINDWA-1

Karibu tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya maisha, nina imani hali yako ya afya ni njema, shukuru Mungu kwa hilo.
Leo nimeona tujifunze swala zima la HOFU.....maana hakuna mafanikio unaweza fikia ikiwa hofu yako imezidi hali ya kawaida.

KUSUDI LA SOMO.
Lengo la somo letu hili ni kujifunza HOFU YA KUSHINDWA, Somo hili lina sehemu tatu ambazo ni.
                   1. CHANZO CHA HOFU
                     2. MADHARA YA HOFU.
                      3.JINSI YA KUISHINDA HOFU YA KUSHINDWA.

NB. zipo hofu za aina nyingi sana Mfn  hofu ya kujaribu, hofu ya kukoselewa  n.k,ila hofu zote hizo matokeo yake ni KUSHINDWA kwa jambo ambalo mtu anakusudia kufanya.
.......Hofu kwa maana halisi ni hali ya kuogopa anayokuwa mtu juu ya matokeo ya jambo flani.
               
               1.CHANZO CHA HOFU YA KUSHINDWA.

Zipo sababu nyingi sana zinazopelekea watu wengi kuwa na hofu ya kushindwa katika mambo yao wanayokusudia kuyafanya, chache kati ya hizo ni;

HISTORIA YA MTU...,katika maisha yapo mambo mengi mtu anapitia ambayo hayakuwa na matokeo mazuri kwake, inaweza kuwa ni mahusiano, biashara , hata katika masomo. Kupitia matokeo mabaya hayo, watu wengi hutengeneza imani ya kukosa uaminifu wa kurudia tena mambo hayo,hivyo mtu huyu anakuwa na hofu ya kushindwa kila anapokutana na mazingira yaliyo mfanya ashindwe.

KUTOJITAMBUA...,mtu asiye tambua mazingira anayostahili kupitia ili kufikia ndoto yake huwa anakuwa na hofu ya kushindwa, kwa nini? kwa sababu hana uhakika na alicho shika,kwa hiyo muda wote anakuwa anawaza kushindwa tu katika harakati zake.

MARAFIKI, marafiki wana nafasi kubwa ya kutengeneza hofu ya kushindwa kwa mtu, ukiwa na rafiki wengi ambao walijaribu na kushindwa. .....kibaya zaidi wakakata tamaa, ni rahisi wewe kutengeneza hofu ya kushindwa katika mambo ambayo rafiki zako walijaribu na kushindwa hadi kukata tamaa.
kuna uwezekano kuwa walio fanikiwa wengi waliacha rafiki zao wenye mtizamo wa kushindwa. ....hiyo iliwasaidia kupunguza hofu ya kushindwa kwenye mambo yao.

KUKOSA JUHUDI, hii ni sababu nyingine kubwa katika kutengeneza hofu ya kushindwa kwa mtu, kabla ya kufanya jambo flani,  kuna hali inakuja ya kukukumbusha juu ya maandalizi uliyo fanya kuhusu jambo hilo, hapo ndipo HOFU huanzia kutokana na majibu utayojipa.
mfano, kabla ya kufanya mtihani lazima juhudi yako ikupe hali ya hofu au ushujaa wa kufanya mtihani huo.

NB. Huwezi kufanya maamuzi sahihi ukiwa katika hali ya hofu, maana watu wenye  hofu mara nyingi hutafuta njia za ziada za kupunguza hofu zao. .......swali, Hizo njia za ziada zina matokeo gani kwenye kesho yako?
       .Hofu ina tiba,fatilia somo hili hadi mwisho utajua tiba yake.


                            See you at the top
                          Scientist Saul kalivubha
                           (0652 134 707 )

Thursday, 16 February 2017

KOSA LA 1 KWENYE MAFANIKIO

Karibu tena kwenye blog hii ya maisha, upande wangu mimi ni mzima, natarijia hivyo kwako pia. Usisahau kumshukuru Mungu kwa kila hatua unayopitia.
Siku ya leo nimeona vyema tujifunze kosa ambalo wengi tunalifanya na kujikuta tunapoteza ndoto zetu.

                       KUSUDI LA SOMO.

Lengo la somo letu hili ni kutafuta kosa la kwanza ambalo limefanya wengi wetu tuwe sehemu tofauti na kusudi.
Kosa la kwanza ambalo wengi tunafanya ni MAAMUZI YA KUCHAGUA RAFIKI. Ili kulielewa somo hili nmejaribu kugawa vipindi vya umri na uhusiano wa kufanya maamuzi ya RAFIKI.
Fatilia kama ifatavyo;

#MAISHA KATI YA MWAKA 1 HADI 17.
Katika umri huu hakuna tatizo sana, maana  wengi katika umri huu huongozwa na malezi ya walezi wao, pia katika umri huu wengi huwa hawajui nini maana ya rafiki katika mafanikio yao, ingawa kulingana na mabadiliko ya mwili vijana wengi hujaribu mengi na wanao jaribu mabaya huwa karibu na rafiki wa aina hiyo.
Ila huwa ni rahisi kurekebisha makosa ya uchaguzi wa rafiki katika umri huu.

#MAISHA KATI YA  UMRI WA MIAKA 18 -28 (KOSA LA 1)
Hapa ndipo kosa la kwanza huwa na asilimia nyingi za kugeuza njia yako, katika umri huu ukikosea kuchagua rafiki kuna uwezekano usijue utofauti wako, Umri huu ni hatari sana maana vijana wengi huwa kwenye mkusanyiko ya watu wenye malengo tofauti, kibaya zaidi ni kwamba. ......kuna uwezekano kati ya watu kumi, watu watatu tu ndo wana uwezo wa kuishi maisha yao halisi ikiwa watajichanganya na watu wenye malengo tofauti na wao. .....
Kuna uwezekano mkubwa kuwa watu ambao hawapo sehemu sahihi katika uzee wao, ndoa zao na mafanikio yao walifanya kosa hilo katika umri huu.
Makosa yapo mengi, ila ukipatia kuchagua RAFIKI kuna uwezekano mkubwa wa kuijua njia yako na kupunguza idadi ya makosa.

#MAISHA KUANZIA UMRI WA MIAKA 30 NA KUENDELEA.
Kama upo kwenye umri huu na ulifanikiwa kuwa na uchaguzi mzuri wa MARAFIKI sio tatizo sana, ila kwa walio kosea huwa hali sio nzuri kwao..............Tatizo moja kwa walio kosea na wapo kwenye kundi hili ni IMANI walizojijengea. .....hili ni tatizo kwa sababu kwa imani hizo inakuwa ni ngumu kurudi kwenye njia zao sahihi  (ingawa kwa umri huu huwa ni Kazi kidogo kurudi kwenye ndoto uliyopoteza ingawa kurudi inawezekana ).

RAFIKI sio jambo la kawaida kama wengi wanavyolichukulia, ni jambo la tofauti katika kukufikisha kwenye kusudi sahihi.
Swali la kujiuliza. ..."unafahamu utofauti ulionao? Rafiki yako anatambua kwa nini yupo hapo alipo? "
Kabla ya kufikia umri wa kutumia nguvu kurudi kwenye njia yako sahihi hakikisha unafanya tasmini ya maamuzi yako ya kuwa na rafiki wa aina hiyo. ....

             Tuonane wiki ijayo


                     See you at the top
                Scientist Saul kalivubha
                         (0652 134 707 )

Thursday, 9 February 2017

NDOTO YA MSIMU -3

Nakukaribisha tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya maisha, mimi ni mzima wa afya, nina imani wewe pia ni mzima.
Tupo kwenye sehemu ya somo letu la NDOTO YA MSIMU , na leo tunamalizia somo letu hili.

 KUSUDI LA SOMO.
Lengo la somo letu la leo ni kujifunza MADHARA YA NDOTO YA MSIMU. Nikukumbushe tu, somo letu lilikuwa na sehemu tatu.
1. MAANA YA NDOTO YA MSIMU.
2.CHANZO CHA MTU KUWA NA NDOTO YA MSIMU.
3.MADHARA YA NDOTO YA MSIMU.
Kabla ya somo la leo ni vyema ukapitia masomo yaliyo pita ya NDOTO YA MSIMU,Ingia Google kisha  andika NDOTO YA MSIMU Kalivubha blog, utaletewa masomo hayo.



                              3.MADHARA YA NDOTO YA MSIMU.
Leo tuangalie ni madhara gani yanaweza kumkuta mtu ambaye hutegemea mabadiliko ya mazingira katika kutengeneza ndotoya yake  (ndoto ya msimu )...........
Tumuangalie mtu huyo kwa kumlinganisha na sehemu tatu, biashara, mahusiano na mafanikio yake.

#BIASHARA; katika biashara huwa ni ngumu mtu mwenye ndoto ya msimu kuendelea, maana mtu huyu hufanya biashara kwa kutegemea maneno ya watu, leo akisikia Ufugaji wa kuku unalipa, hukurupukia Ufugaji huo bila kufanya tasmini kabla, kesho akisikia kilimo kinalipa, anaweka ndoto zake kwenye kilimo na huku bado swala la Ufugaji ajalifanyia uhakiki.
Mwisho wa siku mtu huyu hujikuta ana malengo mengi yasiyo hai. .........ikiwa huna jambo la kusimama, utajikuta kila wazo kutoka nje kwako ni sahihi, ila huwezi fanikiwa kwa mwendo huo.

#MAHUSIANO, Katika mahusiano, mtu mwenye ndoto ya msimu hutegemea mazingira yaongoze mahusiano yake, hawezi kutulia sehemu moja na mtu mmoja.
Leo akisikia flani yupo kwenye mahusiano na yeye atahitaji kuingia kwenye mahusiano, kesho akisikia mahusiano yana changamoto mtu huyo atahitaji kuachana na mahusiano.
Madhara ya mwendo huo ni mtu wa namna hiyo atakuwa na orodha ya watu wengi kwenye mahusiano yake, hali hiyo itampa madhara ya kisaikolojia na mwisho wa siku ataishia sehemu isiyo sahihi.

#MAFANIKIO, mafanikio kwa ujumla kwa mtu mwenye ndoto ya muda mfupi  (msimu ) huwa sio mazuri, maana juhudi za mtu mwenye ndoto ya msimu huwa ni za msimu pia.
Leo akifanya vibaya kwenye masomo, atawekeza juhudi nzito, muda ukipita kidogo husahau na kurudi kwenye hali iliyomfanya apate ufaulu usio mzuri, hata kwenye mambo mengine pia anakuwa na juhudi za muda mfupi.
Hali hii humfanya mtu huyo kuendelea kupata matokeo yale yale kwenye mambo anayofanya. .......

MUHIMU; Dawa pekee ya kuachana na ndoto za muda mfupi ni kuhakikisha unafahamu vizuri kitu unachokitafuta
Ukiwa  na lengo la kupata Chungwa na huku hulifahamu vizuri, ni rahisi wewe kupokea Embe(hali ambayo ni hatari sana kwenye maisha )

SWALI ZURI KUJIULIZA; hali uliyokuwa nayo mwishoni mwa mwaka  (ki malengo ) ndiyo unayo hadi sasa? .....au mazingira ya mwisho wa mwaka kwa kuwa yameisha, umesahau malengo yako yote.... ikifika tena mwisho mwaka utaanza kuwa busy na kuweka malengo. .........JITASMINI.

                     Tukutane week ijayo kwa somo mpya.
                    Jiandae pia kupata kitabu chenye siri za URAFIKI katika mafanikio yako.
                     
                        See you at the top.
                         Scientist Saul kalivubha.
                             ( 0652 134 707 )

Wednesday, 1 February 2017

NDOTO YA MSIMU -2

Naendelea kumshukuru Mungu kwa kuzidi kunipigania katika mwaka, ni furaha yangu kwa kuwa nina imani Mungu ni wetu sote, hivyo wewe pia ni mzima. ......Tupo kwenye muendelezo wa somo letu la NDOTO YA MSIMU,tuliweza kujifunza MAANA YA NDOTO YA MSIMU,  kabla ya kuendelea na sehemu ya leo, kama hukufanikiwa kulipitia somo hilo,fata link hii ujifunze kwanza  (http://kalivubha.blogspot.be/?m=1)).

 KUSUDI LA SOMO. 
Leo nataka tujifunze machache kuhusu sehemu ya pili ya somo letu hili ambayo ni CHANZO CHA MTU KUWA NA NDOTO YA MSIMU. ...... Nakukumbusha tena, somo letu lina sehemu tatu.   
          1 .maana ya ndoto ya msimu. 
           2.chanzo cha mtu kuwa na ndoto ya msimu. 
           3. Madhara ya ndoto ya msimu. 



                 2.CHANZO CHA MTU KUWA NA NDOTO YA MSIMU. 

Hapa nataka tuangalie baadhi ya sababu zinazo fanya watu wasiwe na ndoto za kudumu za maisha yao, kinyume chake mazingira yanawafanya watengeze ndoto za msimu ambazo hupotea baada ya mazingira kubadilika. Zipo sababu nyingi ila chache kati ya hizo ni hizi hapa; 

KUKOSA UBUNIFU. Ubunifu kwa maana ya haraka ni kutengeneza jambo la tofauti , mtu mbunifu huwa maisha yake yana asilimia nyingi ya juhudi zake. ...ila mtu ambaye siyo mbunifu maisha yake yamejengwa na mazingira ya nje. 
Mtu asiye mbunifu  tabia yake kubwa ni kukosa msimamo na alicho nacho , leo akiwa na ndoto hii kesho akikutana mazingira tofauti anatengeneza ndoto nyingine.

KUTOJITAMBUA. Kutojitambua ni tatizo kubwa sana, mtu asiye jitambua ni vigumu kutoa sababu za kwanini yupo pale alipo. .....kwa hiyo kila sehemu kwake ni sahihi maana sehemu sahihi haijui. mtu huyu hata ndoto ya msimu hana,bora uwe na ndoto ya msimu kuliko kutokuwa na ndoto kabisa. 
Mtu asiye jitambua ni sawa na kipofu wa kuzaliwa  anaye bishana na mwenye macho kuhusu uzuri wa mwezi. 

UVIVU. Hii hali inawakumba wengi sana, mtu anaweza kuwa ana ndoto nzuri na ametengeneza mazingira ya kuifikia ndoto yake. .  Ila akawa mvivu. 
Mtu mvivu hupenda mambo rahisi, huyu ni mtu anaye tamani kufanya biashara isiyo na changamoto, ni mtu anayetamani awe kwenye mahusiano ya kutimiza kila a nachohitaji. 
Mtu mvivu hujikuta ameacha ndoto yake na kuingia kwenye ndoto ya msimu kwa lengo la kutafuta urahisi. 

KUKATA TAMAA. Kukata tamaa mara nyingi hutokana na imani ya muhusika  , kuna mtu aliye kata tamaa  (huyu ni hatari zaidi ) na kuna mtu ambaye yupo  karibu na MARAFIKI walio kata tamaa, wote hawa  wamejengwa na imani kuwa kufanikiwa ni bahati na sio juhudi. ......
Mtu wa aliye kata tamaa hawezi kuwa na ndoto ambayo ana mifano ya watu walioshindwa kupitia ndoto hiyo. ......hivyo mazingira humtengenezea ndoto ya msimu. 


         Sentensi inayochosha wengi ila ndiyo uhalisia ni hii ............................

                     " lazima kuna vitu uvipoteze ili uweze   kuifikia ndoto ya kudumu "

                            let's meet on next session!

                   See you at the top. 
             scientist Saul kalivubha                      
                    (0652 134 707 )

Thursday, 26 January 2017

NDOTO YA MSIMU -1

Nakukaribisha tena kwenye blog hii yenye kutoa elimu ya maisha,binafsi namshukuru Mungu kwa makuu yake kwangu, nina imani na wewe ni mzima.
Bado tupo mwanzo wa safari, kila anaye jitambua najua yupo makini na aendapo.

.
   KUSUDI LA SOMO.
Leo nataka tujifunze somo la,NDOTO YA MSIMU,   katika somo hili tutajifunza mambo makuu matatu.
1.MAANA YA NDOTO YA MSIMU.
2.CHANZO CHA MTU KUWA NA NDOTO YA MSIMU.
3. MADHARA YA NDOTO YA MSIMU.

    1.MAANA YA NDOTO YA MSIMU.
Ndoto, ni jumla ya picha mtu anayokuwa nayo kuhusu kesho yake, watu wengi huchanganya kati ya "ndoto"  na "malengo "
Malengo ni sehemu  ndogo ndogo ambazo mtu anapaswa kuziunganisha ili kuifikia ndoto yake.

Ndoto ya msimu ni picha ya maisha ambayo mtu huichora kwa kuchochewa na mabadiliko ya mazingira(msimu ).
NB. ....Ndoto ya msimu inaweza kubadilika na kuwa ndoto ya kudumu ila ni watu wachache sana ambao wanafurahia maisha yameyojengwa na badiliko hilo. ...wengi hujuta.

Kwa upana wa kulielewa vizuri somo hili, pitia mifano hii michache.

#  Wanafunzi wengi katika levels zote za elimu huwa wanajikuta wanatengeza ndoto zao kulingana matukio yanayofanyika shuleni,  ila baada ya siku chache kupita baada ya tukio kuisha, wanafunzi hao husahau kabisa kuwa waliweka ndoto flani. ..siku mazingira ya tukio yakijirudia ndipo wanafunzi hao hupata kumbukumbu (ndoto ya msimu hiyo ).

#Watu wengi mwishoni mwa mwaka huwa wanatengeza ndoto nyingi ili mwaka mpya waweze kuzikamilsha. ....ila mambo huwa tofauti, mwaka Ukianza mpya wanasahau kuwa kuna mambo walijiwekea kuyafanya.
Hali hiyo kuna uwezekano ikawa inasababishwa na mada kuu inayo zungumzwa mwishoni mwa mwaka. .....mwishoni mwa mwaka neno MALENGO huwa kwa wingi masikioni kwa watu, hivyo mazingira hayo humfanya mtu kutengeneza ndoto nje ya uhalisia.

#MAHUSIANO, kuna mtu humpenda mtu kulingana na mazingira, mtu huyu hujikuta moyoni mwake  anatengeneza picha juu ya mtu yule kuhusu kesho yake. ....hatari zaidi mtu huyo kulingana na uchochezi wa mazingira hujikuta anafanya AGANO la kudumu kwenye Upendo wa msimu. .....siku mazingira yale yakipotea mtu huyu ndipo anagundua yupo sehemu isiyo sahihi(ndoto ya msimu )

Nina imani kwa mifano hiyo somo limeeleweka kwa kiasi flanI.
Jiulize ,ndoto uliyonayo ni ya msimu? Kama ndio, umewahi kufikiria ni hali gani utakuwa nayo siku mazingira yameyotengeneza ndoto yako yakitoweka?
NB. ..
Kabla ya kuchukua maamuzi hakikisha umefahamu madhara ya ndoto ya msimu.



                                       See you at the top.
                                       Scientist Saul Kalivubha.
                                              0652 134707.. 

Friday, 20 January 2017

JITAMBUE 2

Nimshukuru  Mungu kwa siku nyingine hii, pia niseme asante kwake kwa uzima wako, Karibu tena kwenye blog hii kwa series ya somo letu la KUJITAMBUA.
Week iliyopita tulijifunza SIFA ZA MTU ASIYE JITAMBUA. ......kama hukupitia somo hilo ni vyema ukalipitia kabla ya kuendelea na hili la leo  (http://kalivubha.blogspot.com/2017/01/jitambue.html?m=1).

Leo nataka tujifunze sehemu zilizobaki kwenye somo letu hili. .....nazo ni MADHARA YA KUTOJITAMBUA NA JINSI YA KUTIBU UGONJWA WA KUTOJITAMBUA. ..


        2.MADHARA YA KUTOJITAMBUA.
Kutojitambua ni tatizo ambalo  limefanya wahusika wawe sehemu zisizo sahihi  (kwenye mahusiano, biashara, mafanikio n.k).
Madhara ya kutojitambua ni matokeo ya kuwa sehemu isiyo ya kwako. ......

 Madhara makubwa ambayo yanaweza beba yote kwa mtu asiye jitambua ni kutofanikiwa kwa jambo lolote, huwezi fanikiwa ikiwa hujui wapi umetoka, wapi ulipo na wapi uendapo, ili mtu afanikiwe kwa jambo lolote lazima ajue vizuri sehemu anayoenda, ikiwa haitoshi lazima mtu atambue vizuri mazingira ya kumfikisha aendapo.

Mtu asiye jitambua mara nyingi hushangiliwa na watu wavivu(watu wanaopenda sehemu rahisi )  hii humfanya mtu huyo kuendelea kufanya mambo ambayo yapo kinyume na jamii inayojitambua, hivyo mtu huyu hupoteza uaminifu. ....

  3. JINSI YA KUTIBU UGONJWA WA KUTOJITAMBUA.  
Kutojitambua huwa nasema ni ugonjwa kwa sababu kila mtu anaweza ambukizwa tabia ya kutojitambua kutoka kwenye mazingira.
Huwa ni rahisi kuzuia ugonjwa huu, ila ni Kazi kubwa sana kuutibu endapo mtu akiupata. ...hii hutokana na wagonjwa wa tabia hii kuwa wagumu kukubali kuwa ni victims.

 Ili mtu apone ugonjwa huu inabidi kwanza yeye mwenyewe atambue kuwa ni mgonjwa, kisha hatua inayofata ni zoezi la kubadili MARAFIKI. .....maana mtu asiye jitambua kuna uwezekano mkubwa hata rafiki zake hawajitambui pia.
Zoezi la kubadili rafiki huwa ni ngumu kidogo  (lina hitaji ujasiri ) Ila ndio tiba pekee ya kuaminika kwa mgonjwa wa aina hii.


Let's meet on the next week , we will be having  a new lesson termed as NDOTO YA MSIMU.



                    see you at the top
                    Scientist Saul kalivubha.

Thursday, 12 January 2017

JITAMBUE 1

 Nashukuru Mungu kwa uzima wangu, bila shaka wewe pia ni mzima wa afya. Ni utamaduni mzuri sana kuwa na ibada ya kumshukuru Mungu kwa makuu yake.

KUSUDI LASOMO
.Tukiwa bado tupo kwenye safari ya maisha nimeona vyema tujifunze somo la KUJITAMBUA. Somo hili litakuwa na sehemu tatu.

   1.SIFA ZA MTU ASIYE JITAMBUA.

  2.MADHARA YA KUTOJITAMBUA.
                        3.JINSI YA KUTIBU UGONJWA WA KUTOJITAMBUA.


Kujitambua kwa maana (definition) rahisi ni kufahamu vizuri mazingira yako, ..kufahamu mazingira yako tu haitoshi, kufahamu kwa nini upo kwenye mazingira hayo ndo Kujitambua kamili.
Kuna uwezekano kuwa watu wengi wapo maeneo yasiyo sahihi kwa sababu tu hawajitambui, na wataendelea kuwa maeneo hayo sababu  ya tatizo la kutofanya TASMINI.


                         SIFA ZA MTU ASIYE JITAMBUA

Kutojitambua
ni tatizo ambalo wengi wetu tunalo,ila ukiwa hujakutana na mazingira ya kulichochea tatizo hilo ni vigumu kuona dalili zake. ......na mara nyingi mtu mwenye tatizo hilo huwa hakubali kama analo. ....

zifatazo ni baadhi ya sifa za mtu aliye na tatizo la KUTOJITAMBUA.

KUTOKUWA NA MALENGO : hii inaweza kuwa ni sifa kuu ya mtu asiye jitambua,  neno malengo kwake anakuwa analisika tu. Kumbuka tu usipokuwa na malengo huwezi kujua usahihi wa eneo ulilopo, kila jambo kwako utaona sahihi ila mazingira yakibadilika kidogo utaona sio eneo sahihi kwako.

 KUTOKUWA NA RATIBA; mtu asiye jitambua huishi kwa ratiba za watu wengine,  kama huna ratiba ya kuongoza maisha yako ni ngumu  kuwa na mipaka ya kulinda muda wako. .....kila ratiba ya nje itakuwa inafanya mabadiliko kwako...kumbuka tu watu hupenda sehemu rahisi, kila wakiwa na free time hutafuta sehemu rahisi ya kupumzikia. ...mtu asiye jitambua huwa busy kwenye free za watu wengine.


KUWA TAYARI KUACHIA ALICHO NACHO; ..Ni jambo jema mtu kufanya tasmini na kubadili mazingira  (endapo akigundua hayupo sehemu sahihi ,ila hii ni tofauti kwa mtu asiye jitambua, ..mtu huyu yupo tayari kuacha sehemu salama na kuelekea pasipo salama,  hii mara nyingi hutokana na tabia kutojiamini (tabia ya mtu asiye jitambua ).....ni vigumu kuamini kitu ulicho nacho na wakati hujui sahihi ni kipi, na ukikosa imani na ulicho nacho just muda wote utakuwa na mawazo ya kukiacha.


KUISHI KWA MAZOEA;  mtu asiye jitambua huishi kwa mazoea, muda wote yeye anakuwa anaamini kufanya mafanikio mwisho wa safari yake,  kwa kuwa amepoteza kujitambua,mtu huyu
hana sababu za kwanini yupo  pale alipo. ....swali zuri la kujiuliza siku zote ni " upo hapo ulipo kwa sababu wengine wapo or upo kwa sababu lipo kusudi la wewe kuwepo hapo ?"


KUKOSA UVUMILIVU; mtu asiye jitambua hana uvumilivu hata kidogo, hii hutokana na kutojua  umuhimu au hasara wa alicho nacho, ni vigumu kuvumilia na huku hujui kwa nini unavumilia. ......wavumilivu ni wale wanao tambua mazingira yao vizuri.


      KUTOJITAMBUA ni ugonjwa wa kuzuia mafanikio, ugonjwa huu tafasiri yake ni sawa na msafiri ambaye huchukua maamuzi ya kupanda gari bila kujua aendapo.

.......welcome again next session on next week.

                 See you at the top.
             Scientist Saul kalivubha.
                 0652 134707